Mzalendowadamu
JF-Expert Member
- Jul 10, 2016
- 218
- 318
Habari za wapambanaji wenzangu katika jukwaa hili.
Leo napenda tujadili kidogo juu ya hawa watu wanao jiita wahamasishaji wa biashara na ujasiriamali au kujiajiri. Binafsi nimekuwa nawafuatilia sana kuona kama naweza kupata chochote chenye kuweza inisaidia katika ujasiriamali au biashara lakini kinyume na matarajio ni kwamba sioni jambo lamaana sana, labda kwakua wengi huongelea ambayo nimeyapitia kwa muda mrefu. Hawa watu wamekua na nadhalia nyingi kuliko uhalisia na zaidi wamekua ni watu wa kusimulia mapito ya Matajiri wakubwa wa dunia kama moja ya nyenzo za kufanya uhamasishaji wao. Pia wachache wanajaribu kujielezea mapito yao binafsi mpaka kufikia walipo leo ingawa hata wao wengi hawaonekani kuwa walio fanikiwa au labda kwakua walipo ndipo walipo tamani kuwa ili kujihesabu walio fanikiwa.
Mada zao kuu zimekua kama zifuatazo. 1. Kujitambua wewe umekuja duniani kufanya nini 2.Kuchukua hatua 3. Kuwa tofauti 4. kuwa mbunifu na maengine machache.
Pia wapo wengine hujifanya kuelimisha na mwisho wa siku hutangaza biashara zao za bidhaa na kuwataka nyie wasikilizaji mjiunge nao muwae wauzaji wao, yaani anatoka kukuhamasisha ujiajiri kisha hapohapo anataka umtumikie. Wengine wanakuuzia kitabu ambacho kimendikwa hayohayo aliyo kuelezea.
Sikumoja nilihudhulia semina moja na baada ya hapo nilimuuliza jinsi ya kukuza biashara katika hali ya ushindani na wapinzani wangu. Kiukweli jibu halikutoka na nikaamua kukausha tu nisije kuharibu dili la mtu maana huo nao ni ujasiriamali.
Kwa uchunguzi wangu, Unatakiwa kuhudhulia semina moja tu, inatosha kama wewe unahisi labda umepungukiwa morari ya kazi tu. Hizi semina huwa ni zakuongeza au kukupa morari tu na wala sio kukufundisha biashara. Biashara zina sura tofauti kwa kila mmoja ingawa kuna mambo yanapatiwa suluhisho kwa njia zinazo shabihina kwa ukaribu. Yapo mengi katika biashara zaidi ya morari na pia zipo changamoto kubwa sana ambazo ukikumbana nazo hata uwe umehudhulia semina laki moja lazima morari ipoe.
Kuna ulazima wa watu kuingia field na kuja na mbinu mpya ya kufundisha Biashara na chngamoto zake kuliko kuishia kupeana morari tu.
Wahamasishaji wengi sio wafanya biashara ambao wanaweza kumshauri mtu kuligana na uhalisia wa mambo bali wengi ni wasaka fursa kwa kutumia mioyo na akili za watu waoga. Sasa tumehamasishwa vya kutosha na leo tuko ulingoni ila tunayo kumbana nayo huku hakuna sehem ya kujifunza namna ya kutatua changamoto halisi.
Semina za hamasa zikome sasa njooni mtufundishe biashara maana tayari tumeingia ulingoni na kuna mambo hamkuyasema, labda mlisubiri tuingie huku na tuyaone ili somo lieleweke vema.
Ushauri wangu, Usiingie biashara kwa mihemuko ya semina na mifano ya akina Jack Ma, Bii Gate na Jeff Bros. Jitahidi kujifunza kwa wafanya biashara wenzako walio kutangulia katika ulingo.
Karibuni tujadili.
Leo napenda tujadili kidogo juu ya hawa watu wanao jiita wahamasishaji wa biashara na ujasiriamali au kujiajiri. Binafsi nimekuwa nawafuatilia sana kuona kama naweza kupata chochote chenye kuweza inisaidia katika ujasiriamali au biashara lakini kinyume na matarajio ni kwamba sioni jambo lamaana sana, labda kwakua wengi huongelea ambayo nimeyapitia kwa muda mrefu. Hawa watu wamekua na nadhalia nyingi kuliko uhalisia na zaidi wamekua ni watu wa kusimulia mapito ya Matajiri wakubwa wa dunia kama moja ya nyenzo za kufanya uhamasishaji wao. Pia wachache wanajaribu kujielezea mapito yao binafsi mpaka kufikia walipo leo ingawa hata wao wengi hawaonekani kuwa walio fanikiwa au labda kwakua walipo ndipo walipo tamani kuwa ili kujihesabu walio fanikiwa.
Mada zao kuu zimekua kama zifuatazo. 1. Kujitambua wewe umekuja duniani kufanya nini 2.Kuchukua hatua 3. Kuwa tofauti 4. kuwa mbunifu na maengine machache.
Pia wapo wengine hujifanya kuelimisha na mwisho wa siku hutangaza biashara zao za bidhaa na kuwataka nyie wasikilizaji mjiunge nao muwae wauzaji wao, yaani anatoka kukuhamasisha ujiajiri kisha hapohapo anataka umtumikie. Wengine wanakuuzia kitabu ambacho kimendikwa hayohayo aliyo kuelezea.
Sikumoja nilihudhulia semina moja na baada ya hapo nilimuuliza jinsi ya kukuza biashara katika hali ya ushindani na wapinzani wangu. Kiukweli jibu halikutoka na nikaamua kukausha tu nisije kuharibu dili la mtu maana huo nao ni ujasiriamali.
Kwa uchunguzi wangu, Unatakiwa kuhudhulia semina moja tu, inatosha kama wewe unahisi labda umepungukiwa morari ya kazi tu. Hizi semina huwa ni zakuongeza au kukupa morari tu na wala sio kukufundisha biashara. Biashara zina sura tofauti kwa kila mmoja ingawa kuna mambo yanapatiwa suluhisho kwa njia zinazo shabihina kwa ukaribu. Yapo mengi katika biashara zaidi ya morari na pia zipo changamoto kubwa sana ambazo ukikumbana nazo hata uwe umehudhulia semina laki moja lazima morari ipoe.
Kuna ulazima wa watu kuingia field na kuja na mbinu mpya ya kufundisha Biashara na chngamoto zake kuliko kuishia kupeana morari tu.
Wahamasishaji wengi sio wafanya biashara ambao wanaweza kumshauri mtu kuligana na uhalisia wa mambo bali wengi ni wasaka fursa kwa kutumia mioyo na akili za watu waoga. Sasa tumehamasishwa vya kutosha na leo tuko ulingoni ila tunayo kumbana nayo huku hakuna sehem ya kujifunza namna ya kutatua changamoto halisi.
Semina za hamasa zikome sasa njooni mtufundishe biashara maana tayari tumeingia ulingoni na kuna mambo hamkuyasema, labda mlisubiri tuingie huku na tuyaone ili somo lieleweke vema.
Ushauri wangu, Usiingie biashara kwa mihemuko ya semina na mifano ya akina Jack Ma, Bii Gate na Jeff Bros. Jitahidi kujifunza kwa wafanya biashara wenzako walio kutangulia katika ulingo.
Karibuni tujadili.