Utabiri wa Mwl. Nyerere na Prof. Kabudi

Chamoto

JF-Expert Member
Dec 7, 2007
8,319
17,474
Mwl. Nyerere alikuwa na maono ya kipekee sana. Mambo mengi aliyoyaongea miaka mingi iliyopita yametokea na mengine yanaendelea kutokea. Moja ya jambo alilolisema na kutokea ni hili lililosimuliwa na Prof. Kabudi wakati wa mdahalo wa katiba 4 Aug 2014. Na haya ndiyo aliyosema Prof.Kabudi;
Na ndiyo yanayonifanya nimalize kwa kuyakumbuka maneno ya mwalimu mwaka 1993 nikiwa Berlin mwanafunzi, amekuja kumzika Willy Brandt, Willy Brandt! Tumekusanyika... alikaa... yeye na Kaunda walikaa... marafiki wakubwa wa Willy Brandt. Tukaa.. dada mmoja sitamtaja jina leo, akamuuliza, "mwalimu huko nyumbani mmeruhusuje vyama vyingi, wakati walio taka ni wachache?" Mwalimu akamtazama akacheka... akasema, "binti! We si unaishi hapa Berlin si umemuona Ceaușescu, wametungua Helicopter eh, ikadondoka eh, wakamuua yeye na mke wake... wakavuta maiti, ni kwasababu Ceaușescu alisubiri wanaomkataa wawe wengi, wakamtungua!"
.


Nimekumbua maneno haya baada ya kusikia yaliyotokea zimbabwe, kama vile yalivyotokea Libya, Egypt, Yemen, Syria, Bahrain na Ivory coast miaka ya nyuma.

Je ni mambo gani mengine mwalimu alitabiri nakuja kutokea?
 
Utabiri wa Mwalimu utatimia hapa Tanzania, kwani watu wanaoichukia CCM wanaongezeka kila uchao, wakubwa wanajaribu kuwaziba watu midomo wasiseme ukweli lakini ukweli huo unaendelea kukua ndani ya mioyo ya watu kitu ambacho bunduki na mabomu haviwezi kuuzuia.
 
Kaulize upate jibu kijana. Unajua hata bei ya vitabu wewe? Umewahi kuingia bookshop katika maisha yako?

Ungeakuwa unasoma usingelialia hovyo hapa. Wanaolia lia wote ni kula kulala tu. Hawajasoma, hawasomi hawafanyi kazi na pesa hawana. Wewe ni mmoja wao
 
the irony of pole pole speaking about "UNAFIKI"
na huyo prof nae miyeyusho sana.
 
Mwl. Nyerere alikuwa na maono ya kipekee sana. Mambo mengi aliyoyaongea miaka mingi iliyopita yametokea na mengine yanaendelea kutokea. Moja ya jambo alilolisema na kutokea ni hili lililosimuliwa na Prof. Kabudi wakati wa mdahalo wa katiba 4 Aug 2014. Na haya ndiyo aliyosema Prof.Kabudi;

.


Nimekumbua maneno haya baada ya kusikia yaliyotokea zimbabwe, kama vile yalivyotokea Libya, Egypt, Yemen, Syria, Bahrain na Ivory coast miaka ya nyuma.

Je ni mambo gani mengine mwalimu alitabiri nakuja kutokea?

Huyu si ndio waziri wa sasa wa Katiba na sheria?. Mbona matendo yake ya sasa hayaendani na maneno yake ya wakati huo.
Au ndo utapeli uleule tunaofanyiwa na wasomi wetu wanapokuwa na njaa wanapiga kelele sana kuikosoa serikali wakionjeshwa kimya serikali inakuwa malaika
 
Wa sasa sijui anasoma vitabu gani maana Dah!
We Sasa anapitia Font Fed kuangalia kama Bashite kaandikwa. Akikuta hajaandikwa anashikwa hasira na kupiga simu kwa wahariri. Huku akiamuru kuvunjwa kwa majengo
 
Back
Top Bottom