Usiingie kwenye biashara kwa mihemuko ya semina na mifano ya akina Jack Ma, Bii Gate na Jeff Bros

Mzalendowadamu

JF-Expert Member
Jul 10, 2016
218
318
Habari za wapambanaji wenzangu katika jukwaa hili.
Leo napenda tujadili kidogo juu ya hawa watu wanao jiita wahamasishaji wa biashara na ujasiriamali au kujiajiri. Binafsi nimekuwa nawafuatilia sana kuona kama naweza kupata chochote chenye kuweza inisaidia katika ujasiriamali au biashara lakini kinyume na matarajio ni kwamba sioni jambo lamaana sana, labda kwakua wengi huongelea ambayo nimeyapitia kwa muda mrefu. Hawa watu wamekua na nadhalia nyingi kuliko uhalisia na zaidi wamekua ni watu wa kusimulia mapito ya Matajiri wakubwa wa dunia kama moja ya nyenzo za kufanya uhamasishaji wao. Pia wachache wanajaribu kujielezea mapito yao binafsi mpaka kufikia walipo leo ingawa hata wao wengi hawaonekani kuwa walio fanikiwa au labda kwakua walipo ndipo walipo tamani kuwa ili kujihesabu walio fanikiwa.

Mada zao kuu zimekua kama zifuatazo. 1. Kujitambua wewe umekuja duniani kufanya nini 2.Kuchukua hatua 3. Kuwa tofauti 4. kuwa mbunifu na maengine machache.
Pia wapo wengine hujifanya kuelimisha na mwisho wa siku hutangaza biashara zao za bidhaa na kuwataka nyie wasikilizaji mjiunge nao muwae wauzaji wao, yaani anatoka kukuhamasisha ujiajiri kisha hapohapo anataka umtumikie. Wengine wanakuuzia kitabu ambacho kimendikwa hayohayo aliyo kuelezea.
Sikumoja nilihudhulia semina moja na baada ya hapo nilimuuliza jinsi ya kukuza biashara katika hali ya ushindani na wapinzani wangu. Kiukweli jibu halikutoka na nikaamua kukausha tu nisije kuharibu dili la mtu maana huo nao ni ujasiriamali.

Kwa uchunguzi wangu, Unatakiwa kuhudhulia semina moja tu, inatosha kama wewe unahisi labda umepungukiwa morari ya kazi tu. Hizi semina huwa ni zakuongeza au kukupa morari tu na wala sio kukufundisha biashara. Biashara zina sura tofauti kwa kila mmoja ingawa kuna mambo yanapatiwa suluhisho kwa njia zinazo shabihina kwa ukaribu. Yapo mengi katika biashara zaidi ya morari na pia zipo changamoto kubwa sana ambazo ukikumbana nazo hata uwe umehudhulia semina laki moja lazima morari ipoe.
Kuna ulazima wa watu kuingia field na kuja na mbinu mpya ya kufundisha Biashara na chngamoto zake kuliko kuishia kupeana morari tu.

Wahamasishaji wengi sio wafanya biashara ambao wanaweza kumshauri mtu kuligana na uhalisia wa mambo bali wengi ni wasaka fursa kwa kutumia mioyo na akili za watu waoga. Sasa tumehamasishwa vya kutosha na leo tuko ulingoni ila tunayo kumbana nayo huku hakuna sehem ya kujifunza namna ya kutatua changamoto halisi.

Semina za hamasa zikome sasa njooni mtufundishe biashara maana tayari tumeingia ulingoni na kuna mambo hamkuyasema, labda mlisubiri tuingie huku na tuyaone ili somo lieleweke vema.

Ushauri wangu, Usiingie biashara kwa mihemuko ya semina na mifano ya akina Jack Ma, Bii Gate na Jeff Bros. Jitahidi kujifunza kwa wafanya biashara wenzako walio kutangulia katika ulingo.

Karibuni tujadili.
 
Kila kitu kina strengths na weekneses ,,binafsi wamenisaidia sikuwahi fikiria kama naweza kufanya biashara Lkn baada ya kuhudhuria semina hizi chuoni kwetu Mzumbe niliyachukua niliyoyaona yananifaa nikanunua na kitabu kimoja tu ,,baada ya kumaliza masomo mwezi July nimeingia ulingon mambo yanaenda ingawa changamoto zipo Lkn huenda bila bila watu hawa wengi tusingepata hamasa ya kufanya mambo mengine TOFAUTI na tuliyosomea ,,its possible!
 
