Utafiti: Joto la laptop linaunguza korodani na hivyo kuharibu rutuba ya mbegu za kium

Baba Mtu

JF-Expert Member
Aug 28, 2008
870
168
UTAFITI: JOTO LA LAPTOP LINAUNGUZA KORODANI NA HIVYO KUHARIBU RUTUBA YA MBEGU ZA KIUME. Posted: 19 Nov 2010 08:19 PM PST

§ Je, wewe ni mwanaume? Unayo tabia ya kutumia laptop yako ikiwa mapajani mwako? Pengine itabidi uache tabia hiyo mara moja kwani unaweza ukawa unaangamiza kizazi kijacho.
§ Utafiti mpya uliochapishwa katika jarida la Fertility and Sterility (Elsevier) unaonyesha kwamba joto la laptop ni hatari kwa sababu linaunguza korodani na hatimaye kuharibu na hata kuangamiza kabisa mbegu za kiume. Joto hilo limetajwa kuwa sababu mojawapo inayosababisha kuongezeka kwa utasa katika nchi zilizoendelea.
§ Mbegu za kiume zilizoathiriwa na joto la laptop hazina vichwa, hazina mikia na zingine zina mikia mifupi; na kwa hivyo haziwezi kuogoelea na kulifikia yai la mwanamke ili kuweza kulirutubisha. Kwa ujumla, joto la laptop linaweza kusababisha utasa wa kudumu kwa wanaume.

Ni mwogeleaji mmoja tu hodari ndiye atashinda hapa...
§ Ushauri wa watalaamu: Kama ni lazima uweke laptop yako mapajani, basi panua miguu yako. Hii inasaidia korodani zisiunguzwe na joto la laptop kwa haraka. Njia ya uhakika zaidi ni kutumia dawati au meza kila unapotumia laptop. Utafiti huu unapatikana hapa: http://www.alligator.org/news/local/article_cd027a6c-f06d-11df-8e00-001cc4c03286.html na hapa: http://www.bionews.org.uk/page_82478.asp au hapa:

CHANZO:
http://matondo.blogspot.com/2010/11...matondo+(Dr.+Matondo)&utm_content=Yahoo!+Mail

 
UTAFITI: JOTO LA LAPTOP LINAUNGUZA KORODANI NA HIVYO KUHARIBU RUTUBA YA MBEGU ZA KIUME. Posted: 19 Nov 2010 08:19 PM PST

§ Je, wewe ni mwanaume? Unayo tabia ya kutumia laptop yako ikiwa mapajani mwako? Pengine itabidi uache tabia hiyo mara moja kwani unaweza ukawa unaangamiza kizazi kijacho.
§ Utafiti mpya uliochapishwa katika jarida la Fertility and Sterility (Elsevier) unaonyesha kwamba joto la laptop ni hatari kwa sababu linaunguza korodani na hatimaye kuharibu na hata kuangamiza kabisa mbegu za kiume. Joto hilo limetajwa kuwa sababu mojawapo inayosababisha kuongezeka kwa utasa katika nchi zilizoendelea.
§ Mbegu za kiume zilizoathiriwa na joto la laptop hazina vichwa, hazina mikia na zingine zina mikia mifupi; na kwa hivyo haziwezi kuogoelea na kulifikia yai la mwanamke ili kuweza kulirutubisha. Kwa ujumla, joto la laptop linaweza kusababisha utasa wa kudumu kwa wanaume.

Ni mwogeleaji mmoja tu hodari ndiye atashinda hapa...
§ Ushauri wa watalaamu: Kama ni lazima uweke laptop yako mapajani, basi panua miguu yako. Hii inasaidia korodani zisiunguzwe na joto la laptop kwa haraka. Njia ya uhakika zaidi ni kutumia dawati au meza kila unapotumia laptop. Utafiti huu unapatikana hapa: http://www.alligator.org/news/local/article_cd027a6c-f06d-11df-8e00-001cc4c03286.html na hapa: http://www.bionews.org.uk/page_82478.asp au hapa:


I agree with you
kuna effect kubwa mimi nimeacha kuweka laptop mapajani
 
Back
Top Bottom