JOHNGERVAS
JF-Expert Member
- Mar 22, 2016
- 470
- 597
Nimesoma Kupitia Instagram ya Mtangazaji wa Star TV Alloyce Nyanda, nimeona pia niwashirikishe
Je ni nani anayezungumziwa kwenye hiyo story?
Je Nyanda alikuwa nabariki Jambazi Sabaya asifungwe na anataka kutuaminisha alimpigania kabisa, Ama je inaweza kuwa na yeye ni sehemu ya waliofaidi matunda ya akzi chafu za sabaya?
haya sasa soma alichopost
***************************************
Hadithi hii nisingeweza kuisema lakini naisimulia kwa sababu moja tu! Nitaisema Mwishoni
Mtu mmoja ni rafiki yangu na ni kiongozi! Nimefahamiana nae kwa Muda mrefu sana Na sijafahamiana nae mitaani tu ipo historia,
Alivyokuwa kiongozi wa kitaifa niliona mabadiliko flani kwake mie nikamwambia kaka umeanza kubadilika acha kuanza kutoa kauli za namna hii kwa watu. Usimuheshimu aliekuteua tu.
Akanijibu sawa kaka tena kwa uungwana, Huyu jamaa alikuwa rafiki yake sana na Lengai ole Sabaya na hata huyu Makonda ni marafiki sana.
Walikuwa marafiki sana na Lengai Hata ile operation ondoa Mbowe Hai alikwenda katika Mikutano kutia nguvu, tulimuona katika Ma Tv
Alikuwa nikikutana nae huyo Kiongozi ananionyesha uswahiba wake ulivyokolea na lengai nami nikasema huu ndio Utu na urafiki wa kweli.
Gafla Mambo yakabadilika Magufuli akafariki . Rais Samia akapanga Safu Lengai akatemwa na bwana yule akahakishwa pale pa awali akapelekwa pengine yupo hadi sasa.
Wakati kesi ya Sabaya inaendelea nikamwambia kaka Lengai amepata hayo nenda kamuone tafadhali jamaa akasema haaa kaka siwezi mambo mengi kidogo
Nikamwambia mie naenda kumsalimia kesho kutwa hakunijibu
Nilivyoenda kwa Sabaya gerezani Lengai akaniuliza Flani yupo? Mwambie aje kunisalimia? Nikamwambia jamaa mzima na nitamwambia swahiba wako
Nilipotoka kule nikamwambia kaka Lengai anakusalimu kamuone kaka, jamaa akasoma sms whats app hakujibu!
Muda ukapita Mwanahabari @korumba_lebabazi siku moja alienda Kisongo kumsalia Lengai kisha akaambiwa msalimia Mtozi akampatia ka ujumbe flani.
Mie nikapokea ila nikamwambia Pia Swaiba wa Lengai kuwa bwana kuna hili ebu tumzame kama binadamu na sio kama swahiba au mhalifu, bwana yule hakujibu na nilikuwa naona status zake nadhani akafuta na namba kabisa
Korumba nikwambia kaka tutafanya wenyewe acha tujaribu na tulifanya
Ila mie niliufahamu uswahiba wa dhati wa bwana yule na Lengai! walipendana sana na kuheshimiana sana ,aliepo jela alimsaidia sana bwana huyu.
Niliskia mawakili wa Lengai wana chagamoto mie nikwambia tena aisee tufanye hiki
.. Nilipomwambia kuwa kaka kuna changamoto ya mawakili wa Lengai yule ni jamaa yako tafadhali tufanye moja mbili , jamaa hakujibu nikasema unajua unaweza kumlaumu mtu kumbe hata simu hana ngoja nimpigie
Nikampigia wiki ya Kwanza hakupokea, nikapiga wiki ya pili hakupokea na hapo kuna siku nampigia hata mara 5 hakupokea akavunja mwezi nikajua mmmh imeisha!
Nikiwa nimekaa ofisin siku moja pale kantini nakula chakula pembeni yangu alikuwepo dada yangu @fashywhite nikamwambia hivi dada Fatma haya maisha huwa yako vipi? Nikamwambia wiki ijayo hukumu ya Lengai huenda akafungwa au akawa huru kama atakuwa huru huyu flani atakuja kusema pole swahiba! Fatma akaniambia hapa Duniani ishi kwa kiasi na watu mkumbatie zaidi Mungu! (Nilimsimulia )
Tarehe ya Hukumu ya Lengai ikafika na akahukumiwa kwenda Jela miaka 30
Muda ule ule taarifa za hukumu ya Lengai zimetoka nilikuta yule bwana amenipigia kama mara 4 sikuwa karibu na simu lakini bwana yule nilikuta amenitumia sms pia ikisema “KAKA NDUGU YETU AMEHUKUMIWA TUSIACHE KUMUOMBEA” Nikasoma ile sms wala siku mjibu
Akawa akinipigia sikuwahi hata kupokea kwa ziadi ya miezi 2 , siku moia nikajiuliza mbona biblia inasema hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu? Sasa mie sio mpumbavu
Nikampigia nikamsema sana na kumuonyesha mambo haya ni dhamana ni mambo ya nyakati, nikamkumbusha Mambo kadhaa nikamsisitiza mambo kadhaa kuwa Dunia hii haina Bingwa
Tuwapende wenzetu wanapokuwa katika nyakati nzito hata kama walifanya makosa wameshapata adhabu sasa sie pia tunaweza kuwa faraja sio dhambi!
Sasa kwa nini nimeandika haya! Sababu kuu ni moja! Usiogope wakiondoka na hata kama watakuachia maumivu, ipo siku watakuja tena wakidai wametoka mbali na wewe.
Na mara zote ukiwa umetingwa na umeanza kupoteza matumaini watasema TUPO PAMOJA hapo ujue wamekaribia kuondoka, Tumaini lako liwe kwa Mungu wako tu si kwa Mwanadamu.
