Usijaribu kufunga ndoa kabla mwili na akili yako haijakomaa

Zero IQ

JF-Expert Member
Dec 21, 2016
13,917
24,674
Jana nilikuwa na jamaa yangu flani hivi tuliosoma wote College. Naweza kusema tulikutana kama bahati tu kwa sababu tangu tumalize mafunzo yetu hatujawahi kuonana.

Ni yule kijana ambae baada ya kumaliza chuo tu wazazi wake wakaforce aingie kwenye Ndoa (kwa mujibu wa maneno yake), kwa sababu kwao wanavihela hela kidogo. Ila binafsi siamini kwa sababu namjua vyema na moja ya kauli yake kubwa wakati tulivyokuwa chuo ni kuwa kabla hajafikisha miaka 24 atakuwa tayari amefunga ndoa, na ni kweli mwaka huu yuko na 25 tayari yupo kwenye ndoa mwaka mmoja na nusu.

Jamaa ni ameoa mke mzuri kweli lakini ukimtazama tu at first unajua kabisa hiyo ndoa kwake ni ya moto,
hana nuru tena usoni kama ile niliyoizoea kuiona wakati tuko chuo tunaunga unga elimu yetu.

Wakati ule Alikuwa mchangamfu aswaa lakini kwa sasa majukumu yamechukua nuru yake.

Tuliongea sana lakini neno lake kubwa kwangu na aliliongea kama utani na mimi nimelichukulia serious ni kwamba:

"Usijaribu kuingia kwenye Ndoa kwa sababu ya Tamaa, kwa sababu hutaki kumpoteza mpenzi wako kwa sababu ya ule uzuri wake, kwa sababu ya kufanya mapenzi kila unapohitaji au kwa sababu umeona flani anaishi kwa furaha na mkewe ukadhani ukioa na wewe utaishi kama wao. Ndoa ina mambo mengi na jambo kubwa usijaribu kufunga ndoa kabla mwili na akili yako haijakomaa.

Namnukuu "Natamani siku zirudi nyuma niache yale mawazo ya mimi kuoa ili nitafute maisha kwanza, nijipange nikiwa mwenyewe nikomae kimwili, kifikra na kiakili ndiyo nije na wazo la kuoa. Nioe kwa sababu ya kuanzisha familia na sio kwa sababu ya uzuri wa mwanamke, nioe kutafuta msaidizi wangu na sio kuoa kwa sababu ya kutaka kufanya mapenzi"

Mwisho wa kumnukuuu.

Vijana wenzangu wa kiume huo siyo utani, sisi tunatofauti kubwa sana na vijana wenzetu wa kike,
mwanamke anaweza kuolewa akiwa kwenye umri wowote kuanzia miaka 18 na akaishi vizuri kwenye ndoa,
lakini sisi wanaume kuoa na umri wa miaka 18-30 ni kujiongopea.

Miaka hiyo hapo kati ndio miaka ambayo kwa mwanaume ni ya kujipanga at least tufikilie kuoa tukiwa tayari tumefika miaka 30 plus.

Kwa sababu hata akili, mwili na matendo vitakuwa vimefika mahala.


Cc Zero IQ
 
Zero IQ,
Uoe una miaka 30+? Mtoto wa kwanza unampata anakuita ba mkubwa.

Mwanaume umefikisha 27 huna mtoto, huna maisha mazuri bado na mke pia huna? Mfano majaliwa yako ni kutoboa ukiwa 70s huko kama mmiliki wa KFC so na wewe utakua unaburuzana na mabinti hadi muda huo hutaki kua committed?

Sababu pekee inayotusumbua ni commitment, maana majukumu hata usipomuoa ila ni mtu wako ni utayavaa tu.
 
Billgate unajua alioa akiwa na miaka mingapi,huyo mmiliki wa Facebook juzi kati tu hapo ndio kamvisha pete mchumba wake unajua ana miaka mingapi?
Hapa unataka kuhalalisha nini? Two world class enterpreneurs unataka kuwafananishia ya kwamba hawakua na akili au majukumu yangechukua nuru zao?

Hapo kuna mmoja uhusiano na mtu wake ulikua tangu chuo.
 
Umenikumbusha jambo nililomuambia Anko jana usiku.

"Kijana yeyote wa kiume akishaanza maisha, akishaanza kujipanga kimaisha, akishanunua tu kiwanja, mwanamke huingia"

Na hapo ndiyo malengo yote yanapoanguka. Mipangilio yote ya maisha inapobadilika.

Sisemi tusioe lakini ishi na mwanamke, oa mwanamke baada ya kukamilisha malengo yako yote maana akishaingia kwenye maisha yako kuna mawili; malengo yako kufa au malengo yako kuchelewa mno.
 
hahahaha usitutisheeeeee in maalimu voice.

kimsingi usioe au kuolewa sababu eti ndo utakuwa na furaha.Msingi mzima wa majuto ya ndoa ni expectations naoa ili nipikie naoa ili nipewe penzi mda wote naoa,naoa ili nipate msaidizi,naolewa ili nipate mtu wa kunijali,naolewa ili niheshimike.Bullshitttttttttttt

Sio lazima upate hivo vitu kwenye ndoa ila ukivipata kwa mwenzA wako shukuru sana, be gratetul.

Hamna unaemdai upendo,hamna unaemdai lolote kubabeki zako face the truth,feel it and accept it.Sasa unaweza kufanya part yako, fanya wajibu yako wewe km mume au mke .She/he has a right to make mistake.Vumilia mpakautakaposhidwa sEPAAAA sio kwa ushauri wa mtu wala msukumo wa mtu bali maamuzi yako mweyewe.imeisha hiyo
 
Kuoa ni utumwa, nilijaribu kuwahi mapema nikakimbia nikaambulia mtoto.... sina ninachokosa kati ya vitu venye nilikuwa napata (ngono) so nitarudi tena baadae sana.
 
Zero IQ,

Zero nakusapoti sana, ndoa ina mambo mengi ya misukosuko na huwa haifanani kila mmoja nayakwake na mwenziye. Umri ukiwa mkubwa haswa above 30 kwa wanaume na above 25 kwa wanawake inasaidia sana watu kuwa na busara katika kukabiliana na migogoro ya ndani, na matatizo makubwa huwa ni kuoana hafu ndo mnaanza kuchunguzana hapo lazima mtaishia kugombana kama hamna busara.
 
Back
Top Bottom