Uspika na Nguvu ya Mafisadi!

KakaKiiza

JF-Expert Member
Feb 16, 2010
11,555
8,552
Nasema nimwaka mbaya kwa kambi ya upinzani katika bunge kwani kitendo cha ccm kuwasimamisha wabunge wanawake kuwania Uspika ni ishara ya kudhoofisha upinzani Bungeni!kwa kulinda maslahi ya wakubwa bungeni kwakutambua kuwa nirahisi kumuingia mwanamke kuliko kumuingia mwanamume kwa matakwa yako ndiyo maana mafisadi wamefanya kila njia kuhakikisha Samweli sita anaanguka kwakujua hilo ndiyo maana Chenge alisimamishwa!!kwakuwa wote wana influence kwenye chama wakatumia hoja wote tuwapige chini Sitta na Chenge!!lakini huku wakijua lengo lao limetimia lakumuangusha Samweli Sitta kwani walitambua angerudi bungeni angekuwa mwiba kwao!Chakuomba wapinzani wachukue kiti hicho cha uspika!!Na team inayomuunga mkono Sitta watachagua upinzani hilo halina kificho hapa! Mafisadi ni wabaya kokote ulimwenguni kwani wana nguvu ana kwenye serikali husika!
 
Kwanza sitegemei kama wabunge wa CCM watakaokuwa na uzalendo wa kumpigia spika wa kutoka upinzani kura wapo. Pili, kwa CCM, kuchagua spika asiyejua sheria na kanuni za bunge (hawa wamama ahkuna anayezimanya), WAMEJIFUNGA GOLI LA NNE...
 
Vyovyote itakavyokuwa spika hana uwezo wa kuzuia hoja bungeni zisisikike kwa wananchi, labda kinachotakiwa kufanyika ni kupiga marufuku matangazo ya moja kwa moja toka bungeni kama hawataki wananchi wakisikia serikali yao inavyokosolewa. Tofauti na hivyo spika akikataa hoja binasfi, bado mbunge mwenye kujua kujenga hoja ataichapia kwenye mijadala mingine mfano wakati wa kuchangia bajeti
 
Tanzania is wrotten, and manners dont stand anymore!
PCCB is a white elephant, and the same dance goes now to the Parliament!...U will be surprised to find ccm mp's voting for Anna Makinda , while they clearly know through experience that she has been a hindrance to most of agendas risen for discussion in the session. Voting for this old granny is accepting or consenting for the corruption squad to stand with all its ugliness!...
Wabunges, u have been sent by your people to make sure that the resources of the country are equally distributed for the betterment of all citizens, so execute your responsibility, and not just favoring your families and the so called 'chama' interests!
 
Nasema nimwaka mbaya kwa kambi ya upinzani katika bunge kwani kitendo cha ccm kuwasimamisha wabunge wanawake kuwania Uspika ni ishara ya kudhoofisha upinzani Bungeni!kwa kulinda maslahi ya wakubwa bungeni kwakutambua kuwa nirahisi kumuingia mwanamke kuliko kumuingia mwanamume kwa matakwa yako ndiyo maana mafisadi wamefanya kila njia kuhakikisha Samweli sita anaanguka kwakujua hilo ndiyo maana Chenge alisimamishwa!!kwakuwa wote wana influence kwenye chama wakatumia hoja wote tuwapige chini Sitta na Chenge!!lakini huku wakijua lengo lao limetimia lakumuangusha Samweli Sitta kwani walitambua angerudi bungeni angekuwa mwiba kwao!Chakuomba wapinzani wachukue kiti hicho cha uspika!!Na team inayomuunga mkono Sitta watachagua upinzani hilo halina kificho hapa! Mafisadi ni wabaya kokote ulimwenguni kwani wana nguvu ana kwenye serikali husika!

Kama unadhani ni mwaka mbaya kwa wapinzani!!! umekosea saana. binafsi nadhani ni mwaka mzuri kupita kiasi kwani CCM imejipiga GOLI LA KISIGINO. Amini nakwambia, CCM haijatosheka na bakora ilizochapwa hivi punde kwenye uchaguzi uliopita. nilidhani zilikuwa ni bakora za kutosha kabisa kumnyoosha mtoto yeyote mtukutu kama CCM. Nilidhani kuanzia baada ya uchaguzi, CCM itakuwa inafanya kila kitu kwa kutazama matakwa ya wananchi na sio matakwa ya WACHUMIA TUMBO.. lakini nimepigwa sana na mshangao wa hiki walichokifanya na inadhihirisha jinsi ambavyo wezi watabaki kuwa wezi hata kama watakabidhiwa dunia iwe mali yao.
Kwa waliolifanya,,,, ni advantage kwa upinzani kwani watanzania wanajua nini kinaendelea na nini dhamira yao katika kumng,oa SITTA

