Usifanye hili kosa unaposalitiwa na Mkeo/Mwanamke wako

Mimi mtu akichepuka ni kesho yuko kwao na nampeleka mwenyewe hadi kwao na kuwapa sababu za kumrudisha mwanao baada ya hapo sipokei simu ya mtu yeyote kutoka kwa huyo mwanamke sina mda wa kukaa nae sijui nichelewe kuja, nipeleke nguo kwa dobi
Kua uyaone ..... nadhani umri wako bado mdogo haujaoa na hauna familia. Omba Mungu mambo kama hayo yasikutokee.
 
Nakubaliana nawee kuna wanawake manunda sana .
Ila kiasili, mpaka mwanamke awe nauwezo wakuhimil hayo, basi huyo ni konkiii !!!.


Wahivo , NAKUFUNGASHIA VILAGO UENDE KWENU, UENDE KUPANGA N.J UTAJUA MWENYEWE UKACHEPUKE HUKOHUKO.


Labda km unazungumzia Kanamume, kanakoabudu Papuchi na bado kalikupata kakaona kama kamekupata kwa bahati nasibu tu.

Kwa ufupi, kanaume, kadogooo, kaogaa, kanalialia, kabebibebi, kanasauti yakike, kanamiko lainiii, kanabadilisha boksa mara mbili kwa siku, kanajifanya kanamapenzi ya dhatiiii, kajingaaa, Bila shaka katakua Kahehe

Hapo mwishoni umesaka vita sasa
 
Yani kauli ya kwamba furaha yangu haihusiani na mume wangu inewakeraa wanaona kama vile ni wake zao wamesema hivyo
Nimesema kabisa mimi binafsi nimevuka hio level ya furaha yangu kumkabidhi mume wangu,either tugombane au tuwe na maelewano ndani Mimi nachukulia ni sehemu ya maisha haiwezi kunitoa furaha yangu
Nimegundua wanaume wanapenda tuwalilie yani comment yangu moja imewapa uchungu wengi mpaka nimeshangaa unadhani nimewashtua wake zao huko majumbani kumbe ni jf tu hio
Wanaume wa humu JF wako so insecure Yani hawapendi mwanamke anayejiamini, mwenye furaha zake na misimamo yake, akiandika tu humu wanaanza kushambulia kwa matusi Mara single mother na blah zisizo kuwa na kichwa Wala miguu.
Na siku wanawake tukitambua kuwa jukumu la kujipa furaha ni la kwake wanawake na sio wanaume wanawake tutapiga hatua.
Na wanaume hufurahia jinsi wanawake wakiteseka na kujiliza Liza kisa mwanaume, sasa wewe mwanamke ukiwa na furaha yako hamna mwanaume wa kukutesa, ila atajitesa mwenyewe loh
 
Wanaume wa humu JF wako so insecure Yani hawapendi mwanamke anayejiamini, mwenye furaha zake na misimamo yake, akiandika tu humu wanaanza kushambulia kwa matusi Mara single mother na blah zisizo kuwa na kichwa Wala miguu.
Na siku wanawake tukitambua kuwa jukumu la kujipa furaha ni la kwake wanawake na sio wanaume wanawake tutapiga hatua.
Na wanaume hufurahia jinsi wanawake wakiteseka na kujiliza Liza kisa mwanaume, sasa wewe mwanamke ukiwa na furaha yako hamna mwanaume wa kukutesa, ila atajitesa mwenyewe loh
Ndo maana nina furaha coz furaha haitokani na mwanamke


Si eti ndugu zangu
 
Poa Mkuu, ngoja niingie ,nione !!

Ila kwakua Tabia ni ngozi, changamoto ya Usaliti nitaihandle iviivi sidhan kama nitabadilika.


Nikweli kabisa kila ndoa ina changamoto zake, lkn ukweli nikua, Changamoto ya Uchepukaji, wengi sababu ni zile zile

Watu wanatofautiana kuzitatua ,ndo maana kuna mwengine atazuga kakasirikaa wee lkn mwisho wasiku atajirud kwa mkewe .

Mwingine yeye hawez kuhimil yeye anapiga na kuua au ulemavu.

Kwa sisi tunaopenda maisha yetu, aaahhhh Unaacha, unajipa muda, unavuta Kifaa kingine pasipo kujali ulitoa mahari kiasi gani.
Maisha ya ndoa sio rahisi kama mnavotoa maamuzi yenu humu jamvini, kueni myaone!
 
