B Prosper
JF-Expert Member
- Dec 16, 2016
- 2,183
- 3,539
Naandika haya nikiwa na machungu sana,
Siku hizi uaminifu umepotea sana tena ni adimu kama cent 5 hasa kwenye suala la pesa.
Mwaka jana nilikopesha sana watu na asilimia kubwa ni hawa "marafiki na workmates" siyo kwamba ninafedha hapana, hapa nilipo hata uwanja tu sina.
Mtu anakuja anakueleza matatizo yake na unamwambia kwakweli saizi sina kitu, anakubembeleza weeeee mwisho unamwonea huruma unaamua kuingia kwenye account na kumpa kiasi kadhaa.
Muda wa kurejesha ukifika sasa maelezo yanaanza kuwa mengi mara ooh subiri kidogo matikiti yapo shamba wiki ijayo naenda kuvuna, baada ya wiki ukimpigia simu hapokei na ikipokelewa anapokea mkewe tena anakuambia mwenye simu hayupo
Wengine sasa... Brother naomba nivumilie kidogo mwisho wa mwezi nitarekebisha then anaingia mitini. Juzi jamaa kanipigia simu (saizi yupo chuoni) ameenda kujiendeleza na ni mwajiriwa serikalini, aliniomba nimtumie hela kwani amekwama sana nikamjibu sina then nikakata simu yake, huyo jamaa mwaka 2017 nilimkopesha laki kwa makubaliano atarudisha mwisho wa mwezi lakini akatokomea kusiko julikana na mimi niliamua tu kusamehe.
Leo nimeamka nikapiga hesaba kama watu wote wangenirudishia hela yangu ningekuwa na kiasi fulani cha pesa nikabaki nahuzunika tu nakujiona kumbe mimi mjinga sana
Saizi sitaki kabisa mchezo na pesa yangu, hela yangu watapata ndugu wa damu moja na wazazi FULL STOP.
Siku hizi uaminifu umepotea sana tena ni adimu kama cent 5 hasa kwenye suala la pesa.
Mwaka jana nilikopesha sana watu na asilimia kubwa ni hawa "marafiki na workmates" siyo kwamba ninafedha hapana, hapa nilipo hata uwanja tu sina.
Mtu anakuja anakueleza matatizo yake na unamwambia kwakweli saizi sina kitu, anakubembeleza weeeee mwisho unamwonea huruma unaamua kuingia kwenye account na kumpa kiasi kadhaa.
Muda wa kurejesha ukifika sasa maelezo yanaanza kuwa mengi mara ooh subiri kidogo matikiti yapo shamba wiki ijayo naenda kuvuna, baada ya wiki ukimpigia simu hapokei na ikipokelewa anapokea mkewe tena anakuambia mwenye simu hayupo
Wengine sasa... Brother naomba nivumilie kidogo mwisho wa mwezi nitarekebisha then anaingia mitini. Juzi jamaa kanipigia simu (saizi yupo chuoni) ameenda kujiendeleza na ni mwajiriwa serikalini, aliniomba nimtumie hela kwani amekwama sana nikamjibu sina then nikakata simu yake, huyo jamaa mwaka 2017 nilimkopesha laki kwa makubaliano atarudisha mwisho wa mwezi lakini akatokomea kusiko julikana na mimi niliamua tu kusamehe.
Leo nimeamka nikapiga hesaba kama watu wote wangenirudishia hela yangu ningekuwa na kiasi fulani cha pesa nikabaki nahuzunika tu nakujiona kumbe mimi mjinga sana
Saizi sitaki kabisa mchezo na pesa yangu, hela yangu watapata ndugu wa damu moja na wazazi FULL STOP.