Kila kitu kina strengths na weekneses ,,binafsi wamenisaidia sikuwahi fikiria kama naweza kufanya biashara Lkn baada ya kuhudhuria semina hizi chuoni kwetu Mzumbe niliyachukua niliyoyaona yananifaa nikanunua na kitabu kimoja tu ,,baada ya kumaliza masomo mwezi July nimeingia ulingon mambo yanaenda ingawa changamoto zipo Lkn huenda bila bila watu hawa wengi tusingepata hamasa ya kufanya mambo mengine TOFAUTI na tuliyosomea ,,its possible!
Nakubaliana na wewe, kama umenifuatilia vema hata mimi nimewahi hudhulia mara moja, na nimeshauri kuwa mara moja inatosha na kuchukua hatua. Tambua kuna watu wanahudhulia kila semina kwa mada zilezile za kuhamasishwa tu. Sidhani wewe hapo ulipo fikia unahutaji kuhamasishwa bali unahitaji kupewa mbinu za biashara zaidi. Asante kwa mchango wako, pamoja sana
 
I see, sijawahi kuhudhuria hizi semina za kibongo, binafsi naangaliaga semina za akina Kiyosaki mtandaoni, vitu wanavyoelekeza ni real na vinasaidia, sijui huko kwenye semina zenu wanawafundisha nini.
 
Nakubaliana na wewe, kama umenifuatilia vema hata mimi nimewahi hudhulia mara moja, na nimeshauri kuwa mara moja inatosha na kuchukua hatua. Tambua kuna watu wanahudhulia kila semina kwa mada zilezile za kuhamasishwa tu. Sidhani wewe hapo ulipo fikia unahutaji kuhamasishwa bali unahitaji kupewa mbinu za biashara zaidi. Asante kwa mchango wako, pamoja sana
Ninapingana na wewe kusema kuwa unahitaji kuhudhuria mara moja tu, kwa msingi kwamba huwezi kuelewa ujasiria mali kwa mara moja.. Labda umesema hivyo kwa kuzingatia gharama za hizo semina ( sijui wanatoza kiasi gani). Lakini ukihudhuria semina moja na ukadhani umeiva, kitaa lazima upotee..

Pia ninachokiona, wewe umehudhuria semina ya motivation tu, bado unahitaji kujua vitu vingi. Motivation(hamasa/morari)ni nzuri lakini kama hujui basics zingine haisaidii sana.
 
Nakubaliana na wewe, kama umenifuatilia vema hata mimi nimewahi hudhulia mara moja, na nimeshauri kuwa mara moja inatosha na kuchukua hatua. Tambua kuna watu wanahudhulia kila semina kwa mada zilezile za kuhamasishwa tu. Sidhani wewe hapo ulipo fikia unahutaji kuhamasishwa bali unahitaji kupewa mbinu za biashara zaidi. Asante kwa mchango wako, pamoja sana[/QUOT

Shukrani Mkuu nadhani semina hzi kama ulivyo sema zinatutia joto ya kufanya zaidi kujifunza ni kwenye ulingo wenyewe wakuu
 
Ukiona unshawishiwa sana kuingia kwenye fursa basi we mwenyew ndio fursa
Hapa kuna vitu viwili tofauti, anakupa mbinu za kwenda kujikwamua mwenyewe mtaani au anakushawishi kujiunga na kitu flani? The former is an educator, the later is a salesman.
 
Kuna Sean Combs, Eric thomas hawa watu ukiwasikiliza unakuwa masikini watakujaza mihasira na ukitizama muda uliopoteza ni mwingi kuliko uliobakia
Katika rules zao kuna - Surround yourself with greatness na create with authenticity mara get into lion mode
Matokeo yake unakufa masikini kuigaiga kubaya fanya yako
 
Kuna Sean Combs, Eric thomas hawa watu ukiwasikiliza unakuwa masikini watakujaza mihasira na ukitizama muda uliopoteza ni mwingi kuliko uliobakia
Katika rules zao kuna - Surround yourself with greatness na create with authenticity mara get into lion mode
Matokeo yake unakufa masikini kuigaiga kubaya fanya yako
Sijawahi kuwasikia hawa, fafanua kidogo mkuu mafundisho yao kama hautajali..
 
IMG-20180720-WA0009.jpg
 
Motivation speaker wengi Hawako realistic baina ya masomo na real situation in business. Pia wengi wao inachangia hawajawahi Fanya biashara Yeyote kwa muda mrefu. So hawana uzoefu kwa kile wanachokifundisha. Biashara honest ni tough sio simple maana changamoto zake if your nor strong enough unaclose business. Ukikutana na challenge ya wafanyakazi face to face Au kuibiwa Au masoko Au cost ya kuendesha Au what u invest Vs profit..etc.. Ndio utaelewa biashara ni kitu gani.
 
