PROFESSOR JOACHIM
Member
- Oct 11, 2015
- 49
- 35
Kama mchambuzi wa maswala ya siasa hapa nchini nisiyekua na chama chochote, huu ndo utabiri wangu kwa siasa za nchi yetu katika miaka 10 ijayo;
CCM itashinda uchaguzi mkuu kwasababu wamesimamisha mgombea mwadilifu, mzalendo wa kweli, mchapakazi, mwajibikaji na mwajibishaji, kimsingi wamesimamisha 'masihi' wa aina yake. Ukawa itashindwa na kulalamika kua wameibiwa kura naam SIRAHA YA MUOVU YOYOTE NI UONGO. Ukawa watashindwa kwasababu wanachama wa upinzani waliochukizwa na kitendo cha ukawa kumpokea fisadi papa, wengi watampigia magufuli, naam waliokua wafuasi wa DR. SRAA na PROF. LIPUMBA wataongeza kura zao kwa Dr. Magufuli, wasomi wengi wazalendo kama mimi tuliokua tunaichukia sana ccm lakini kwa ccm kumsimamisha kiongozi mahiri na madhubuti msomi wa PhD, wengi tutaongeza kura zetu kwa TINGATINGA na kumpa ushindi.
Vyama vinavyounda ukawa yaani Chadema, cuf, nccr na nrd vitapoteza ushawishi wao kwa wananchi baada ya kushindwa vibaya katika uchuguzi mkuu. Chadema, cuf, nccr na nrd vitafifia katika ramani ya siasa nchini kama si kufutika kabisa. Hivyo wanachama wengi sana wa chadema na vyama vinavyounda ukawa watahamia ACT na CCM, hivyo CCM na ACT vitaongeza ushawishi wao kwa wananchi na kupata wafuasi lukuki kutoka ukawa. Ndipo ukawa na vyama vyake vitafutika au kufifia katika ramani ya siasa nchini huku CCM na ACT viking'aa zaidi na kuwa na ushawishi mkubwa katika siasa za tz. Hivyo kwa miaka kumi ijayo na zaidi tutabaki na vyama viwili tu vikubwa, CCM na ACT. Nini kitatokea nchin kipindi cha miaka kumi ijayo? Siasa ya nchi itabadilika kutoka siasa za matusi, vurugu, propaganda chafu n.k na kua siasa safi kwa maendeleo ya nchi. Kutokana na uongozi safi na bora wa kiongozi mahiri na madhubuti Dr. John Pombe Magufuli, viongozi watawajibika na kuwajibishwa, uchumi wa nchi utakua kwa kasi na kuimalika, nchi itaendelea mara kumi zaidi kuliko kipindi cha jakaya, na baada ya magufuli kumaliza muda wake nchi yetu itakua miongoni mwa nchi zenye uchumi mkubwa na imara barani afrika, na tutaingia katika nchi zenye uchumi wa kati.
Huu ndo utabili wangu kulingana na uzoefu wangu katika siasa za nchi yangu. Buriani chadema, buriani ukawa, buriani ufisadi, unafiki na siasa chafu. Karibu sana sana uadilifu, maendeleo kwa wote na uchumi imara na madhubuti nchini. Zaidi ya yote uchaguzi wa mwaka huu utavunja rekodi kwa kufanyika kwa amani, haki na usawa. Amani usiamini ujumbe huu utakua shahidi baada ya miezi kadhaa kwamba utabiri wangu ni kweli. MUNGU ibariki tz, Mungu mbariki Dr. J.P Magufuli, Mungu wabariki wapiga kura wenye moyo wa uadilifu na uzalendo kama mimi.
Waaibike, wafedheheke, wanaojali maslahi ya vyama vyao bila kujali maslahi mapana ya taifa letu tukufu la Tanzania. Amen.
CCM itashinda uchaguzi mkuu kwasababu wamesimamisha mgombea mwadilifu, mzalendo wa kweli, mchapakazi, mwajibikaji na mwajibishaji, kimsingi wamesimamisha 'masihi' wa aina yake. Ukawa itashindwa na kulalamika kua wameibiwa kura naam SIRAHA YA MUOVU YOYOTE NI UONGO. Ukawa watashindwa kwasababu wanachama wa upinzani waliochukizwa na kitendo cha ukawa kumpokea fisadi papa, wengi watampigia magufuli, naam waliokua wafuasi wa DR. SRAA na PROF. LIPUMBA wataongeza kura zao kwa Dr. Magufuli, wasomi wengi wazalendo kama mimi tuliokua tunaichukia sana ccm lakini kwa ccm kumsimamisha kiongozi mahiri na madhubuti msomi wa PhD, wengi tutaongeza kura zetu kwa TINGATINGA na kumpa ushindi.
Vyama vinavyounda ukawa yaani Chadema, cuf, nccr na nrd vitapoteza ushawishi wao kwa wananchi baada ya kushindwa vibaya katika uchuguzi mkuu. Chadema, cuf, nccr na nrd vitafifia katika ramani ya siasa nchini kama si kufutika kabisa. Hivyo wanachama wengi sana wa chadema na vyama vinavyounda ukawa watahamia ACT na CCM, hivyo CCM na ACT vitaongeza ushawishi wao kwa wananchi na kupata wafuasi lukuki kutoka ukawa. Ndipo ukawa na vyama vyake vitafutika au kufifia katika ramani ya siasa nchini huku CCM na ACT viking'aa zaidi na kuwa na ushawishi mkubwa katika siasa za tz. Hivyo kwa miaka kumi ijayo na zaidi tutabaki na vyama viwili tu vikubwa, CCM na ACT. Nini kitatokea nchin kipindi cha miaka kumi ijayo? Siasa ya nchi itabadilika kutoka siasa za matusi, vurugu, propaganda chafu n.k na kua siasa safi kwa maendeleo ya nchi. Kutokana na uongozi safi na bora wa kiongozi mahiri na madhubuti Dr. John Pombe Magufuli, viongozi watawajibika na kuwajibishwa, uchumi wa nchi utakua kwa kasi na kuimalika, nchi itaendelea mara kumi zaidi kuliko kipindi cha jakaya, na baada ya magufuli kumaliza muda wake nchi yetu itakua miongoni mwa nchi zenye uchumi mkubwa na imara barani afrika, na tutaingia katika nchi zenye uchumi wa kati.
Huu ndo utabili wangu kulingana na uzoefu wangu katika siasa za nchi yangu. Buriani chadema, buriani ukawa, buriani ufisadi, unafiki na siasa chafu. Karibu sana sana uadilifu, maendeleo kwa wote na uchumi imara na madhubuti nchini. Zaidi ya yote uchaguzi wa mwaka huu utavunja rekodi kwa kufanyika kwa amani, haki na usawa. Amani usiamini ujumbe huu utakua shahidi baada ya miezi kadhaa kwamba utabiri wangu ni kweli. MUNGU ibariki tz, Mungu mbariki Dr. J.P Magufuli, Mungu wabariki wapiga kura wenye moyo wa uadilifu na uzalendo kama mimi.
Waaibike, wafedheheke, wanaojali maslahi ya vyama vyao bila kujali maslahi mapana ya taifa letu tukufu la Tanzania. Amen.