GeniusBrain
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 4,315
- 306
Jana katika gazeti la Tanzania Daima , ukurasa wa mbele kabisa kulikuwa na kichwa cha habari ' Dk Slaa kinara wa urais 2015'. Habari hii, ilionyesha utafiti ambao ulifanywa na Jamii Forum.
Katika hali kushangaza, utafiti huu umeonyesha waliochangia mawazo yao hawazidi hata watu 1,500 kati ya watanzania takriban zaidi ya million 45. (hii ni sawa na asilimia 0.0033).
Utafiti huu umepondwa kwa sababu zifuatazo
1. Idadi ya uwakilishi wa walio ulizwa ni ndogo mno mno mno sana, kiasi cha kwamba huwezi kujumuisha mawazo ya watu ambao hata asilimia 1 haijafika , ukasema matokeo yako ni sahihi
2. Imekuwa ikitanabahishwa kuwa JF ni mtandao wa CDM, na imedhihiri hivyo. Sasa kwa mintarafu hiyo, huwezi ukafanya utafiti kwenye mtandao wako na wewe mwenyewe unaumiliki na watu wakauamini . Ile dhana ya uwazi inakosekana kwa maana hiyo.
Kwa sababu hizo pamoja na nyingineo ambazo zinatakiwa ili utafiti uwe bora, hazikupatikana kwenye utafiti huu. Kwa hivyo basi, twaweza sema ni utafiti wakukurupuka na wakimagumashi.
Katika hali kushangaza, utafiti huu umeonyesha waliochangia mawazo yao hawazidi hata watu 1,500 kati ya watanzania takriban zaidi ya million 45. (hii ni sawa na asilimia 0.0033).
Utafiti huu umepondwa kwa sababu zifuatazo
1. Idadi ya uwakilishi wa walio ulizwa ni ndogo mno mno mno sana, kiasi cha kwamba huwezi kujumuisha mawazo ya watu ambao hata asilimia 1 haijafika , ukasema matokeo yako ni sahihi
2. Imekuwa ikitanabahishwa kuwa JF ni mtandao wa CDM, na imedhihiri hivyo. Sasa kwa mintarafu hiyo, huwezi ukafanya utafiti kwenye mtandao wako na wewe mwenyewe unaumiliki na watu wakauamini . Ile dhana ya uwazi inakosekana kwa maana hiyo.
Kwa sababu hizo pamoja na nyingineo ambazo zinatakiwa ili utafiti uwe bora, hazikupatikana kwenye utafiti huu. Kwa hivyo basi, twaweza sema ni utafiti wakukurupuka na wakimagumashi.