Mjadala umeibuka nchini baada ya Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Spika wa Bunge la JMT iliyoachwa wazi baada ya Ndugai kujiuzulu. Hoja bishaniwa imekuwa ni iwapo Dk. Tulia ana sifa au la za kugombea nafasi hiyo.

Kwa mujibu wa Sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge (Na. 3 ya 1988) hususani kifungu cha 41 (1&2), Dk. Tulia kwa sasa ni Kaimu Spika wa Bunge mpaka pale kiti cha Spika kitakapojazwa. Ibara ya 84 (2) ya Katiba ya JMT inaeleza kuwa mtu mwenye madaraka ya aina nyingine yoyote yaliyotajwa na Sheria ya Bunge, hana sifa za kugombea uspika.

Sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge inamtaja Dk. Tulia kwa sasa kuwa ni Kaimu Spika, hii ni ofisi/madaraka na imetajwa na Sheria ya Bunge. Dk. Tulia hana sifa za kugombea uspika, asijidanganye kuwa Ibara ya 84 (2) haijamtaja, asome Sheria namba ya 1988 aone kuwa kwa cheo chake cha Kaimu Spika amezuiwa kugombea uSpika. HANA SIFA

View attachment 2079266
Aah,, sasa unaharibu, unaharibu bana...

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Napata shida na hiki watu walichokikomalia kwa Tulia,

Huu mchakato unaoendelea ni wa kichama (Maccm) yanapambana kupata mgombea watakaye mdhamini. Kwa vyovyote mpaka muda huu Tulia anazo sifa kama mwanachama yeyote lakini ikitokea ccm wameteua jina la Tulia awe mgombea wao wa kiti Cha Uspika ni lazima Tulia ajiuzulu unaibu Spika ndipo apate sifa ya kuchukua fomu ya kuwa mgombea rasmi.

Sijui kinachowaumiza watu kuhusu Tulia mpaka hapo.
Ok, uko sahihi

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Tanzania hatuna astute lawyers bali tuna watu wenye kujaza makaratasi ya uanasheria tupu bila kujua kutafsiri katiba na sheria na wenye kuona na kukbali kuona katiba inachezewa na sheria zikifanyiwa asusa. RIP Mchungali Christopher Mkitila najua angeshalisongesha front kuanzia kwa Ndungai hadi na hii ya Tulia
 
Baada tuu ya Spika kujiuzulu, automaticaly Naibu Spika anakuwa kaimu Spika, hivyo kifungu hicho kina mhusu
p

Pasi ngoja nitulie kuna kitu nitaongezea katika ule mjadala wako wa Job kujihudhuru na mambo ya kukiuka utaratibu na sheria ila pia naona Mzee Pius Msekwa keshalitolea ufafanuzi katika maandiko yake huko Daily news, wewe ni msomaji mzuri na habari ni tasnia yako nina imani utaisapua uongeze maarifa
 
Napata shida na hiki watu walichokikomalia kwa Tulia,

Huu mchakato unaoendelea ni wa kichama (Maccm) yanapambana kupata mgombea watakaye mdhamini. Kwa vyovyote mpaka muda huu Tulia anazo sifa kama mwanachama yeyote lakini ikitokea ccm wameteua jina la Tulia awe mgombea wao wa kiti Cha Uspika ni lazima Tulia ajiuzulu unaibu Spika ndipo apate sifa ya kuchukua fomu ya kuwa mgombea rasmi.

Sijui kinachowaumiza watu kuhusu Tulia mpaka hapo.
Kinachowafanya watu wamshangae Tulia anavyoleta ukanyagaji wa Katiba ni kwa kuwa jina lake litakapopita kwenye Chama ndio anakuwa mgombea uSpika. Hakunaga muda tena wa kuchukua fomu kwa kuwa uspika unagombewa kwa chama cha siasa kuwasilisha bungeni jina la mgombea wao - kama mgombea ni mbunge (kwa njia ya barua tu) na kama mgombea sio mbunge basi chama kinawasilisha jina hilo katika Tume ya uchaguzi na Tume ya Uchaguzi ndio inawasilisha bungeni jina la mgombea, hakuna fomu za kujaza . Sasa huyo Tulia anatakiwa kujiuzulu sasa ili apate sifa za kugombea na pia anapewa elimu hii mapema ili ajifunze, maana kwa uelewa wake anaona kuwa hajakosa sifa. Kuna video yake hapo anasema Naibu Spika hajazuiliwa kugombea, yeye hawazi hizo habari za mchakato wa Chama, anaona kuwa ana sifa kwa kuwa cheo cha Naibu spika hakijatajwa kwenye ibara ya 84(2) ya Katiba ya JMT. Mfundisheni
 
