Albinoomweusi
JF-Expert Member
- Oct 28, 2016
- 3,175
- 8,187
WANAUME KUNA VITU LAZIMA TUVIELEWE KWA WANAWAKE.
Biblia inasema:
MWANAMKE NI KIUMBE DHAIFU
Hapo hapo inasema;
TUKAE NAO KWA AKILI.
Na bado inasema;
MWANAMKE NI JESHI KUBWA
Swali?
Walijifunza saa ngapi uwanajeshi na ili kudhibitisha kwamba ni Mwanajeshi Mungu anamtuma kwa Mwanamme akamlinde.
Yeremia 31:22 ....
Kwa maana Bwana ameumba jambo jipya Duniani; Mwanamke atamlinda Mwanamume.
KUMBUKA HILI MWANAUME MWENZANGU.
●Mtu wa Kwanza kukutana na SHETANI live ni Mwanamke pamoja na kwamba walizungumza mengi na kula tunda kiukweli hatujui mengine waliozungumza mbali na kula tunda.
●MWANAMKE aliumbwa ukiwa usingizini wewe MWANAUME hujui ni kitu gani walichozungumza na Mungu kabla ya wewe kuzinduka.
●MWANAMKE ndiye aliyemwelewa Mungu alipoambiwa ana mimba ya Roho Mtakatifu wewe MWANAUME ulitaka kumkimbia badala ya kukabiliana na changamoto hiyo.
●MWANAMKE ndiye Mtu wa kwanza kwenda kuhakikisha kama kweli Yesu amefufuka na kusambaza habari.
●MWANAMKE ndiye anayeongoza kwa ushawishi mkubwa, Mwanaume huna ujanja mfano.
■Eva kwa Adamu
■Delila kwa Samson
■Ester kwa Ahasuero
■Raheli kwa Labani n.k
Usimuudhi Mke wako ana Siri kubwa sana usione kakaa na wewe anakuvumilia pamoja na ukatili wako.
Anaweza akatekeleza walichozungumza na Mungu au anaweza kutekeleza pia alichozungumza na shetani
Oohoo!
Tafakari Ndugu yangu ngoja na mimi niendelee Kutafakari....