Je ni nani anayezungumziwa kwenye hiyo story?
Je Nyanda alikuwa nabariki Jambazi Sabaya asifungwe na anataka kutuaminisha alimpigania kabisa, Ama je inaweza kuwa na yeye ni sehemu ya waliofaidi matunda ya akzi chafu za sabaya?
haya sasa soma alichopost
***************************************
Hadithi hii nisingeweza kuisema lakini naisimulia kwa sababu moja tu! Nitaisema Mwishoni
Mtu mmoja ni rafiki yangu na ni kiongozi! Nimefahamiana nae kwa Muda mrefu sana Na sijafahamiana nae mitaani tu ipo historia,
Alivyokuwa kiongozi wa kitaifa niliona mabadiliko flani kwake mie nikamwambia kaka umeanza kubadilika acha kuanza kutoa kauli za namna hii kwa watu. Usimuheshimu aliekuteua tu.
Akanijibu sawa kaka tena kwa uungwana, Huyu jamaa alikuwa rafiki yake sana na Lengai ole Sabaya na hata huyu Makonda ni marafiki sana.
Walikuwa marafiki sana na Lengai Hata ile operation ondoa Mbowe Hai alikwenda katika Mikutano kutia nguvu, tulimuona katika Ma Tv
Alikuwa nikikutana nae huyo Kiongozi ananionyesha uswahiba wake ulivyokolea na lengai nami nikasema huu ndio Utu na urafiki wa kweli.
Gafla Mambo yakabadilika Magufuli akafariki . Rais Samia akapanga Safu Lengai akatemwa na bwana yule akahakishwa pale pa awali akapelekwa pengine yupo hadi sasa.
Wakati kesi ya Sabaya inaendelea nikamwambia kaka Lengai amepata hayo nenda kamuone tafadhali jamaa akasema haaa kaka siwezi mambo mengi kidogo
Nikamwambia mie naenda kumsalimia kesho kutwa hakunijibu
Nilivyoenda kwa Sabaya gerezani Lengai akaniuliza Flani yupo? Mwambie aje kunisalimia? Nikamwambia jamaa mzima na nitamwambia swahiba wako
Nilipotoka kule nikamwambia kaka Lengai anakusalimu kamuone kaka, jamaa akasoma sms whats app hakujibu!
Muda ukapita Mwanahabari @korumba_lebabazi siku moja alienda Kisongo kumsalia Lengai kisha akaambiwa msalimia Mtozi akampatia ka ujumbe flani.
Mie nikapokea ila nikamwambia Pia Swaiba wa Lengai kuwa bwana kuna hili ebu tumzame kama binadamu na sio kama swahiba au mhalifu, bwana yule hakujibu na nilikuwa naona status zake nadhani akafuta na namba kabisa
Korumba nikwambia kaka tutafanya wenyewe acha tujaribu na tulifanya
Ila mie niliufahamu uswahiba wa dhati wa bwana yule na Lengai! walipendana sana na kuheshimiana sana ,aliepo jela alimsaidia sana bwana huyu.
Niliskia mawakili wa Lengai wana chagamoto mie nikwambia tena aisee tufanye hiki
.. Nilipomwambia kuwa kaka kuna changamoto ya mawakili wa Lengai yule ni jamaa yako tafadhali tufanye moja mbili , jamaa hakujibu nikasema unajua unaweza kumlaumu mtu kumbe hata simu hana ngoja nimpigie
Nikampigia wiki ya Kwanza hakupokea, nikapiga wiki ya pili hakupokea na hapo kuna siku nampigia hata mara 5 hakupokea akavunja mwezi nikajua mmmh imeisha!
Nikiwa nimekaa ofisin siku moja pale kantini nakula chakula pembeni yangu alikuwepo dada yangu @fashywhite nikamwambia hivi dada Fatma haya maisha huwa yako vipi? Nikamwambia wiki ijayo hukumu ya Lengai huenda akafungwa au akawa huru kama atakuwa huru huyu flani atakuja kusema pole swahiba! Fatma akaniambia hapa Duniani ishi kwa kiasi na watu mkumbatie zaidi Mungu! (Nilimsimulia )
Tarehe ya Hukumu ya Lengai ikafika na akahukumiwa kwenda Jela miaka 30
Muda ule ule taarifa za hukumu ya Lengai zimetoka nilikuta yule bwana amenipigia kama mara 4 sikuwa karibu na simu lakini bwana yule nilikuta amenitumia sms pia ikisema “KAKA NDUGU YETU AMEHUKUMIWA TUSIACHE KUMUOMBEA” Nikasoma ile sms wala siku mjibu
Akawa akinipigia sikuwahi hata kupokea kwa ziadi ya miezi 2 , siku moia nikajiuliza mbona biblia inasema hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu? Sasa mie sio mpumbavu
Nikampigia nikamsema sana na kumuonyesha mambo haya ni dhamana ni mambo ya nyakati, nikamkumbusha Mambo kadhaa nikamsisitiza mambo kadhaa kuwa Dunia hii haina Bingwa
Tuwapende wenzetu wanapokuwa katika nyakati nzito hata kama walifanya makosa wameshapata adhabu sasa sie pia tunaweza kuwa faraja sio dhambi!
Sasa kwa nini nimeandika haya! Sababu kuu ni moja! Usiogope wakiondoka na hata kama watakuachia maumivu, ipo siku watakuja tena wakidai wametoka mbali na wewe.
Na mara zote ukiwa umetingwa na umeanza kupoteza matumaini watasema TUPO PAMOJA hapo ujue wamekaribia kuondoka, Tumaini lako liwe kwa Mungu wako tu si kwa Mwanadamu.