Lokissa
JF-Expert Member
- Nov 20, 2010
- 7,446
- 2,490
Ustaadhi' amiliki Danguro la watoto Monday, 17 January 2011 10:35 WAKATI asasi mbalimbali za Serikali na zisizo za Serikali zikiwa katika harakati za kutetea haki za watoto ili kuwaepusha na majanga mbalimbali, jitihada hizo zimeonekana kugonga mwamba kwa kuwa asilimia kubwa ya watoto imejiingiza katika biashara ya ukahaba Temeke.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika danguro lenye wanachama zaidi ya 40 katika nyumba moja iliyopo Tandika inayodaiwa kumilikiwa na 'Ustadhi' (jina tunalo) ambaye pia inasemekana ni mjumbe wa shina (namba ya shina tunalo), umebaini katika nyumba hiyo wamo na watu wazima pia wanaojiuza pamoja na watoto hao.
Imedaiwa kuwa watoto hao, ambao wako chini ya umri wa miaka 18, wengi wao ni wanafunzi wa shule za msingi na wengine huwa wanazitoroka familia zao kwa ajili ya kujitafutia maisha.
"Ukimwangalia mtoto mdogo kama huyu, utadhani kuwa hawezi kustahimili vishindo na mikiki tunayokumbana nayo sisi wakubwa, lakini ukimkatalia asifanye kazi hii huwa wanatutukana sana na kudai kuwa sisi siyo wazazi na kwamba wako kikazi kama sisi tulivyo," amesema mama mmoja ambaye hakupenda kutaja jina lake kwa kuhofia kupoteza wateja.
Kahaba mwingine katika eneo hilo amesema licha ya changamoto wanazokumbana nazo kutoka kwa watoto hao, pia wamekuwa wakimlipa mmiliki wa nyumba hiyo kiasi cha sh. 3,000 hadi 5,000 kwa siku kwa kila kizimba ambacho kitanda cha futi tatu kwa sita kinaingia.
"Kitanda cha (futi) tatu kwa sita, ukichoma ndani dakika moja unahudumiwa kwa kiasi cha sh. 2, 000 hadi sh. 3,000 na baada ya kazi kila siku huwa tunalipia sh. 3,000 hadi 5,000 kwa kizimba, hiyo ni sawa na sh. 90,000 hadi sh. 150,000 kwa mwezi na kama unaona tunafanya kazi mbaya unadhani tutaishi vipi hapa!" amehoji kahaba huyo.
Baadhi ya watoto hao walipohojiwa na gazeti hili wamedai kuwa wao siyo watoto kama wanavyofikiriwa.
"Ninaweza kumridhisha mteja wangu kama hawa watu wazima, kama ni shule sisomi na hapa sikuja kufanya biashara, nimekuja kuishi kama wanavyoishi wengine. Hivyo kama na wewe unataka huduma ingia ndani," amesema mtoto huyo ambaye jina lake tunalo.
Hata hivyo, kiongozi wa makahaba hao aliyejitambulisha kwa jina Marieta Ally, maarufu kwa jina la Mchicha Mboga ya Haraka, amekiri kuwapo kwa biashara hiyo na jambo linalowakera ni kuwpao kwa watoto hao wadogo katika eneo hilo na hivyo anaiomba Serikali na mashirika mengine ya kutetea haki za watoto yaingilie kati suala hilo.
"Wanatutukana, na nikijaribu kuwaonya wasiendelee na biashara hii wananiona mimi ni mnafiki sana, matusi mengi yanaporomoshwa kwangu hadi ninaona aibu mwenyewe. Hivyo naiomba Serikali iingilie kati kuwaondoa watoto hawa ili kuwaepusha na majanga mbalimbali na ikiwezekana wapelekwe shule," amesema Marieta.
Hata hivyo, jitihada za kukutana na 'Ustadhi' huyo anayemiliki nyumba hiyo hazikufanikiwa kwa kile kilichodaiwa kuwa yupo safarini na kurudi kwake haijulikani kwani yupo huko kikazi.
"Yupo kikazi hivyo jitihada za kumpata labda arudi kutoka safari na hatujuhi hatarudi lini hivyo basi kama unahitaji ufafanuzi wa nyumba hii pita huko nyuma utapata maelezo zaidi," amesema mama mmoja ambaye alikuwa nje ya nyumba hiyo.
Uchunguzi zaidi umegundua kuwa wakati makahaba hao wanapopata mimba na kujifungua, huwapeleka watoto hao kwa majirani wa eneo hilo kwa ajili ya kuwatunzia kwa gharama ya sh. 1,000 kwa siku.
wanataka tutengane, wanaona maaskofu kama wauaji,wanadai nchi inaongozwa na maaskofu,je matendo yao ?????