Utabiri: Tanzania kwenda total lockdown mwezi April

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,824
35,827
Wakuu huu ni utabiri tu si kama ile ndoto ya mheshimiwa Lema hivyo nadhani si haba kuuweka hadharani.

Utabiri huu unazingatia ukweli kuwa serikali ya awamu ya tano imesheheni wasomi wazamivu na wasomi wabobezi kweli kweli. Kwa ma PhD na ma Profesa wote wale chini ya mkuu mwenyewe ambaye pia ni daktari itakuwa 'too naive' na kutokujitendea haki kudhani kuwa hajui wala hawajui nini cha kufanya kuuzuia na kuutokomeza ugonjwa huu.

Haya ya uchaguzi mkuu kuwa uko palepale ni geresha tu katika jitihada za kutupatia cha kuongelea wakati April anasubiriwa kwa hamu mno aje.

Hapa tulipo ni vyema kujua kuna kinachosubiliwa tu (ambacho ni top secret). Mara kitakapojiri jitihada za kumdhibiti na kumtokomeza kirusi huyu ndipo kitaanza sasa.

"Cha kusikitisha tu ni kuwa katika hii subiri subiri kuna watu itawagharimu maisha pia gharama zitakuwa kubwa zaidi", anasema Cyril Ramaphosa Rais wa Afrika kusini.

NB: Huu ni utabiri tu pasi na kuwa Kibwetere wala Mwampesa.
 
.yaani huo utabiri wako kamwe hautatimia ..
Tunaendelea kudunda..
Hakuna lock down NA CORONA SI MUDA INAISHA.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kumbe ni wewe? Wayakumbuka haya?

Nilichukua muda kidogo kukuelimisha nikidhani unaweza kutambua hatari ilivyo na fursa zilipo kwenye gonjwa hili.

Sinao muda mwingi wa kupoteza na mtu asiyeelewa wala kuwa na nafasi ya kujifunza akaelewa.

Si unajua akili zote kubwa na ndogo zimeumbwa na maulana?

Ukipenda rejea mabandiko yangu yote.

Ningependa mno binafsi na familia yangu, wewe na yule tukanusurika na janga la ugonjwa huu. Hilo halitatokea kwa kukaa tu au kwa hatua zozote zilizopo sasa.

Utanikumbuka kitakapo nuka sawa sawa.

Kwa heri ya kuonana.

Sina mpango wa kutwanga maji kwenye kinu.

Kwa heri ya kuonana.
 
Iliyokuwa top secret kwa serikali kutokuchukua hatua in March yaweza kuwa ni hii:


Yaonyesha alikuwa kapanga kuwakamua vilivyo walipa kodi kwanza. Mengine yote (uchaguzi mkuu nk) yalikuwa geresha tu.

Hata hivyo tutampongeza mno kwa kwenda total lockdown bila ya kuchelewa zaidi.

Rwanda wanabakiza siku 2 za lockdown the process is worth and doable. Tayari kasi ya maambukizi imeshaanza kupungua.

Kasi ya maambukizi Afrika kusini imeshaanza kupungua pia kufuatilia total lockdown.


Source: Kwa hatua hii ya BOT, naamini Sasa Magufuli naye Ameelewa COVID-19 is serious, tujiandae kwa Curfew/lockdown - JamiiForums
 
Unasema rwanda maambukizi yamepungua?.
Wakati wapo 75.
Na lock down yao.
Unadhani wakimaliza hyo lock down ndo CORONA ITAKUWA IMEISHA au wataongeza siku nyingine?
Iliyokuwa top secret kwa serikali kutokuchukua act in March yaweza kuwa ni hii:


Yaonyesha alikuwa kapanga kuwakamua vilivyo walipa kodi kwanza. Mengine yote (uchaguzi mkuu nk) yalikuwa geresha tu.

Hata hivyo tutampongeza mno kwa kwenda total lockdown bila ya kuchelewa zaidi.

Rwanda wanabakiza siku 2 za lockdown the process is worth and doable. Tayari kasi ya maambukizi imeshaanza kupungua.

Kasi ya maambukizi Afrika kusini imeshaanza kupungua pia kufuatilia total lockdown.


Source: Kwa hatua hii ya BOT, naamini Sasa Magufuli naye Ameelewa COVID-19 is serious, tujiandae kwa Curfew/lockdown - JamiiForums
20200401_064229.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tb Joshua alitabiri corona ingeisha tar 27/03/2020.....
Labda nabii tito atatutabiria vizuri
 
Lockdown ya wanafunzi ndio ya pekee. Yotal lockdown nyingine hamna. Sasa hivi ni measures za kujiepusha ndio zatiliea mkazo. Mfano sanitaiza na kuosha mikono pamoja na hili la levo siti ktk daladala na makampuni kufanya kazi kwa shift imepunguza msongamano.

Na katika hili mpaka sasa tumefanikiwa. Watu wanapata mkate wao wa kila siku ila kwa tahadhali, tukifungiwa ndani kwa watanzania wengi itakuwa chaos, familia nyingi ni wazazi/ walezi wametoka kwenda tafuta na hela wanayopata leo kesho inalisha familia. Serikali imefikiria hilo pia.
 
Back
Top Bottom