Utafiti wabaini upotofu madai ya ugaidi Tanzania

Hizb Tahrir Tanzania

JF-Expert Member
Feb 18, 2020
258
235
UTAFITI WABAINI UPOTOFU MADAI YA UGAIDI TANZANIA. NI ULE WA MTAFITI PETER BOFIN

Na Bakari Mwakangwale

Utafiti umeonyesha kuwa chokochoko zote katika suala la ugaidi, hazina na hazionyeshi uhalisia kuwa Waislamu ndani ya Tanzania wanahusika.

Hayo yamesemwa na Bw. Peter Bofin (Mu-Irish) ambaye ni mtafiti wa masuala ya ugaidi katika nchi za Tanzania, Kenya na Msumbiji ambaye pia amefanikiwa kufika kwenye maeneo yote yaliyodaiwa kutokea ugaidi katika nchi hizo.

Bw. Bofin ameyabainisha hayo Julai 2, 2020 akiongea na Mtafiti nguli wa Historia ya Tanganyika (Tanzania) Mzee Mohammed Said, alipomtembelea nyumbani kwake Magomeni Jijini Dar es Saalam.

Mzee Said amesema, alifanya mazungumzo mengi na Bw. Bofin, lakini maongezi yao zaidi yalitawaliwa na historia ya Waislamu na masuala ya ugaidi nchini Tanzania.

Mzee Said, alisema Bw. Bofin, amemfahamisha kwamba ameishi Tanzania kwa miaka 15 na kwamba utafiti wake umeonesha kuwa chokochoko zote alizokutana nazo katika suala la ugaidi, hazina chanzo kutoka kwa Waislamu ndani ya Tanzania.

Mzee Said, alisema katika maongezi yao alimueleza Mtafiti huyo kuwa Wazee wa Kiislamu walipigania haki yao ya kuwa huru kutoka kwa Mkoloni chini ya TANU na hawakunyanyua silaha, bali waliwaunganisha wananchi wote bila ya kujali dini na kabila zao kuondoa dhulma ili haki na usawa vipatikane kwa wote.

Hapo ndipo utaona kuwa hawakumbagua Mwl. Julius Nyerere kwa Ukristo wake na walimchagua kuwa kiongozi wao, wakati Nyerere akija na kuanza siasa Dar es Salaam katika mji wa Waislamu.”

“Nikamweleza huo ndiyo msimamo wa Waislamu wengi wa Tanzania na ikiwa haki itaonekana inatendeka kwa wote, itakuwa vigumu kwa mbegu ya ugaidi kumea katika ardhi ya Tanzania. Amesema Mzee Said, akinukuu maongezi yake na Bw. Bofin.

Aidha, Mzee Said, alisema katika maongezi yao kwa pamoja walirejea Historia ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), ambapo alimfahamisha kuwa katika kudumisha amani ni muhimu kwa Serikali kusikiliza nini Waislamu walio nje ya BAKWATA, wanasema.

Mazungumzo yetu yote tulifanya kwa Kiswahili, kwani Bw. Bofin, anakifahamu vizuri, tuombe dua kuwa taarifa yake popote inapokwenda iakisi fikra nilizomweleza na isaidie katika kutafuta haki kwa nia ya kudumisha amani katika nchi yetu. Amesema Mzee Said.

Awali Mzee Said, alisema Bw. Bofin, amemueleza kuwa amesoma kila alichoandika kuhusu Waislamu Tanzania, amesoma utafiti aliofanya katika madai ya ugaidi na mauaji yaliyo tokea Jijini Tanga katika miji ya Kilindi na Handeni 2013, pia amesoma paper aliyowasilisha Chuo Kikuu cha Ibadan, Nigeria 2006 kuhusu ugaidi.

Mzee Said, alisema Bw. Bofin, amemueleza kuwa kajulishwa kwake na Prof. James Brennan wa Chuo Kikuu Cha Illinois, Urbana Champaign Marekani, ambae yeye (Mzee Said) ni rafiki yake kwa miaka mingi, ambaye pia (Prof. Brennan) ni mtaalamu wa Historia ya Tanzania, aliyeandika vitabu na paper kadhaa kuhusu Tanzania.

(Gazeti la Anuur)

Maoni:

Ikiwa hiyo ndio hali ya dhulma kwa Waislamu tuendeleeni kupaza sauti kutetea mahabusu kadiri inavyowezekana..

