Zitto
Former MP Kigoma Urban
- Mar 2, 2007
- 1,562
- 10,880
Maswali muhimu kutoka Ripoti ya CAG 2016/17 SERIKALI KUU( rejea kurasa za Ripoti Kuu ya CAG ) Ripoti ya CAG kwa mwaka ulioishia 30 Juni, 2017 imejaa madudu
- Zipo wapi Shilingi Trilioni 1.5 zilizokusanywa na Serikali Lakini hazikutolewa kwa matumizi wala kukaguliwa? Ukurasa 34
- Kwanini Serikali imekopa TZS 500 bilioni zaidi ya kiwango kilichoidhinishwa na Bunge. Uk 30
- Kwanini Serikali imetekeleza 68% tu ya Bajeti ya Maendeleo kwa Serikali Kuu na 51% tu kwa Serikali za Mitaa? uk 38
- Kwanini Serikali ilitumia zaidi ya shilingi 219 bilioni, kulipa madeni ya nyuma ambayo hayakuwa kwenye Bajeti? uk 40
- Kwanini Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Wametoa Takwimu za Uongo za Mapato ya Kodi ya zaidi ya shilingi 2.2 trilioni? uk 109
- Serikali ya Jamhuri ya Muungano imepata Hati Chafu ( Hesabu Jumuifu za Taifa ). Kwanini Katibu Mkuu Hazina hajachukuliwa hatua kama ilivyokuwa kwa Wakurugenzi wa Serikali za Mitaa? uk 296-298