kudamademede
Member
- Jan 1, 2020
- 62
- 241
Kiza kimetanda, wananchi wanahaha mitaani, hawajui watakula nini kesho.
Mama anaamka, huku amelala na njaa ya siku mbili. Maziwa ya mtoto yamekata. Anajikokota kutafuta unga apike uji wa mwanae wa miezi 7.
Ikiwa takribani wiki mbili tangu rais Mseveni atangaze lockdown tena kwa siku 42 hapa nchini Uganda, maisha yamekuwa magumu sana.
Kila mmoja analia, si mama ntilie, sio wamachinga na hata wafanyabiashara wakubwa, wote wanalia... Wanyonge wanalia.
Zamani tulishuhudia baa la njaa likiua watu huko Sudani kwa sababu ya ukame, Sasa huu umekuwa ukame wa kujitakia.
Nikiwa nimetoka Masaka kuelekea Entebbe, njiani kweupe, Giza limetanda. Jana yake tukiwa tumetoka Mbalala, tulikutana na mmachinga mmoja aliyetupa stori ya shangazi yake alizika watoto wawili kwa sababu ya chanjo ya Corona. Huku njaa kwa sababu ya lockdown, huku chanjo ya Corona ikiua. Ukikosa kufa kwa sababu ya kutochanjwa, basi huenda ukadhoofika hata kufa kwa sababu ya baa la njaa.
Na huko Tanzania ambako tulikuwa tunajivunia ushujaa wa mwamba mmoja Afrika, mzee Magufuli, nasikia nako chanjo inaingia...
Ukiongea na Waganda wanakwambia Afrika ilikuwa imebaki nchi moja nayo ni Tanzania ambayo haijapiga goti kwa mbepari. Waganda walikuwa wanaenda kifua mbele kuona Tanzania watu hawavai barakao.
Rafiki yangu mmoja aliyeko Tanzania aliniambia kuwa mtaa wa Kongo-Kariakoo ulikuwa unafurika utadhani Corona haipo duniani. Sasa nayo Tanzania imesalimu amri kwa mbepari.
Sisi hapa Uganda tumeona madhara ya lockdown. Haifai kabisa. Tumeshindwa kuipinga kwa sababu rais wetu amekubali kutuuza kwa mabeberu. Ametuuza mpaka sasa yanazikwa majeneza feki, yasiyo na watu ilimradi ionekane watu wanakufa...Ili chanjo ihalalishwe kwa Waganda wote hapa ndo Afrika tulipofikia. Tunauzana sisi kwa sisi kwa mbepari. Je, hii sio vita ya wenyewe kwa wenyewe?
Tulisikia mbunge mmoja wa Tanzania, kama sikosei alikuwa Humphrey Polepole akisema kwa ujasiri kwamba Tanzania isiache njia zilizoivusha mwaka uliopita mpaka ikaingia uchumi wa kati.
Siku nyingine tukasikia askofu Gwajima akisema Tanzania isikubali chanjo, maana kila chanjo ina madhara. Na mojawapo ya madhara ni vifo. Walau tunafarijika kwa hawa Wabunge shupavu walioko Tanzania.
Ikiwa Tanzania imekubali kuanza kuvaa barakoa tena; na nasikia kwamba imeagiza chanjo pia, je ni kweli kwamba Mama Samia naye amekubali kuwauza Watanzania kama walivyofanya Mseveni, Kenyata na Kagame?
Amekubali kuwa mshirika wa hawa waliowauza watu wao kwa dola za magharibi?
Nani amesalia Afrika? Watanzania endelea kumuomba Mungu wenu. Mungu yule aliyewasaidia mwaka jana labda atawasaidia tena kipindi hiki.
Ernest Busingye
Masaka - Uganda
Email: ebusingye@gmail.com
Mama anaamka, huku amelala na njaa ya siku mbili. Maziwa ya mtoto yamekata. Anajikokota kutafuta unga apike uji wa mwanae wa miezi 7.
Ikiwa takribani wiki mbili tangu rais Mseveni atangaze lockdown tena kwa siku 42 hapa nchini Uganda, maisha yamekuwa magumu sana.
Kila mmoja analia, si mama ntilie, sio wamachinga na hata wafanyabiashara wakubwa, wote wanalia... Wanyonge wanalia.
Zamani tulishuhudia baa la njaa likiua watu huko Sudani kwa sababu ya ukame, Sasa huu umekuwa ukame wa kujitakia.
Nikiwa nimetoka Masaka kuelekea Entebbe, njiani kweupe, Giza limetanda. Jana yake tukiwa tumetoka Mbalala, tulikutana na mmachinga mmoja aliyetupa stori ya shangazi yake alizika watoto wawili kwa sababu ya chanjo ya Corona. Huku njaa kwa sababu ya lockdown, huku chanjo ya Corona ikiua. Ukikosa kufa kwa sababu ya kutochanjwa, basi huenda ukadhoofika hata kufa kwa sababu ya baa la njaa.
Na huko Tanzania ambako tulikuwa tunajivunia ushujaa wa mwamba mmoja Afrika, mzee Magufuli, nasikia nako chanjo inaingia...
Ukiongea na Waganda wanakwambia Afrika ilikuwa imebaki nchi moja nayo ni Tanzania ambayo haijapiga goti kwa mbepari. Waganda walikuwa wanaenda kifua mbele kuona Tanzania watu hawavai barakao.
Rafiki yangu mmoja aliyeko Tanzania aliniambia kuwa mtaa wa Kongo-Kariakoo ulikuwa unafurika utadhani Corona haipo duniani. Sasa nayo Tanzania imesalimu amri kwa mbepari.
Sisi hapa Uganda tumeona madhara ya lockdown. Haifai kabisa. Tumeshindwa kuipinga kwa sababu rais wetu amekubali kutuuza kwa mabeberu. Ametuuza mpaka sasa yanazikwa majeneza feki, yasiyo na watu ilimradi ionekane watu wanakufa...Ili chanjo ihalalishwe kwa Waganda wote hapa ndo Afrika tulipofikia. Tunauzana sisi kwa sisi kwa mbepari. Je, hii sio vita ya wenyewe kwa wenyewe?
Tulisikia mbunge mmoja wa Tanzania, kama sikosei alikuwa Humphrey Polepole akisema kwa ujasiri kwamba Tanzania isiache njia zilizoivusha mwaka uliopita mpaka ikaingia uchumi wa kati.
Siku nyingine tukasikia askofu Gwajima akisema Tanzania isikubali chanjo, maana kila chanjo ina madhara. Na mojawapo ya madhara ni vifo. Walau tunafarijika kwa hawa Wabunge shupavu walioko Tanzania.
Ikiwa Tanzania imekubali kuanza kuvaa barakoa tena; na nasikia kwamba imeagiza chanjo pia, je ni kweli kwamba Mama Samia naye amekubali kuwauza Watanzania kama walivyofanya Mseveni, Kenyata na Kagame?
Amekubali kuwa mshirika wa hawa waliowauza watu wao kwa dola za magharibi?
Nani amesalia Afrika? Watanzania endelea kumuomba Mungu wenu. Mungu yule aliyewasaidia mwaka jana labda atawasaidia tena kipindi hiki.
Ernest Busingye
Masaka - Uganda
Email: ebusingye@gmail.com