Utabiri: Bernie Sanders Ndiye Rais Ajaye Wa Marekani

Chamoto

JF-Expert Member
Dec 7, 2007
8,319
17,474
Bernie Sanders ndiye atakayekuja kuwa Rais wa 46.

Kuna vita Marekani kati ya matajiri na masikini, mfumo uliopo sasa unakandamiza sana watu wa kawaida. Pengo kati ya matajiri na wafanyakazi limezidi kuongezeka. Mfano, watu watatu matajiri kabisa wanautajiri mkubwa kuliko nusu ya wananchi wa kawaida.

Matajiri wa kupindukia wamezidi kuongeza utajiri wao na hivyo kuhakikisha hali hiyo ikiendelea. Wanafanya hivi kwa kuwatumia wanasiasa kupitisha sheria zinazotungwa kila kukicha ili waendelee kujilimbikizia mali.

Wafanyakazi wa kawaida wanaendelea kuzidi kuwa masikini, kwa kuwa gharama za maisha zimeongezeka, huku vipato vikibaki vile vile. Moja ya gharama kubwa za maisha ni afya ambapo bima za afya zimezidi kuongezeka. Makampuni ya madawa yanaweka gharama juu sana ili hisa za makampuni hayo ziongezeke na hivyo kufanya makampuni ya bima kupeleka gharama hizo kwa wateja wao.

Kwenye elimu nako hakuna uwiano wa pesa zinazotolewa na serikali, kati ya jamii masikini na zile za kati. Hii inasababisha watoto wanaokaa maeneo ya watu wenye vipato vya chini kupata elimu duni wakati serikali inayotoa pesa kwa umma ni moja.

Tukija kwenye huduma za jamii kama maji ni hivyo hivyo, hakuna uwiano wa usafi wa maji baina ya maeneo ya matajiri na masikini. Mfano bomba la mafuta la North Dakota lilibadilishwa njia kutoka kupita kwenye jamii ya watu wenye uwezo na kupelekwa kwa masikini.

Katika chaguzi za Demokrati za kumtafuta mgombea wa chama zinazofanyika mwaka huu, Bernie Sanders ndiye mgombea pekee ambaye sera zake zinawalenga wananchi wa kawaida. Amepanga kongeza wigo wa bima ya wazee ya serikali (Medicare) ili iwe kwa watu wa umri wote. Hii itaondoa ukiritimba wa sasa kwa makampuni binafsi ya bima ya afya kunyanyasa raia wa kipato cha chini.

Pia amepanga kuleta uwiano wa pesa zinazotolewa na serikali katika vitongoji mabalimbali ili watu wote wapate wanachostahili. Pesa hizi ni pamoja zile za shule na maktaba.

Bwana Sanders yeye amekataa kuchukua pesa za matajiri, ambao wanakawaida ya kuhonga wagombea, pesa za kampeni ili waweze kushinda chaguzi zao. Wagombea hao wanaposhinda huenda kuwafanyia kazi makampuni na matajiri badala ya wananchi. Hiki ndicho chanzo cha kuendelea kuwa na pengo la matabaka Marekani ambapo tajiri namba moja duniani, kampuni yake (Amazon) haijalipa kodi (mwaka jana) hata senti moja. Huku mwalimu wa chekechea akilipa kodi 15% ya kipato chake cha mwaka.

Sera hizi za Sanders zimemfanya apendwe sana na wamarekani wengi. Na kuna tetesi kuwa, mwaka 2016 wafuasi wengi wa Sanders walimpigia kura Rais Trump kwa hasira baada ya bwana Sanders kunyang'anywa na chama nafasi ya kuwa mgombea. Mwaka huu watu hao wanategemewa kumpigia mgombea huyo pale atakapo chaguliwa na chama na hatimaye Rais wa nchi.

Wazee wa chama cha demokrati hawamtaki bwana Sanders kuwa mgombea, kwa kuwa wanafaidika na mfumo uliopo sasa. Hivyo, wamekuwa wakitumia njia nyingi ikiwemo vyombo vya habari kumzuia asionekane na wananchi. Hata hivyo kadri siku zinapokwenda mzee wa watu anazidi kuyoyoma na anategemewa kunyakuwa kiti cha mgombea wa chama.

====
Japo siyo kwa umuhimi, niliwahi kutabiri hapa kuwa atachaguliwa mgombea wa chama (December 6th 2019).

Screenshot_2020-02-22 Battle Dar es Salaam vs Nairobi.png
 
Sawa na hapa ambapo kikundi kidogo cha watu ndani ya CCM AU mtu mmoja ndani ya CCM (a) kinahodhi umiliki wa WaTanzania as objects of that kikundi/AU objects zake
Katika mambo ambayo mwalimu aliwalaumu CCM ni kuondoa hoja ya kuwa na mgombea binafsi. Hii huwa inasaidia kuleta haki kama kuna mtu/watu wanaweka kauzibe kwenye kutafuta mgombea ndani ya chama.
 
Maneno laini na ahadi kedekede hazijawahi kuishinda pesa.