Sijawahi kuwasikia hawa, fafanua kidogo mkuu mafundisho yao kama hautajali..
Sean combs rules for success
(1) have a champion mindset
(2) be competitive
(3) know yourself worth
N.k
Eric thomas rules
(1) know you're amazing
(2) Ser strong goals
(3) Be driven to succeed
N.k hawa jamaa ni very good entrepreneur na nahisi mazingira yao yana favour wao kufanya lolote
Huku kwetu kuset goals tu miaka 6 na mengine mengine miaka 40 umefikisha bado haujaumwa malaria unakufa kizembe
 
Sean combs rules for success
(1) have a champion mindset
(2) be competitive
(3) know yourself worth
N.k
Eric thomas rules
(1) know you're amazing
(2) Ser strong goals
(3) Be driven to succeed
N.k hawa jamaa ni very good entrepreneur na nahisi mazingira yao yana favour wao kufanya lolote
Huku kwetu kuset goals tu miaka 6 na mengine mengine miaka 40 umefikisha bado haujaumwa malaria unakufa kizembe
Huyo Sean Combs si ndio mwanamziki anajiita P Didy? Hawa naona wako ki sports zaidi, wanafaa kuwamotivate wanamichezo..
 
Motivation speaker wengi Hawako realistic baina ya masomo na real situation in business. Pia wengi wao inachangia hawajawahi Fanya biashara Yeyote kwa muda mrefu. So hawana uzoefu kwa kile wanachokifundisha. Biashara honest ni tough sio simple maana changamoto zake if your nor strong enough unaclose business. Ukikutana na challenge ya wafanyakazi face to face Au kuibiwa Au masoko Au cost ya kuendesha Au what u invest Vs profit..etc.. Ndio utaelewa biashara ni kitu gani.
Huwa nasikitika sana, hivi kwa nini unakubali kufundishwa biashara na mtu ambae sio mfanyabiashara?
 
Shida kubwa ya kizazi cha nyakati hizi kimekosa subira na ustahimilivu....!!!

Subira ni moja ya nguzo ya mafanikio!! Ukiwa na subira na ustahimlivu utafanikiwa mambo mengi sana!!!....

Mambo huchukua muda kuweza kuwa!!!....

Hata hao waliofanikiwa leo ime wachukua miaka mingi kufika hapo walipo.....

Play your part and be patient
 
Huyo Sean Combs si ndio mwanamziki anajiita P Didy? Hawa naona wako ki sports zaidi, wanafaa kuwamotivate wanamichezo..
Biashara ni mchakato ambao mtu anajifunza kadri anavyoendelea kuifanya kulingana na changamoto anazokutana nazo!!!!

Hata mfanyabiashara hawezi kukufundisha biashara kwa kuwa inawezekana changamoto alizopitia sizo ambazo wewe unapitia kwenye biashara zako!!!!!

Ukitaka kuijua na kujifunza biashara fungua biashara!!!....utaimarika na kujifunza kadri siku zinavyosonga
 
Biashara ni mchakato ambao mtu anajifunza kadri anavyoendelea kuifanya kulingana na changamoto anazokutana nazo!!!!

Hata mfanyabiashara hawezi kukufundisha biashara kwa kuwa inawezekana changamoto alizopitia sizo ambazo wewe unapitia kwenye biashara zako!!!!!

Ukitaka kuijua na kujifunza biashara fungua biashara!!!....utaimarika na kujifunza kadri siku zinavyosonga
Ni kweli, njia nzuri ya kujifunza kitu ni kufanya, lakini, hakuna principles ambazo zina apply bila kujali mazingira au aina ya biashara?
 
Ni kweli, njia nzuri ya kujifunza kitu ni kufanya, lakini, hakuna principles ambazo zina apply bila kujali mazingira au aina ya biashara?
Biashara ni kitu cha ajabu sana!!!....

Mabadiliko na mafunzo unayapata kadri uanvyoifanya!!!!

Unaweza ukaanza na biashara hii ukajikuta baadae unabobea kwenye biashara nyingine ambayo hata hukuwaza kuifikiria
 
Biashara ni kitu cha ajabu sana!!!....

Mabadiliko na mafunzo unayapata kadri uanvyoifanya!!!!

Unaweza ukaanza na biashara hii ukajikuta baadae unabobea kwenye biashara nyingine ambayo hata hukuwaza kuifikiria
Ndio maana nikauliza, hakuna kitu kinachoweza kuniguide hata kama nimebadili biashara?
 
Back
Top Bottom