Uchaguzi 2020 Utabiri wangu 2020: Ni Dr. John Pombe Magufuli (CCM) na Wakili Msomi Tundu Antipas Lissu (Upinzani) Urais. Tuwafuatilie; tuwachambue na tuwachague!

Nimefuatilia kimyakimya lakini kwa umakini mkubwa shauri la Lissu Mahakama Kuu ya Tanzania kuhusu Ubunge wake. Kuanzia siku alipowasilisha Maombi yake hadi leo ulipotolewa uamuzi wa kuyatupilia mbali mapingamizi ya awali ya Serikali, nimefuatilia.

Ukitazama muitikio wa watu kuhudhuria shauri la Lissu Mahakama Kuu; majopo yaliyoshiba ya Mawakili Wasomi wa pande zote za shauri na jinsi uamuzi wa leo ulivyopokelewa mahakamani na kwingineko, utakubaliana nami kuwa Lissu si tu ni maarufu ila ni mtu 'mzito' kwenye uga wa kisiasa wa Tanzania.

Bila kuzingatia kitakachotokea mwisho wa Maombi ya Msingi ya Lissu yanayoendelea kuishi Mahakama Kuu ya Tanzania baada ya Uamuzi wa Jaji Matupa leo wa kutupilia mbali mapingamizi ya Serikali, shauri hilo limeshatoa picha kumhusu Lissu: si mtu wa kubezwa.

Natabiri kuwa Lissu atagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2020 kupitia chama chochote cha upinzani na atakuwa mpinzani mkuu wa mgombea wa CCM ambaye natabiri atakuwa Rais wa sasa Jemedari Dr. John Pombe Magufuli.

Kwakuwa tumeshawajua, tuwafuatulie na tuwachambue uimara na udhaifu wao kwa staha na kwenye mtazamo wa kujenga nchi yetu pendwa ya Tanzania. Muda ukifika, tumchague Rais wetu wa Tanzania kwa miaka miaka mitano ijayo kuanzia mwaka 2020.

Muda ukifika na utabiri wangu kutimia, nitamchagua wa kusimama naye!


WATANZANIA AMKENI


CCM KATU HAIWEZI KUKUBALI DEMOKRASIA IFUATE MKONDO WAKE

KIHISTORIA-- CCM NI AFRO SHIRAZI + TANU

AFRO SHIRAZI haikukubali Demokrasia kufuata mkondo ake na ikatafuta msaada wa Tanu Tanganyika na kupindua matakwa ya wananchi

TANU - Baada ya kupata Uhuru , NYERERE alivifungia vyama vyote vya upinzani na kuanzisha mfumo wa Chama kimoja


KWA HALI HII CCM NI CHAMA KISICHOKUBALIANA NA MAAMUZI YA WANANCHI NA TOKEA MFUMO WA UCHAGUZI KUANZA WANAENDELEZA UHARAMIA WAO
 
Nimefuatilia kimyakimya lakini kwa umakini mkubwa shauri la Lissu Mahakama Kuu ya Tanzania kuhusu Ubunge wake. Kuanzia siku alipowasilisha Maombi yake hadi leo ulipotolewa uamuzi wa kuyatupilia mbali mapingamizi ya awali ya Serikali, nimefuatilia.

Ukitazama muitikio wa watu kuhudhuria shauri la Lissu Mahakama Kuu; majopo yaliyoshiba ya Mawakili Wasomi wa pande zote za shauri na jinsi uamuzi wa leo ulivyopokelewa mahakamani na kwingineko, utakubaliana nami kuwa Lissu si tu ni maarufu ila ni mtu 'mzito' kwenye uga wa kisiasa wa Tanzania.

Bila kuzingatia kitakachotokea mwisho wa Maombi ya Msingi ya Lissu yanayoendelea kuishi Mahakama Kuu ya Tanzania baada ya Uamuzi wa Jaji Matupa leo wa kutupilia mbali mapingamizi ya Serikali, shauri hilo limeshatoa picha kumhusu Lissu: si mtu wa kubezwa.

Natabiri kuwa Lissu atagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2020 kupitia chama chochote cha upinzani na atakuwa mpinzani mkuu wa mgombea wa CCM ambaye natabiri atakuwa Rais wa sasa Jemedari Dr. John Pombe Magufuli.

Kwakuwa tumeshawajua, tuwafuatulie na tuwachambue uimara na udhaifu wao kwa staha na kwenye mtazamo wa kujenga nchi yetu pendwa ya Tanzania. Muda ukifika, tumchague Rais wetu wa Tanzania kwa miaka miaka mitano ijayo kuanzia mwaka 2020.

Muda ukifika na utabiri wangu kutimia, nitamchagua wa kusimama naye!
Lissu si chochote si lolote. Msipoteze muda kumjadili.
 
Nimefuatilia kimyakimya lakini kwa umakini mkubwa shauri la Lissu Mahakama Kuu ya Tanzania kuhusu Ubunge wake. Kuanzia siku alipowasilisha Maombi yake hadi leo ulipotolewa uamuzi wa kuyatupilia mbali mapingamizi ya awali ya Serikali, nimefuatilia.