Hashtags
#KomeshaUkandamizajiWaKisheriaNaUtekaji (Swahili)
#StopOppressiveLawsAndAbduction (English)

hizb or.tz
 
Njoo Lindi na Mtwara uje tukueleze sisi kinachoendelea TASK FORCE HAWALALI KWA AJILI YA MI MTU ILIYO BRAIN WASHED NA UISLAM achana na huo utafiti wa maelezo ya mzee SAID kutoka kibiti hadi Mozambique tunawaswaga wajinga wajinga kama nyie.
 
Njoo Lindi na Mtwara uje tukueleze sisi kinachoendelea TASK FORCE HAWALALI KWA AJILI YA MI MTU ILIYO BRAIN WASHED NA UISLAM achana na huo utafiti wa maelezo ya mzee SAID kutoka kibiti hadi Mozambique tunawaswaga wajinga wajinga kama nyie.
Kwahiyo unapingana na utafiti
 
ugaidi ni mpango wa waarabu kuitawala dunia, na wanatumia kichaka cha din ya uislam kupandikiza fikra ovu ili wafanikishe lengo lao...

hapa tanzania ugaidi ulikua umekita mizizi 2012-2016 bt serikali wakashtuka wakawakamata na kuwatandika vibaya alafu nyie msojua kitu mnaleta tafiti uchwara zenu hapa...
 
UTAFITI WABAINI UPOTOFU MADAI YA UGAIDI TANZANIA. NI ULE WA MTAFITI PETER BOFIN

Na Bakari Mwakangwale

Utafiti umeonyesha kuwa chokochoko zote katika suala la ugaidi, hazina na hazionyeshi uhalisia kuwa Waislamu ndani ya Tanzania wanahusika.

Hayo yamesemwa na Bw. Peter Bofin (Mu-Irish) ambaye ni mtafiti wa masuala ya ugaidi katika nchi za Tanzania, Kenya na Msumbiji ambaye pia amefanikiwa kufika kwenye maeneo yote yaliyodaiwa kutokea ugaidi katika nchi hizo.

Bw. Bofin ameyabainisha hayo Julai 2, 2020 akiongea na Mtafiti nguli wa Historia ya Tanganyika (Tanzania) Mzee Mohammed Said, alipomtembelea nyumbani kwake Magomeni Jijini Dar es Saalam.

Mzee Said amesema, alifanya mazungumzo mengi na Bw. Bofin, lakini maongezi yao zaidi yalitawaliwa na historia ya Waislamu na masuala ya ugaidi nchini Tanzania.

Mzee Said, alisema Bw. Bofin, amemfahamisha kwamba ameishi Tanzania kwa miaka 15 na kwamba utafiti wake umeonesha kuwa chokochoko zote alizokutana nazo katika suala la ugaidi, hazina chanzo kutoka kwa Waislamu ndani ya Tanzania.

Mzee Said, alisema katika maongezi yao alimueleza Mtafiti huyo kuwa Wazee wa Kiislamu walipigania haki yao ya kuwa huru kutoka kwa Mkoloni chini ya TANU na hawakunyanyua silaha, bali waliwaunganisha wananchi wote bila ya kujali dini na kabila zao kuondoa dhulma ili haki na usawa vipatikane kwa wote.

Hapo ndipo utaona kuwa hawakumbagua Mwl. Julius Nyerere kwa Ukristo wake na walimchagua kuwa kiongozi wao, wakati Nyerere akija na kuanza siasa Dar es Salaam katika mji wa Waislamu.”

“Nikamweleza huo ndiyo msimamo wa Waislamu wengi wa Tanzania na ikiwa haki itaonekana inatendeka kwa wote, itakuwa vigumu kwa mbegu ya ugaidi kumea katika ardhi ya Tanzania. Amesema Mzee Said, akinukuu maongezi yake na Bw. Bofin.

Aidha, Mzee Said, alisema katika maongezi yao kwa pamoja walirejea Historia ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), ambapo alimfahamisha kuwa katika kudumisha amani ni muhimu kwa Serikali kusikiliza nini Waislamu walio nje ya BAKWATA, wanasema.

