Melki the Storyteller
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 5,700
- 9,778
Maake kuna jibaba huwa linafaulishwa mida ya saa 2 asubuhi kwenye chumba cha mwanamke ambaye mume huondoka kwenda kazini saa 12 asubuhi!
Leo mume karudi nyumbani saa 4 kasalimu majirani na kusema kuwa tumbo linamsokota, kufika kabisha hodi, mlango umefunguliwa baada ya dk 10 kupita, mume kuingia ndani ikasikika sauti yake, "umefuata nini ndani kwangu!?" Kimya kikatawala, hakuna mtu alotoka ndani, sio mke, sio mume, sio jibaba!
Muda huu(saa 10) ndo namwona jibaba anatoka ndani ya chumba cha watu anapita katikati yetu anaenda zake
N.B: Kibarua kiliota nyasi, msije niuliza kuwa sasa hivi nyumbani natafuta nini!
Ila hii dunia bhana!