Usijaribu kusoma kozi hizi, utakufa njaa

AdvocateFi

JF-Expert Member
Jan 15, 2012
11,492
5,040
Bwana Yesu asifiwe wakuu..

Jamani nimeona ni vyema kutoa muongozo hasa kwa Form6 ambao mpo kwenye mchakato wa application za vyuo, kama kweli unapenda maisha yako na huna kaka wala Mama mbunge (Referee) nakuomba usisome kozi hizi.

Sociology, Political and Public Admnistration (PSPA), Public Admnistration (BPA), Conflict resolution, Mass communication (Mascom), International relation, Public relation, Law (LLB), Theology, Arabic language, Tax Management, Community development, Rural development planning etc.
NOTE:
Lengo langu si kukashifu mtu bali kutoa elimu.

Stay blessed.
 
Hahaha,hapo umeshataja course zote za arts,sijui watasoma nini sasa?but kwa ufupi umeongea ukweli mtaani hzo course kupata kazi ni bahati nasibu hasa hasa hio sociology,public na PSPA pia hio international relation sisy wng tokea 2011 yupo ubaoni hana hata kibarua

Kweli mkuu ni vyema watu waelewe hili suala mapema.
 
Mkuu hebu fafanua kwanini wasisome hizo kozi, pia toa madhara ya kusoma hizo kozi, usipo fanya hivyo watakulumu siku nyinge.

Sp

Mkuu nadhani Thread inajieleza tu yenyewe kwamba kwa mazingira ya sasa hizo kozi zina maelfu ya graduates kitaa tena wengine wana miaka mingi tu hivyo urahisi wa kupata ajira through hizo skillz zinazotokana na kozi hizo inakuwa ni utata mtupu hata tu kuitwa kwenye interview ni kwa mbinde.

Mostly, kozi hizo hazitoi directly and defined skillz inayomuwezesha mtu kujiajiri mfano PSPA labda uanzishe chama cha siasa kama Zitto na ACT.
 
Ongezea na Education maana napo jam kuanzia mwakani sijui itakuwaje maana shule zimejaa walimu wa arts mpaka balaaa miye nadhani tubuni njia mbadala maana hali ni teter

Education haina shida sana maana naskia kuna mchongo wa kufundisha shule za msingi.
 
Back
Top Bottom