Tanzania hatuna astute lawyers bali tuna watu wenye kujaza makaratasi ya uanasheria tupu bila kujua kutafsiri katiba na sheria na wenye kuona na kukbali kuona katiba inachezewa na sheria zikifanyiwa asusa. RIP Mchungali Christopher Mkitila najua angeshalisongesha front kuanzia kwa Ndungai hadi na hii ya Tulia
Kulinda katiba ni jukumu la kila mwananchi bila ya kujali elimu au cheo chake. Ni wajibu wako kuzuia uvunjwaji wa Katiba
 
Afadhali kuna kitu kama hiki..japo hakupenda kabisa kijulikane kwa wengine
Amekomaa na ibara ya Katiba tu wakati Katiba imeelekeza kusoma sheria nyingine. Aseme anagombea kibabe lakini asitudanganye kuwa ana sifa za kugombea kisheria.
 
Tulia anagombea ndani ya Chama, ambao watapeleka jina moja bungeni. Tulia hajagombea akiwa bungeni, ila akiwa ndani ya Chama.
 
Mimi naona hili suala limeangaliwa upande mmoja..Mimi naona tulia Yuko sahihi coz amegombea ndani ya chama na si bungeni..jina lake likipitishwa na kumpelekea bungeni kule atakutana na wagombea wengine hapo ndio katiba itafanya kazi..na ndio hapo ataresign...yeye kaonyesha kutaka kugombea nje ya bunge..sio ndani

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Nakubaliana na hoja Yako. Bado hajagombea bungeni.
 
Watu wanataka mtu mpya. Sio damu ya zamani ya kunguni.

Tulia alikuwa creation ya Jiwe ili amtumie kumuongezea muda wa kutawala baada ya huhula wake hapo ungemallizika ; na pia alishiriki kuvunja katiba kuwaruhusu wale covi19 kuingia bungeni!! Hafai, anahitajika Spika anaejiamini na hawezi kuyumbishwa!
 
Bunge bado halijatoa fomu za kugombea uspika..Dk Tulia anagombea ndani ya chama chake,itakapofika CCM wamempitisha na Bunge kuanza kutoa fomu hiyo sheria itamhusu.
 
Mimi naona hili suala limeangaliwa upande mmoja..Mimi naona tulia Yuko sahihi coz amegombea ndani ya chama na si bungeni..jina lake likipitishwa na kumpelekea bungeni kule atakutana na wagombea wengine hapo ndio katiba itafanya kazi..na ndio hapo ataresign...yeye kaonyesha kutaka kugombea nje ya bunge..sio ndani

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Huko bungeni huwa wanapeleka majina mangapi
 
Bunge bado halijatoa fomu za kugombea uspika..Dk Tulia anagombea ndani ya chama chake,itakapofika CCM wamempitisha na Bunge kuanza kutoa fomu hiyo sheria itamhusu.
Ndugu, Bunge hawatoi fomu za mtu kugombea uspika. Bunge linasubiri tu kupokea jina kutoka vyama vya Siasa (ikiwa wagombea ni wabunge) au kutoka Tume ya uchaguzi ikiwa wagombea watakuwa sio wabunge. Ukipata nomination ya chama imetoka, chama ndio kinapeleka jina lako bungeni
 
Mimi naona hili suala limeangaliwa upande mmoja..Mimi naona tulia Yuko sahihi coz amegombea ndani ya chama na si bungeni..jina lake likipitishwa na kumpelekea bungeni kule atakutana na wagombea wengine hapo ndio katiba itafanya kazi..na ndio hapo ataresign...yeye kaonyesha kutaka kugombea nje ya bunge..sio ndani

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Kwa hiyo CCM itakaa na kujadili ili kumpitisha mtu asiyekuwa na sifa za msingi za kugombea kuwa Spika ili akishapitishwa ndio aende kuwa na sifa?

Kwa hiyo Tulia ameingi mkataba binafsi na CCM kuwa akipitishwa kugombea uspika ndio ataachia kiti cha unaibu spika?

Kwa hiyo CCM inafanya shughuli zake kama bahati nasibu au betting?

Kama CCM watafanya hivyo hicho kitakuwa ni chama cha ajabu ajabu sana.
 
Back
Top Bottom