Utafiti wa REDET wampa KIKWETE 71% Dk. Slaa 12%

HALISI
please come out ututhibitishie hizi taarifa maana naona kama ni bandiko tu lisilo na depth ndani yake pls


Kwa sisi wanasayansi result hiyo hatuwezi kuipinga kwa kuwa research methodology hatujaambiwa ikoje... Kama sample ni wajumbe wa NEC ya CCM, au Wafanyakazi wa TBC1 inawezekana kabisa kupata matokeo hayo ya JK %88. Tusubiri watangaze watuambie sample size ilikuwaje ndo tuanze kujadili, vinginevyo tutapoteza muda bure. Na wanajua kabisa kuwa researchers Tanzania siku hizi ni wengi na pia future ya taasisi hiyo inategemea uadilifu so njaa zao za kujikomba ili wakombolewe na JK leo itawanyima kula kesho
 
Wamegawa khanga na mafulana. Wamezomewa. Itakuwa REDET ambayo Watanzania hawaelewi hata maana yake.

Mwaka huu mutaisoma!!
 
Kwa sisi wanasayansi result hiyo hatuwezi kuipinga kwa kuwa research methodology hatujaambiwa ikoje... Kama sample ni wajumbe wa NEC ya CCM, au Wafanyakazi wa TBC1 inawezekana kabisa kupata matokeo hayo ya JK %88. Tusubiri watangaze watuambie sample size ilikuwaje ndo tuanze kujadili, vinginevyo tutapoteza muda bure. Na wanajua kabisa kuwa researchers Tanzania siku hizi ni wengi na pia future ya taasisi hiyo inategemea uadilifu so njaa zao za kujikomba ili wakombolewe na JK leo itawanyima kula kesho
The Following User Says Thank You to Ulukolokwitanga For This Useful Post:

Msanii (Today)​
 
Utoto huo labda kama sample ilikuwa kwa ndugu zake Kikwete ingewezekana.
 
Naungana na Mwanakijiji
Uchaguzi wauhairishe tu maana kuna kila kigezo cha UPUMBAVU ndani yake.

Watu wazima wanafanya mambo utadhani hawajaacha ziwa


Na wenyewe walichotaka ni kufanya damage kama hii na inaelekewa wanatak kufanikiwa kwako na kwa mwnakijiji ALUTA CONTINUAAA!!!!
 
chee!
hivi kuna mwanaJf yoyote aliyewahi kuhojiwa na hawa jamaa?mi sijuhi huwa wanawahoji akina nani,maana sijawahi kumsikia/kumuona mtu aliyekutana nao.I think wanapika data tu!
 
Uchaguzi huu kweli Dr Slaa kaleta mambo!!! CCM wanajaribu ku-fire through all cylinders: Synovate (walikwama wako kimya) halafu JWTZ, sasa ni hii Redet ya Mkandala. Next.....
 
Huu ni utafiti uliofanywa ndani ya kamati kuu ya sisiemu na si kwa watu mbalimabli so sioni tatizo hapa isipokuwa kwamba hata ndani ya NEC bado kuna watu hawamuungi mkono mgombea wao mpendwa!
 
Ukitaka kujua ni uongo jiulize wewe binafsi umeshiriki katika utafiti huo kama hapa jukwaa zima hamna aliyeshirikishwa basi ni takwimu za kupikwa hizo

Na ule unaodaiwa na Slaa kuwa Synovate wanauficha wewe ulishiriki? Kweli nyani haoni kundule jamani. :tonguez:
 
Ni vizuri tukapewa design na methodology ya utafiti huu. Pia, ni vizuri tukajua analysis ilivyofanyika. Kwa sababu kama methodology au design ni mbovu basi na matokeo ni mabovu. Mfano, tukiambia data collection methods, say, questionnaire tungejaribu kuangalia kama kuna lead questions. Pia, sampling procedure ni muhimu sana - je sample ilikuwa ya kutosha, je sample hiyo imetoka kwenye 'voters' register'? Kama wamewauliza na under 18 basi matokeo sio sahihi!

Kwa kifupi, kama sample yao haikutoka kwenye "voters' register" hilo ni tatizo. Pili sampling technique iliyotumiwa - kwa sababu kuna kuna uwezekano wa kukikosa kizazi kipya, vyama pinzani.
 
Hiyo ni taarifa ya utafiti waliofanya REDET. Ipokeeni na ichambuliwe kisomi bila jaziba. Nawaomba wachangiaji wasome kwa makini na walete hoja. Mathalani sample size iliyotumiwa ni watu 2568. Je sample size hiyo ni representative ya wapiga kura wa nchi hii. Hakuna mahala popote ndani ya ripoti hiyo ulinganifu huo umezungumziwa. kwa mantiki hiyo Ripoti hiyo inatoa viashiria vya mwelekeo wa upepo wa kisiasa kama walivyouona wao mwezi septemba 2010. Mwezi mmoja au hata Wiki katika Kampeni za kisiasa inatosha kubadiri upepo. Kwa hiyo kama wachangiaji walivyoshauri kuwa pande zote zinazohusika ziyachukue matokeo ya utafiti huo kama changamoto. Watakaobweteka shauri yao. Oktoba 31 Mwaka 2010 ndiyo Mwamuzi. Kaza buti muda unayoyoma.

Kwa sample ya 2568 sidhani kama inatakiwa kujadiliwa na great thinkers, watuambie na characteristics of the sample pia... Lakini hapa JF kuna poll yenye sample size 8870 na imemgalagaza vibaya mno JK so hatudanganyiki kiurahisi.
 
Wapiga kura ni milioni 19, sample iliyotumika ni watu 2,568. Je imetokana na waliomo kwenye daftari la wapiga kura? Procedure ya kupata sample hiyo ni ipi? Usanii huo! Ripoti hii ni sawa na matamshi ya Shimbo!
 
Jamani REDET mnaaibisha kutoa tafiti ya uongo,kwa hali ilivyo sasa matokea ya kura ya maoni tu,ya wananchi wa kawaida inaonyesha hawa wagombea wawili wanakabana koo,lakini ukweli halisi tutaupata hapo oktoba 31,

Lakini REDET kuweni makini mnaabisha na kufedhehesha taaluma zenu,siku zote tafiti zina base kwenye facts,

Kwa ufupi nyie REDET ni CCM,hiyo kazi waachie wengine

Elisante
 
Kwa sample ya 2568 sidhani kama inatakiwa kujadiliwa na great thinkers, watuambie na characteristics of the sample pia... Lakini hapa JF kuna poll yenye sample size 8870 na imemgalagaza vibaya mno JK so hatudanganyiki kiurahisi.

Labda utujuve nini maana ya sample na ni kitu kinafanya sample ya JF kuwa ya kuaminika na sio ya REDET???
 
REDET NI KAMA MKIA WA NG'OMBE KILA UTINGISHWAPO UNATINGISHIKA

REDET SASA WANAKULA MAKOMBO YA MSALANi KWA CCM
 
Back
Top Bottom