Utafiti wa mpya wa Kisayansi uliochapishwa jana wathibitisha Rais Magufuli alikuwa sahihi kutoweka katazo la kutoka nje "lockdown"

Mtu Mzima

JF-Expert Member
Oct 4, 2007
394
124
Utafiti mpya kabisa wa kisayansi uliochapishwa jana kwenye Jarida la Sayansi la BMJ (BMJ 2020;371:m3588 ) umethibitisha kuwa JPM alikuwa sahihi kutowafungia watu kwa sababu ya corona.

Utafiti huo unaonyesha kuwa kuwafungia watu kunaongeza madhara zaidi ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya vifo pamoja na ugonjwa kuendelea kuwepo ndani ya jamii na kusababisha milipuko ya kujirudia ya ugonjwa huo.

Utafiti huo umefanyika Uingereza na umefanywa na watafiti toka chuo kikuu cha Edinburgh kilichopo nchini humo na matokeo yake kuchapishwa jana (October 7, 2020).

Soma zaidi utafiti huo hapa
na kiambatanisho (full paper)
 

Attachments

  • bmj.m3588.full.pdf
    545.7 KB · Views: 20
Mbona nchi kibao hazijawaweka wananchi wao lockdown na wala haijawa ishu mpaka kufikia hatua hizi za kuona kama jamaa kama kafanya miujiza!!
Kusifia kilicho chako Kwanza kabla ya kusifia Cha wengine sio Jambo baya.
 
..Umesahau wakati covid19 imeingia nchini Jiwe alikwenda kujificha Chato kwa siku zaidi ya 40?
Lakini baada ya kurudi aliwaambia msivae barakoa korona haiui na mkafanya alichosema. Umekufa kwa korona kisa hukufungiwa lockdown?
 
Magufuli huyu huyu aliyejichia Chattle kwa majuma 6 wakati Watanzania wanakufa?

Utafiti mpya kabisa wa kisayansi uliochapishwa jana kwenye Jarida la Sayansi la BMJ (BMJ 2020;371:m3588 ) umethibitisha kuwa JPM alikuwa sahihi kutowafungia watu kwa sababu ya corona.

Utafiti huo unaonyesha kuwa kuwafungia watu kunaongeza madhara zaidi ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya vifo pamoja na ugonjwa kuendelea kuwepo ndani ya jamii na kusababisha milipuko ya kujirudia ya ugonjwa huo.

Utafiti huo umefanyika Uingereza na umefanywa na watafiti toka chuo kikuu cha Edinburgh kilichopo nchini humo na matokeo yake kuchapishwa jana (October 7, 2020).

Soma zaidi utafiti huo hapa
na kiambatanisho (full paper)
 
Lakini baada ya kurudi aliwaambia msivae barakoa korona haiui na mkafanya alichosema. Umekufa kwa korona kisa hukufungiwa lockdown?

..Amiri Jeshi Mkuu hapaswi kuwakimbia wananchi wake wakati wa vita.

..Binafsi nawakubali Ummy Mwalimu na Dr.Ndugulile, hawa walikuwa nasi wakati tukipambana na korona.
 
Rais wa Dunia

Mfano wa kuigwa
Usomi wake wa Chemistry.. umeokoa Taifa na janga hili.. ambalo bado linaua wengi huko nchi zingine.. R.I.P. waliotangulia

Kwa kweli JPM ni chaguo la Mungu kwetu

2020 💚💛💛💚💛💛💚
 
..Umesahau wakati covid19 imeingia nchini Jiwe alikwenda kujificha Chato kwa siku zaidi ya 40?
Kule mzee alienda kuvaa uhalisia wake na kufanya makeke mpaka covid 1 kasepa,huyu mzee unaambiwa yuko fit pande zote ndio maana TL anajamba jamba tu unaambiwa wamemsusia ili abebe lawama za kupata kura chache maana jamaa ndani ya chama ana ujuaji mwingi sana na kujifanya yeye ndio msomi kuliko mwenyekiti.
 
Back
Top Bottom