Ukitazama muitikio wa watu kuhudhuria shauri la Lissu Mahakama Kuu; majopo yaliyoshiba ya Mawakili Wasomi wa pande zote za shauri na jinsi uamuzi wa leo ulivyopokelewa mahakamani na kwingineko, utakubaliana nami kuwa Lissu si tu ni maarufu ila ni mtu 'mzito' kwenye uga wa kisiasa wa Tanzania.

Bila kuzingatia kitakachotokea mwisho wa Maombi ya Msingi ya Lissu yanayoendelea kuishi Mahakama Kuu ya Tanzania baada ya Uamuzi wa Jaji Matupa leo wa kutupilia mbali mapingamizi ya Serikali, shauri hilo limeshatoa picha kumhusu Lissu: si mtu wa kubezwa.

Natabiri kuwa Lissu atagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2020 kupitia chama chochote cha upinzani na atakuwa mpinzani mkuu wa mgombea wa CCM ambaye natabiri atakuwa Rais wa sasa Jemedari Dr. John Pombe Magufuli.

Kwakuwa tumeshawajua, tuwafuatulie na tuwachambue uimara na udhaifu wao kwa staha na kwenye mtazamo wa kujenga nchi yetu pendwa ya Tanzania. Muda ukifika, tumchague Rais wetu wa Tanzania kwa miaka miaka mitano ijayo kuanzia mwaka 2020.

Muda ukifika na utabiri wangu kutimia, nitamchagua wa kusimama naye!
Upo bro?!
Uchaguzi utakuwa huru na wa haki??! Tuanzie hapa!
Lissu 90%
Ukiwa uchaguzi ule ule wa miaka yote basi tunapoteza muda
 
Magufuli ilikuwa ni ajali mbaya Sana kwa taifa kumpa nafasi ya pili kwa mwendo alioliendesha taifa tunaweza kuingia kwenye machafuko maana itakuwa ngumu umma mkubwa kumvumilia Kama atapita itakuwa shida dhiki na majuto ya taifa yetu macho.
 
Hazina manufaa kwa maisha ya mwananchi mmoja mmoja

..zitakuwa na manufaa kama kweli tutafikia uchumi wa kati, na siyo ubabaishaji.

..mkulima wa jembe la mkono hawezi ku-afford usafiri wa ndege au treni ya mwendo kasi.

..pia sgr na stieglers ni miradi ya muda mrefu, inahitajika miradi ya muda mfupi na muda wa kati ambayo itawaandaa waTz kuweza kufaidika na sgr, madege, na stieglers gorge.
 
..JPM ni sgr, stieglers, na ndege.

..sasa TL au ZK itabidi waweke kete zao mezani.

..baada ya hapo ndiyo wananchi wafanye maamuzi.

JokaKuu

Huku Shinyanga, Mwanza, Simiyu na kwingineko hakuna SGR wala Stigler wala hizo ndege tunazoziona kwenye picha tu. Huku tuna reli ya Mjurumani ya tangu mwaka 1914....

Sijui watatuambia nini tu. Maana hata maisha yenyewe ni taabu na magumu maradufu kuliko ilivyokuwa miaka mitano iliyopita....

Zao la pamba lililokuwa tegemeo letu huku limekufa toka msimu uliopita kwa sababu ya utaratibu na sera mbovu za serikali ya awamu ya 5 na CCM kwa ujumla...

Kwa kifupi Mwanza na Shinyanga na Simiyu ni ileile aliyoiacha Jakaya Kikwete mwaka 2015. Nothing has changed. Hakuna kilichobadilika...!!

Hizo picha za kwenye TV ni photoshop tu za kuenezea propaganda, hakuna lolote....!!
 
Kampeni ya mara hii hakuna pushup, ni kupewa za uso tu, ukinuna, ukilia, ukidoka, ukisimama jamaa anakupa za uso tena bila gloves.
 
JokaKuu

Huku Shinyanga, Mwanza, Simiyu na kwingineko hakuna SGR wala Stigler wala hizo ndege tunazoziona kwenye picha tu. Huku tuna reli ya Mjurumani ya tangu mwaka 1914....

Sijui watatuambia nini tu. Maana hata maisha yenyewe ni taabu na magumu maradufu kuliko ilivyokuwa miaka mitano iliyopita....

Zao la pamba lililokuwa tegemeo letu huku limekufa toka msimu uliopita kwa sababu ya utaratibu na sera mbovu za serikali ya awamu ya 5 na CCM kwa ujumla...

Kwa kifupi Mwanza na Shinyanga na Simiyu ni ileile aliyoiacha Jakaya Kikwete mwaka 2015. Nothing has changed. Hakuna kilichobadilika...!!

Hizo picha za kwenye TV ni photoshop tu za kuenezea propaganda, hakuna lolote....!!

..nilishangaa watia nia wa ubunge wa ccm, wakati wa kuomba kura, wanataja matatizo badala ya kutaja mafanikio.

..na baadhi ya watia nia hao ni wa kanda ya ziwa ambao nilidhani wana ahueni kulinganisha na maeneo mengine.
 
Back
Top Bottom