Hayo makampuni hayatakuwa tayari kuona mfumo wao unaangushwa kizembe namna hiyo
Ktk dunia ya capitalists hakuna aliyetayari kuona kidudumtu chenye roho ya kimasikini ya kunyanga'anya pesa matajiri na kuzipeleka kwa mama ntilie na machinga kinashika hatam Uchumi wa nchi hauwezi jengwa na watu hao.

Hawana uwezo wa kujenga viwanda n.k. SIONI KAMA UTABIRI WAKO UTATIMIA ngoja tusubiri
 
Maneno laini na ahadi kedekede hazijawahi kuishinda pesa.
Alexandria Ocasio-Cortez (AOC) alimshinda establishment Joe Crowley ambaye alitegemewa aje kuwa spika na alikuwa anamzidi AOC pesa za kampeni mara kumi.

Trump mwenyewe alishinda kwa kujitofautisha na establishment, akijiweka upande wa wananchi masikini (coal miners n.k). Bernie yeye hafanyi siasa, ndivyo alivyo, amekuwa akipigania haki kwa wote toka 1963.

Hawana uwezo wa kujenga viwanda n.k. SIONI KAMA UTABIRI WAKO UTATIMIA ngoja tusubiri
Walishaondoka kwenye uchumi wa viwanda, sasa hivi kiasi kikubwa cha uchumi kinaendeshwa na utoaji huduma. Bw. Sanders ameshinda kura nyingi katika state zote tatu walizopiga kura mpaka sasa, hii haijawahi kutokea katika historia ya uchaguzi Marekani, kwa vyama vyote.
 
Yule mzee ni shida. Kumbe Marekani maisha magumu tu kama bongo ? Bima haighalamii insulin ? Yani mtu anaishi kwenye nchi tajiri zaidi duniani anakufa kwa kukosa pesa ya matibabu?
Aibu sana.

Kashinda Nevada kwa tofauti kubwa sana.

Naona wameanza kumsukumia kashfa kwamba Urusi inamsaidia.

Sema natamani kuona akienda head on na trump. Itakua mshike mshike balaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MjuviKitambo,
Hali haikuwa hivi miaka ya nyuma, umimi uliletwa na kizazi cha baby boomers (kilichozaliwa 1945 - 1968).

Hawa wakati wao wanasoma vyuoni elimu ilikuwa kama bure. Ila wao waliposhika uchumi wakaanza kuweka sera za umimi na ubinafsi, hasa kipindi cha Rais Reagan. Mfano, kwenye mikopo ya chuo (inayotolewa na serikali) waliweka utaratibu wa kuwa na makampuni binafsi kusimamia utoaji mikopo. Hii iliongeza gharama kwa wanafunzi, kiasi kwamba kwa mtu aliyesomea udaktari ni kawaida kuwa na deni la zaidi ya $300,000.

Hata kuanza maisha inakuwa ngumu.

Madaktari wengi wenye madeni hujikuta wakirubuniwa na kuhongwa na makampuni ya kutengeneza madawa. Na hivyo kugeuzwa kuwa wasambazaji wa dawa ghali za kampuni. Utakuta kadawa tuu ka kupaka kwenye ngozi kinagharimu $700 na ndo hiyo hiyo daktari anakuandikia. Halafu unakuta makampuni ya bima yanakataa kulipia baadhi ya dawa au matibabu na hivyo gharama kwenda moja kwa moja kwa raia.

Ukiangalia yote hayo, ndiyo hapo utaelewa kwa nini bw. Sanders anamzidi kura mpinzani anayemfuatia kwa zaidi ya 25%
Trump hatashindwa
Kumbuka pia Trump alisaidiwa na wapiga kura wa Sanders kwa hasira baada ya DNC kumpora uteuzi na kumpa mama Clinton kwa kutumia superdelegates (2016). Sasa hivi hao wote watampigia Sanders, pia vijana wengi wenye madeni ya shule wamehamasika kumpigia kura.
 
@ Chamoto sasa nimeelewa nilikua sijajua maana ya hao boomers halafu nikawa nashangaaa kwa nini ni wazee?

Team Bernie inapiga kazi kuwavuta hawa wazee upande wao wanaanza kufanikiwa.

Nafuatilia kuna mengi ya kujifunza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chamoto,
Mimi sio muumini sana wa historia, Sanders hawezi kushindana na Trump hizo reference huwa naona ni useless kabisa.

Without a shitload of money you can't hope to compete with the trump campaign and it's resources. They will overwhelm and confuse and rip you everywhere but heaven. Good Luck to oldman Sanders hahahaha
 
Mimi sio muumini sana wa historia, Sanders hawezi kushindana na Trump hizo reference huwa naona ni useless kabisa.

Without a shitload of money you can't hope to compete with the trump campaign and it's resources. They will overwhelm and confuse and rip you everywhere but heaven. Good Luck to oldman Sanders hahahaha
AOC was outspent 10 - 1 by Joe (in NYC, out of all places) and won.

Who told you team Bernie doesn't have money? His team, not just has the ability to raise hundreds of small donations but uses guerrilla marketing tactics to reach out to new voters. Trust me, those techniques work.
 
Back
Top Bottom