 
Wabunge wote wa CCM wenye mapenzi mema na hii nchi msimchague spika aliyepitishwa na mafisadi......huyo ataendeshwa kwa remote ya mafisadi...........hii nchi imefika mahali pabaya sana kwani Rais amewakabithi mafisadi nchi, Eti wanasema wameona ni muda muafaka wa kumpa mwanamke madaraka makubwa......aibu kwao!! Hii ni danganya toto!! msifikiri watanzania ni wajinga kama manavyofikiria, Kumtoa Sita Itawagarimu CCM (chama cha mafisadi) na aliyewashauri mkaingia kingi amewapoteza! Wabunge wa CCM wapinga mafisadi mpigieni Marando Kura zenu Kwa Manufaa ya Taifa.....msiangalie Chama angalia mstakabali wa taifa kwani hata mafisaid hawaangalii chama wanaangalia maslahi na ulinzi wa mali walizoiba ndo maana wamemngoa Sita. Mafisaidi wakiwapa rushwa pokeeni lakini kura ni siri yako.......Mungu atakubariki, tunawaombea wapambanaji wote...........Mungu wetu ni mwaminifu, atasimama, Mungu awalinde. AMEN.
 
Wabunge muwe wazalendo kwa maslai ya watanzania kama walivyo wamarekani linapokuja swala lakutanguliza maslai ya nchi yao mafisadi wasime ndiyo washika usukani wanchii!!!
 
Kwasababu mafisadi wanatumia mbinu chafu kutaka kukandamiza nguvu ya umma nivyema wapinzani nao wakatafuta mbinu mbadala ya kuhakikisha sauti ya umma haimezwi...

Wazo
tumuombe Slaa amuoe Anna Makinda kama A M atapitishwa kuwa spika wa bunge. Hii itasaidia slaa kuwa spika kwa mlango wa nyuma
 
Vyovyote vile iweje, vita ya ufisadi isipoanzia bungeni itaanzia kwa wananchi na itawaondoa wabunge wote wa ccm mwaka 2015. Msiwe na wasi wasi ngoja tuone Makinda atafanya nini!

Kufikiri kwamba wabunge wa ccm watampa Marando ni uongo. Najua huwa wamelishwa dawa chungu hawa. Huwa akili zao hazifiri nje ya upeo wa macho yao hadi waenguliwe kwenye uongozi.

Ila sina shaka sisi huku tutaendelea kuwahukumu.
 
Wametimiza walichotaka kumtoa six kwenye hicho kiti ni kosa ambalo watakuja kushtuka baadae kwa sasa wanawafurahisha wafazili wa chama
 
Katika hotuba yake baada ya kuapishwa Rais wa JMT na Mwenyekiti wa CCM alisema kwamba kutokana na kipigo walichokipata katika uchaguzi mkuu kwa kupoteza majimbo mengi (Nyamagana, Ilemela na Iringa kutaja machache). kama chama wangekaa na kuangalia wapi walijikwaa na kuangukia pua. Maskini ccm kabla hawajafanya tathmini ya uchaguzi wamejikwaa tena. Kwa kumtoa Sitta katika kinyang'anyilo cha Uspika, ccm imejikwaa tena. Tusubiri kuona itaangukia wapi.
 
Mimi nachoona kwaharaka nikwamba wameongeza mpasuko ndani ya ccm kwani sitta watu wanaomuunga mkono lazima hawatamsapoti yule atakaeingia japo cc imetimiza ilichokitaka!!kwakudhani kwamba wamemaliza mpasuko kazi nikubwa iliyopo mbele zao wametengeneza makundi kwakutojua.
 
Watanzania bwana, tunapenda witch hunting. Primary responsibility ni ya kwetu, nayo ni kuwaingiza wabunge wengi wa UPINZANI bungeni na kuinyima out right majority CCM. Tutakuwa tume solve mizengwe ya CCM ya kutumikia mafisadi.

Lakini kuingiza wabunge wengi wa CCM bungeni na kuwaomba wabunge wa CCM wampigie SPIKA wa upinzani It is a wshiful thinking.

Jiulize wewe umefanya nini kuhakikisha CCM hatupatia SPIKA wa mafisadi? Jibu ni rahisi kumpigia kura mgombea wa ubunge wa UPINZANI.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom