Trust None
JF-Expert Member
- Feb 12, 2018
- 1,260
- 4,415
Itakuwaje siku siasa zikiruhusiwa na aliyezizuia? Je viongozi wa upinzani watakamatwa kwa uchochezi kwa kuwa watakayoyanena yatakuwa yanakosoa utawala uliopo? Je, wananchi watawaunga mkono kwasababu ya maisha magumu wanayopitia katika awamu hii? Au watawasusa kwa kuwa wanaishi maisha ya raha kuliko awamu zote zilizopita?
Miaka mitano (2015-2020) ikipita tukiendelea kuona na kuishi maisha hayahaya kama tunavyoyaona, je miaka mingine mitano ya mwisho (2020-2025) itakuwaje? Je, atafuata mkondo uleule wa Mseveni, Kagame, Nkurunzinza au Mugabe?
Je, watumishi, wakulima, wafanyabiashara, wanafunzi wa elimu ya juu na wananchi kwa ujumla, kwa maisha mnayoishi sasa hivi, itakuwaje baada ya 2020? Yataendelea kuwa hayahaya? Yatakuwa bora zaidi? Au yatakuwa magumu zaidi?
Tumuombe Mungu ili Wakurugenzi, Polisi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi watende haki mwaka huo maana yajayo YANAFIKIRISHA! yatabadili taswira ya Tanzania kitaifa na kimataifa.
Tunakuomba Mungu Baba muweza wa yote, Mwaka huo utuepushe na mapungufu kama yale ya uchaguzi wa marudio wa Ukonga, Kinondoni, Siha na Kakonko.
Tunakuomba pia utuepushe na yale ya Uchaguzi mkuu wa 2015 wa Raisi, Wabunge na Madiwani. Yasitokee kama yale yaliyotokea Tabora, Nyamagana, Mtama na sehemu nyingine katika uchaguzi mkuu wa 2015, yasijirudie tena 2020.
Tunakuomba utujalie baraka zako kwasababu kuna mgombea hatakubali kirahisi iwapo matokeo halali yatabadilishwa/yatapindishwa. Ataungwa mkono na jumuia za kimataifa hivyo kuiweka nchi ya Tanzania katika historia mpya.
Miaka mitano (2015-2020) ikipita tukiendelea kuona na kuishi maisha hayahaya kama tunavyoyaona, je miaka mingine mitano ya mwisho (2020-2025) itakuwaje? Je, atafuata mkondo uleule wa Mseveni, Kagame, Nkurunzinza au Mugabe?
Je, watumishi, wakulima, wafanyabiashara, wanafunzi wa elimu ya juu na wananchi kwa ujumla, kwa maisha mnayoishi sasa hivi, itakuwaje baada ya 2020? Yataendelea kuwa hayahaya? Yatakuwa bora zaidi? Au yatakuwa magumu zaidi?
Tumuombe Mungu ili Wakurugenzi, Polisi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi watende haki mwaka huo maana yajayo YANAFIKIRISHA! yatabadili taswira ya Tanzania kitaifa na kimataifa.
Tunakuomba Mungu Baba muweza wa yote, Mwaka huo utuepushe na mapungufu kama yale ya uchaguzi wa marudio wa Ukonga, Kinondoni, Siha na Kakonko.
Tunakuomba pia utuepushe na yale ya Uchaguzi mkuu wa 2015 wa Raisi, Wabunge na Madiwani. Yasitokee kama yale yaliyotokea Tabora, Nyamagana, Mtama na sehemu nyingine katika uchaguzi mkuu wa 2015, yasijirudie tena 2020.
Tunakuomba utujalie baraka zako kwasababu kuna mgombea hatakubali kirahisi iwapo matokeo halali yatabadilishwa/yatapindishwa. Ataungwa mkono na jumuia za kimataifa hivyo kuiweka nchi ya Tanzania katika historia mpya.