Zinduna
JF-Expert Member
- Nov 6, 2011
- 2,378
- 3,379
Jana nilikuwa nadadavua nyota ili kujua yatakayojiri mwaka 2013:
Kwa mujibu wa nyota mwaka 2013 utatawaliwa na nyota ya Mizani, hii tunaweza kuita ni nyota ya upatanisho au nyota ya usawa, lile tishio la vita kuu ya tatu ya dunia halitakuwepo tena kutokana na pande mbili za mashariki ya kati zilizoanza kugombana tangu mwaka 1947 kumaliza tofauti zao. Hata ule mgogoro uliozikumba nchi za kiarabu utakwisha na amani itarejea katika ukanda huo.
Vita kati ya serikali na waasi katika baadhi ya nchi za Africa vitamalizwa kwa njia ya amani na nchi hizo zitaimarisha demokrasia.
Dunia itakumbwa na majanga ya asili kama matetemeko ya ardhi maporomoko ya milima vimbunga na volcano itazikumba baadhi ya nchi.
Kutakuwa na tishio la ukame na njaa kwa nchi zilizopo kusini mwa Jangwa la Sahara na hiyo itasababisha wananchi wake kukimbilia katika nchi za jirani ili kuhemea, hali hiyo itasababisha taharuki kwa wenyeji .
Nikiliangalia bara la Africa kinyota, naona wingu jeusi, nasikia vilio huku na huko, naona kuna mtu mzito akiwa amelala katika jeneza, mtu huyo amekufa. Kifo chake kitaleta simanzi si kwa Afrika pekee bali kwa dunia nzima. Ni mtu ambaye anaheshimika sana. Je ni nani huyu mtu. Hakika simfahamu lakini naona ni mtu mzito.
Lakini pia kutakuwa na vifo vya wanasiasa na wasanii vitakavyolikumba bara la Africa, kwa upande wa wasanii, inasikitisha sana kwani wengi wataangamia kwa kukosa maarifa. Kwa wanasiasa vifo vyao vitatokana na mtindo wa maisha wanayoishi watu wengi wenye kipato cha kuridhisha. Ulaji wa vyakula usiozingatia afya utakuwa ni chanzo kizuri cha kuwaletea maradhi ya moyo, kisukari, shinikizo la chini na la juu la damu kitu ambacho kitawasababishia vifo.
Natabiri kiongozi mmoja wa juu kabisa katika nchi iliyoko katika bara la afrika kufariki akiwa madarakani, kupatikana kwa mrithi wake kunaweza kuitikisha nchi hiyo kidogo, lakini mambo yatasawazishwa na amani kurejea.
Pia bara za Afrika litakumbwa na mabadiliko makubwa ya uongozi, Kutaibuka kundi kubwa la vijana wakitaka kushika madaraka. Kwa zile nchi zitakazofanya uchaguzi mwakani, tutashuhudia hayo mabadiliko, lakini zile ambazo hazitafanya uchaguzi tutaona vuguvugu la vijana wakiibuka kama uyoga ili kuleta mabadiliko katika nchi zao. Iwapo viongozi watakaidi kukubaliana na vuguvugu hilo, wataziingiza nchi zao katika matataizo makubwa au hata kuziingiza katika vita, ingawa hilo sidhani kama linaweza kutokea kutokana na nyota ya Mizani kushika hatamu hapo mwakani.
Kwa mujibu wa nyota mwaka 2013 utatawaliwa na nyota ya Mizani, hii tunaweza kuita ni nyota ya upatanisho au nyota ya usawa, lile tishio la vita kuu ya tatu ya dunia halitakuwepo tena kutokana na pande mbili za mashariki ya kati zilizoanza kugombana tangu mwaka 1947 kumaliza tofauti zao. Hata ule mgogoro uliozikumba nchi za kiarabu utakwisha na amani itarejea katika ukanda huo.
Vita kati ya serikali na waasi katika baadhi ya nchi za Africa vitamalizwa kwa njia ya amani na nchi hizo zitaimarisha demokrasia.
Dunia itakumbwa na majanga ya asili kama matetemeko ya ardhi maporomoko ya milima vimbunga na volcano itazikumba baadhi ya nchi.
Kutakuwa na tishio la ukame na njaa kwa nchi zilizopo kusini mwa Jangwa la Sahara na hiyo itasababisha wananchi wake kukimbilia katika nchi za jirani ili kuhemea, hali hiyo itasababisha taharuki kwa wenyeji .
Nikiliangalia bara la Africa kinyota, naona wingu jeusi, nasikia vilio huku na huko, naona kuna mtu mzito akiwa amelala katika jeneza, mtu huyo amekufa. Kifo chake kitaleta simanzi si kwa Afrika pekee bali kwa dunia nzima. Ni mtu ambaye anaheshimika sana. Je ni nani huyu mtu. Hakika simfahamu lakini naona ni mtu mzito.
Lakini pia kutakuwa na vifo vya wanasiasa na wasanii vitakavyolikumba bara la Africa, kwa upande wa wasanii, inasikitisha sana kwani wengi wataangamia kwa kukosa maarifa. Kwa wanasiasa vifo vyao vitatokana na mtindo wa maisha wanayoishi watu wengi wenye kipato cha kuridhisha. Ulaji wa vyakula usiozingatia afya utakuwa ni chanzo kizuri cha kuwaletea maradhi ya moyo, kisukari, shinikizo la chini na la juu la damu kitu ambacho kitawasababishia vifo.
Natabiri kiongozi mmoja wa juu kabisa katika nchi iliyoko katika bara la afrika kufariki akiwa madarakani, kupatikana kwa mrithi wake kunaweza kuitikisha nchi hiyo kidogo, lakini mambo yatasawazishwa na amani kurejea.
Pia bara za Afrika litakumbwa na mabadiliko makubwa ya uongozi, Kutaibuka kundi kubwa la vijana wakitaka kushika madaraka. Kwa zile nchi zitakazofanya uchaguzi mwakani, tutashuhudia hayo mabadiliko, lakini zile ambazo hazitafanya uchaguzi tutaona vuguvugu la vijana wakiibuka kama uyoga ili kuleta mabadiliko katika nchi zao. Iwapo viongozi watakaidi kukubaliana na vuguvugu hilo, wataziingiza nchi zao katika matataizo makubwa au hata kuziingiza katika vita, ingawa hilo sidhani kama linaweza kutokea kutokana na nyota ya Mizani kushika hatamu hapo mwakani.