Mazungumzo yetu yote tulifanya kwa Kiswahili, kwani Bw. Bofin, anakifahamu vizuri, tuombe dua kuwa taarifa yake popote inapokwenda iakisi fikra nilizomweleza na isaidie katika kutafuta haki kwa nia ya kudumisha amani katika nchi yetu. Amesema Mzee Said.

Awali Mzee Said, alisema Bw. Bofin, amemueleza kuwa amesoma kila alichoandika kuhusu Waislamu Tanzania, amesoma utafiti aliofanya katika madai ya ugaidi na mauaji yaliyo tokea Jijini Tanga katika miji ya Kilindi na Handeni 2013, pia amesoma paper aliyowasilisha Chuo Kikuu cha Ibadan, Nigeria 2006 kuhusu ugaidi.

Mzee Said, alisema Bw. Bofin, amemueleza kuwa kajulishwa kwake na Prof. James Brennan wa Chuo Kikuu Cha Illinois, Urbana Champaign Marekani, ambae yeye (Mzee Said) ni rafiki yake kwa miaka mingi, ambaye pia (Prof. Brennan) ni mtaalamu wa Historia ya Tanzania, aliyeandika vitabu na paper kadhaa kuhusu Tanzania.

(Gazeti la Anuur)

Maoni:

Ikiwa hiyo ndio hali ya dhulma kwa Waislamu tuendeleeni kupaza sauti kutetea mahabusu kadiri inavyowezekana..

Hashtags
#KomeshaUkandamizajiWaKisheriaNaUtekaji (Swahili)
#StopOppressiveLawsAndAbduction (English)

hizb or.tz
Ukisikia ujinga ndiyo huu. Bofin ameongea na Said na mwandishi ni Bakari. Tutegemee mwislam aseme uislam ni ugaidi? Waliouawa Kibiti walikuwa Wakristo?

Navurugwa sana na habari za ugaidi.
 
",hazina chanzo kutoka kwa Waislamu ndani ya Tanzania."

Kwa mujibu huo ulioita kuwa ni utafiti,maana yake ugaidi tumeletewa na jamii iliopokea hapa Tz inafahamika.
 
UTAFITI WABAINI UPOTOFU MADAI YA UGAIDI TANZANIA. NI ULE WA MTAFITI PETER BOFIN

Na Bakari Mwakangwale

Utafiti umeonyesha kuwa chokochoko zote katika suala la ugaidi, hazina na hazionyeshi uhalisia kuwa Waislamu ndani ya Tanzania wanahusika.

Hayo yamesemwa na Bw. Peter Bofin (Mu-Irish) ambaye ni mtafiti wa masuala ya ugaidi katika nchi za Tanzania, Kenya na Msumbiji ambaye pia amefanikiwa kufika kwenye maeneo yote yaliyodaiwa kutokea ugaidi katika nchi hizo.

Bw. Bofin ameyabainisha hayo Julai 2, 2020 akiongea na Mtafiti nguli wa Historia ya Tanganyika (Tanzania) Mzee Mohammed Said, alipomtembelea nyumbani kwake Magomeni Jijini Dar es Saalam.

Mzee Said amesema, alifanya mazungumzo mengi na Bw. Bofin, lakini maongezi yao zaidi yalitawaliwa na historia ya Waislamu na masuala ya ugaidi nchini Tanzania.

Mzee Said, alisema Bw. Bofin, amemfahamisha kwamba ameishi Tanzania kwa miaka 15 na kwamba utafiti wake umeonesha kuwa chokochoko zote alizokutana nazo katika suala la ugaidi, hazina chanzo kutoka kwa Waislamu ndani ya Tanzania.

Mzee Said, alisema katika maongezi yao alimueleza Mtafiti huyo kuwa Wazee wa Kiislamu walipigania haki yao ya kuwa huru kutoka kwa Mkoloni chini ya TANU na hawakunyanyua silaha, bali waliwaunganisha wananchi wote bila ya kujali dini na kabila zao kuondoa dhulma ili haki na usawa vipatikane kwa wote.

Hapo ndipo utaona kuwa hawakumbagua Mwl. Julius Nyerere kwa Ukristo wake na walimchagua kuwa kiongozi wao, wakati Nyerere akija na kuanza siasa Dar es Salaam katika mji wa Waislamu.”

“Nikamweleza huo ndiyo msimamo wa Waislamu wengi wa Tanzania na ikiwa haki itaonekana inatendeka kwa wote, itakuwa vigumu kwa mbegu ya ugaidi kumea katika ardhi ya Tanzania. Amesema Mzee Said, akinukuu maongezi yake na Bw. Bofin.

