Usiku wa 900 itapendeza na Dr.Shika 9 Desemba

white hat

JF-Expert Member
Dec 16, 2016
3,323
2,487
Usiku wa 900 itapendeza ni shoo/hafla inayotarajiwa kufanyika 9 Disemba 2017
Uwanja wa Dar Live kumtambulisha dr.Shika kwenye muonekano mpya wakibilionea na Kumpongeza kwa kushindwa kushinda mnada wa nyumba za Lugumi
Watu kuanzia Elfu nne mpaka elfu tano wanatarajiwa kuhudhuria hafla hiyo pia Mgeni rasmi wa Halfa hiyo atakuwa ni aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Mh.Lawrence Masha

Pia kutakuwa na bendi ya twanga pepeta juma nature na wasanii wengine mbalimbali kama wa bongoflava n.k
Unaweza kumsikiliza waandaaji na Dr.Shika mwenyewe hapo chini

 
nicheke tuu
bora ucheke tu uongeze siku za kuishi tu
huyo mdada ndo kanivunja mbavu anakuambia ni hafla ya kumpongeza kwa kutangazwa kuwa mshindi wa mnada wa nyumba za Lugumi
 
Mnh haya bana inaonekana itakuwa shoo ya kukata na shoka.
Haya kiingilio sh ngapi
 
Kumbe nimegundua hakuna nchi duniani yenye watu wanye furaha kama bongo...
Mara ukipita huku wakuta na kigodoro watu wanafurahi, ukirudi huku fiesta, ukikatiza huku show ya makonda mcty hujakaa sawa ya kumpongeza dr shika kushinda mnada japo nyumba hakununua...
Twende kazi tz ya viwonder ndiyo ya awamu hii
 
Huyu mimi nilishatilia mashaka hata elimu aliyosema anayo ukiachilia mbali umri wake alipoenda kusomea udaktari Urusi akiwa na miaka 14.
 
Mnh haya bana inaonekana itakuwa shoo ya kukata na shoka.
Haya kiingilio sh ngapi
hapo kwenye video jamaa wamesema kawaida ni 5000 na VIP ni 15000
alaf mtu atakuambia eti vyuma vimekaza
 
Kumbe nimegundua hakuna nchi duniani yenye watu wanye furaha kama bongo...
Mara ukipita huku wakuta na kigodoro watu wanafurahi, ukirudi huku fiesta, ukikatiza huku show ya makonda mcty hujakaa sawa ya kumpongeza dr shika kushinda mnada japo nyumba hakununua...
Twende kazi tz ya viwonder ndiyo ya awamu hii
:D:D:D:D viwanda vya kiki
 
Hahaha Dr anakamata fursa waende zao awe makini asijegeuzwa fursa halafu baadae akajkuta wenzake wanasukuma mi audi yeye bado yuko vile vile kama wasanii flani
kwa matangazo aliyopiga na sehemu mbalimbali alizoalikwa saivi alitakiwa awe na mkwanja flani hivi sijui hata kama anajua kubargain kweli au wanamlalia tu.
sema wabongo wanajua kulalia sana usikute wanampa hela ya msosi na nauli tu halaf akiisha umaarufu ndio basi.
 
kwa matangazo aliyopiga na sehemu mbalimbali alizoalikwa saivi alitakiwa awe na mkwanja flani hivi sijui hata kama anajua kubargain kweli au wanamlalia tu.
sema wabongo wanajua kulalia sana usikute wanampa hela ya msosi na nauli tu halaf akiisha umaarufu ndio basi.
Watakuwa wanampa ela ya kawaida unaweza kukuta hakuna tangazo ambalo kalipwa hata milion 10
 
Back
Top Bottom