Utafiti: Nyumba za kupanga zinavyoharibu akili

Elitwege

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
5,154
10,809
Kama unaishi nyumba za kupanga zenye masharti lukuki hii inakuhusu sana, wataalamu wa afya ya akili na wanasaikolojia wameonya kuwa masharti hayo ni moja ya kichocheo cha mtu kukumbwa na magonjwa ya afya ya akili ikiwemo sonona.

Takwimu za magonjwa ya afya ya akili kwa mwaka jana kutoka Wizara ya Afya zinaonyesha Watanzania milioni saba wana matatizo ya afya ya akili, huku Mkoa wa Dar es Salaam ukionekana kinara na idadi kubwa ya watu wenye matatizo hayo.

Kauli ya wataalamu hao inakuja wakati Debora Maiko mkazi wa Mbezi Afrikana Dar es Salaam, akisimulia mama mwenye nyumba wake kumkataza kuamka alfajiri kabla yake na wakati mwingine haruhusiwi kutoka ndani hadi mama huyo amwage maji barazani.

Akizungumza hivi karibuni na Mwananchi Debora alisema jambo la ajabu katika mkataba mama huyo hakuainisha masharti hayo, pia hakuna mpangaji anayeruhusiwa kupiga nyimbo za dini au kutoka nje kabla ya mama huyo kuamka.

Alisema kunapotokea hali ya kukiuka utaratibu huo, mwenye nyumba hutishia kusitisha mkataba kwa madai kuwa mtenda tukio anamuharibia mambo yake.

Kauli ya Debora ianungwa mkono na Sophia Urasa mkazi wa Mabibo anayeshangazwa na masharti ya jirani yao asiyepangisha vijana waliooa ndani ya nyumba yake au familia yenye mtoto mchanga kuishi kwake.

Daktari Idara ya Afya ya Akili, kutoka Hospitali Rufani Kanda ya Mbeya, Dk Raymond Mgeni alisema vitisho na masharti kandamizi anayotoa mmiliki wa nyumba kwa mpangaji wake humsababishia mpangaji kupata msongo wa mawazo ambao huchangia mtu kuingia katika kundi la magonjwa ya akili ikiwemo sonona.

“Mwenye nyumba anapoweka masharti magumu bila kufahamu aina ya watu anaowapangisha aidha ni wanafunzi, mtu mwenye kipato chenye kutia shaka, anayepitia changamoto ya mahusiano au kodi kwa pamoja vinamuingiza mtu huyo katika sonona,’’ alisema.

Nyumba za kupanga zinavyoharibu akili | Mwananchi - Nyumba za kupanga zinavyoharibu akili
 
Alafu wawe hawanashuguli ya kufanya wenzangu na mm...
Akili mawazo yao kodi tu...shida haziishii

Ova

Hawachelewi kuingia chumbani kuja kukagua.

Mara uambiwe wageni hawaruhusiwi

Mda mwengine unaambiwa kuingia ndani mwisho saa 5.

Unaweza kuambiwa Singles hawaruhusiwi, wengine watoto hawataki, wengine hawataki partners.

Kupamgiwa Zam za usafi wakati mwenye nyumba anaishi humo humo yeye hajipangii hizo zam.

Mwenye nyumba kuja kukupiga virungu na mikopo, wakati wewe ukichelewa klipa kodi wiki tu amekuhamisha.

NIliwahi letewa kesi kuwa mwenye nyumba anasema sisalimi majira wake.

Kwa kweli ni hatari sana.
 
Unajua binadamu tunatofautiana pakubwa mno hatufanani hio ni moja, mbili kila binadamu ana tabia, utashi na akili zake binafsi.

Kila eneo lina mipaka na kila binadamu anaishi kwa mipaka. Let say, kwa mfano: wewe ni mwenye nyumba umepangisha mdada/binti wa makamo tufanye ana umri wa miaka 21 ambae anaishi bila mume namaanisha hajaolewa, vyumba vyenu vimepaka kimshazari dirisha lake na dirisha lako yanaangaliana kwa kuangaliana akitoka ndani anapitia dirishani kwako na ukitoka unapitia dirishani kwake kwa hio anachofanya ndani unasikia na unachofanya ndani anasikia hata akisogeza sahani unasikia, siku yeye anaamua kuja kuingiza mwanaume ndani (kumbuka hajaolewa) inageuka kua kero, kwanza wanaongea usiku mzima sauti ya mwanamke haisikiki ila sauti ya mwanaume ndio inasikika zaidi na anaongea usiku mzima as if nyumba ameijenga yeye, wanabinua binua vitanda huko ndani km wanatafuta kunguni au mende aliekatisha sebreni, mwenye nyumba anasikiliza matukio yote.

Siku ya Kwanza inapita mwenye nyumba anahisi labda ni usiku mmoja tu yamepita kumbe mwanaume anakua amefungiwa ndani kisha mwanamke anaingia kwenye mizunguko yake. Jioni ikifika mwanamke akirudi anamfungulia mwanaume upuuzi unaanza upya mwanaume anaongea usiku mzima kelele tupu.

Siku ya pili inapita mwenye nyumba anahisi labda ni usiku wa pili tu mwanaume atakua ameondoka, inafika jioni kumbe mwanaume bado yupo amefungiwa ndani. Mwanamke anaporudi upuuzi ni ule ule unaanza upya mwanaume anaongea yeye anacheka yeye km nyumba ameijenga yeye. Wakati kabla mwanaume hajaja dada wa watu alikua na nidhamu, mtiifu na mkimya na hapakua na kelele zozote.

Siku ya tatu, mwenye nyumba anajua labda mwanaume ameondoka kumbe bado mwanaume kafungiwa ndani analala tu siku nzima, ikifika jioni mwanamke anamfungulia anaenda kuoga na yeye anaoga wanakula chakula kisha upuuzi unaanza upya, kelele usiku mzima mwanaume anaongea yeye tu ni kelele tupu.

Sasa mtu km huyu umempangisha ukimchukulia hatua utakua unakosea ukiwa km wewe ndio mwenye nyumba?

Nawasilisha..
 
Back
Top Bottom