Aidha, Mzee Said, alisema katika maongezi yao kwa pamoja walirejea Historia ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), ambapo alimfahamisha kuwa katika kudumisha amani ni muhimu kwa Serikali kusikiliza nini Waislamu walio nje ya BAKWATA, wanasema.

Mazungumzo yetu yote tulifanya kwa Kiswahili, kwani Bw. Bofin, anakifahamu vizuri, tuombe dua kuwa taarifa yake popote inapokwenda iakisi fikra nilizomweleza na isaidie katika kutafuta haki kwa nia ya kudumisha amani katika nchi yetu. Amesema Mzee Said.

Awali Mzee Said, alisema Bw. Bofin, amemueleza kuwa amesoma kila alichoandika kuhusu Waislamu Tanzania, amesoma utafiti aliofanya katika madai ya ugaidi na mauaji yaliyo tokea Jijini Tanga katika miji ya Kilindi na Handeni 2013, pia amesoma paper aliyowasilisha Chuo Kikuu cha Ibadan, Nigeria 2006 kuhusu ugaidi.

Mzee Said, alisema Bw. Bofin, amemueleza kuwa kajulishwa kwake na Prof. James Brennan wa Chuo Kikuu Cha Illinois, Urbana Champaign Marekani, ambae yeye (Mzee Said) ni rafiki yake kwa miaka mingi, ambaye pia (Prof. Brennan) ni mtaalamu wa Historia ya Tanzania, aliyeandika vitabu na paper kadhaa kuhusu Tanzania.

(Gazeti la Anuur)

Maoni:

Ikiwa hiyo ndio hali ya dhulma kwa Waislamu tuendeleeni kupaza sauti kutetea mahabusu kadiri inavyowezekana..

Hashtags
#KomeshaUkandamizajiWaKisheriaNaUtekaji (Swahili)
#StopOppressiveLawsAndAbduction (English)

hizb or.tz
Eti dar ni mji wa "waislam" waislam ndio waliopigania uhuru,wakati wa Tanganyika wa mikoa mingine wakiwa wamelala!!!
Kinjekitile,Mkwawa,Mirambo,Mangi sina,Mtemi Isike,
Ebu tuambieni wale waliopigana vita ya majimaji,walikuwa wanaswali masjid gani?!!
Kwa masimulizi ya namna hii,basi Hata South Africa,uhuru umeletwa na wakristo,maaana wengi wa wapigsnia uhuru wana majina ya kikristo Mandela,Steve biko,Desmond tutu,
 
Hayo mazungumzo yao hayana manufaa kwa mustakabali wa nchi, ugaidi hauonekani mdomoni au usoni, ugaidi ni jambo la siri linaloanzia moyoni kwa mtu mmoja na kisha kusambaa.

Hakuna mtu/binadamu atakayekwambia sisi familia yetu ni majambazi au tunauza bunduki za kuulia tembo NO!.
 
Utafiti uelezeee haya matukio yaliyotokea ni nn?

Kwann yanahusianishwa na Waarabu ( maana dini ni safi)

Dini haina ukatili lkn kabila Lina ukatili wa kutisha.
 
ugaidi ni mpango wa waarabu kuitawala dunia, na wanatumia kichaka cha din ya uislam kupandikiza fikra ovu ili wafanikishe lengo lao...

hapa tanzania ugaidi ulikua umekita mizizi 2012-2016 bt serikali wakashtuka wakawakamata na kuwatandika vibaya alafu nyie msojua kitu mnaleta tafiti uchwara zenu hapa...
Kati ya mtafiti anayeaminika na wewe usiyejua hata kisawahili vizuri unadhani Nani anapaswa kufuatwa?
 
Foolish and childishness research. It worth be referred as someone opinion not research report
Thanks but not even worthy to be called an opinion but "A fool's opinion" Full Stop. Ukiona jina Bakar au Ally jua kuwa tiyari tunalishwa sumu tu. Ni watu wasotosheka. Ni watu wa ile hadith ya ngamia kuomba kuweka o pua kwa hema hadi alipoomba aweke mkia na hema ikaanguka wote wakafa baridi. Jus see what is going on with the muungano. They are never satisfied
 
Back
Top Bottom