Mimi mke wangu anachepuka,na nikamgundua huyo mwanaume anayechepuka nae,nilinyamaza kimya,sijamuuliza mrs wala huyo bwana.Huyo bwana akaanza kunichukia mimi,maana ghafla akawa hanisalimii,tunakutana eapoti tukisafiri hanisemishi na kuna siku alinivyonza,mimi nimenyamza kimya hadi hii leo nipo kimya nawatazama tu,nikishika hamsini zangu.Sijalalamika kwa mtu yoyote hadi leo.Huyo bwana akateuliwa na rais kuwa mtu mkubwa mie ni kimya sana.
Kuna kitu naona kinamkera mrs wangu maana anaona waziwazi kuwa sijali na yeye ana hofu na mie lakini mimi nipo kimya kabisa
Duu mzee Kuna level Fulani umevuka... Hongera. Je bado unakula mzigo?? Huogopi anaweza kukudhuru kwa namna yoyote??
 
Lazima kuwe na matamanio kutoka kwa kila mmoja wenu nnapoingia kwenye ndoa.

Mnaamua kuwekana mbele kwa kila kitu. She/He comes first... Ilamunapoanza miaka mitano mpaka kumi ni matazamio probation period..

Mtu kwanza ajipende yeye.. kama hajipendi akijifanya anakuoenda sana anakuigizia.. mkipata watoto angalia handling ya watoto... Jinsi anavyo deal na wanawe (flesh and blood) ndivyo atadeal na ww uzeeni utakapokuwa unamuhitaji

Baada ya hapo.. ujanani mapitio tu ..fainali uzeeni.. kosa leo ujute kesho..
 
Hii ni ishara ya kiburi na majivuno ambayo kwa kiasi kikubwa huleta madhara hasi katika ndoa. Mtu mwenye tabia kama hii anaweza kufanya jambo baya kusudi akijua kuwa ataomba msamaha na atalazimisha kusamehewa maana mwenza wake atakuwa anajua kabisa kuwa asipo samehe basi mambo yanaharibika. Unapata muda wa kujutia kibaya ulichofanya?
Huyo ni nunda, kufikiri atajutia kosa ni sawa na kusubiri embe idondoke kutoka kwenye mnazi! Ni aina ya mabinti jeuri ni ksma kunguru wa zenji😂!
 
mbona mi hivyo vitu havinitishi,nikikuomba msamaha nina limit ya siku za kuomba after that utajijua mwenyewe kama utanisamehe au la,ila hizo drama za kutokulala chumbani etc poa tu tutaishi hivyo hivyo siku yakiisha sawa yasipo isha sawa pia

Hii ulioandika ni kwa wanawake wanao amini furaha wanaipata kwa mume tu,kwa mapigo hayo lazima wadate
Tabia za kutoka nazo kwa mama hizi
 
Huyo ni nunda, kufikiri atajutia kosa ni sawa na kusubiri embe idondoke kutoka kwenye mnazi! Ni aina ya mabinti jeuri ni ksma kunguru wa zenji😂!
Hawa ndio wale baba zao wamefanywa mazezeta na mama zao, yani mwenye sauti ni mama baba kafunikwa kwenye chungu
 
Kuna mambo yanasikitisha sana...

Samehe saba mara sabini...
Sababu binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
Nimejibu vizuri sababu ya kuwa hivyo
Mimi ni mtu napenda mambo yawe solved haraka labda ni moja ya mapungufu nilio nayo
Huwa sipendi drama
Nikuombe msamaha wewe upo busy kunitesa kisaikolojia ashong utasubiri sana
It’s either yes or no,una samehe au husamehi tumalizane

Note:sijatetea kitendo cha kuchepuka
Mimi nawashangaa kwanini mtumie Nguvu zote hizo kuhama chumba,kuchelewa kurudi,naona mnajitesa
@Maya Angelou unanipa burudani sana. Unajijua vyema.. na uzuri upungufu wako umeung'amua pia. Kudos.

Sema go getter as you call yourselfs ni aina ngumu sana kwenda nayo.. often other people's wellbeing/emotions/feelings don't count to you! Ambayo inakuwa ni entitlement.

Unakuwa mtu unayekubali kosa, ila haukubali consequences... Au ukizikubali unazitaka ziwe administered kwa namna inayofaa au unayotaka wewe.. :) that's bold.

Ndoa furaha na amani yako iko kwa mwenzi wako.. unaanzaje kulala au kula kwa furaha wakati mwenzako hayuko na raha wala furaha!?

Nadharia ya mwili mmoja ina maana sana.. huwezi ukawa na raha wakati mkono umevunjika .. ukasema kwakuwa mdomo haujavunjika wacha nile raha.. au ukae useme huu mkono lazima upone sasa hivi la sivyo ukatwe..kama tiba inachukua muda mrefu.. :) unanipata lakini!? :)

Anyways kudos nakutakia burdani jioni ya leo..

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom