safuher
JF-Expert Member
- Feb 11, 2019
- 11,161
- 15,835
Usije ukadharau wazazi wako mkuu, Wazazi ni watu wazito katika maisha yako,hakuna mwenye mwisho mzuri kwa kuwadharau wazazi wake, hiyo ndo kanuni ya ulimwengu.
Jiulize tu kuwa hapa duniani ulipo ulitaka mwenyewe uje au umekuja kwa sababu wazazi wako ndo walipanga uje?
Kama hukupanga wewe kuja hapa unadhani kuwa aliepanga wewe uje atafurahi kuona haumjali wala kumthamini?
Eti unasema una mambo mengi huwezi kuwasaidia wazazi wako,yani umepelekwa ugenini na waenyeji alafu unataka ujifanye ushaujua mji tayari, heshimu wazazi.
Unajua kuwa wazazi kibao wanatoa mimba lakini wazazi wako wakakukaushia uje nawe ushangae hapa duniani?
Unaposubiri mzazi akuombe ndo umpe unadhani na wao wangesubiri wewe uombe kuzaliwa ungekuepo?
Unaposema mzazi anaomba hela sana,msumbufu,analeta umasikini kwa kukutegemea wewe mtoto kwani wao hawakuona kuwa wewe mtoto wanaekuleta duniani kuwa utaleta umasikini?
Unaonaje wewe kuwahudumia watu ambao wanajjilea wenyewe na vile wao kukuhudumia wewe ambae pia wanakulea.
Usisubiri mzazi akuombe, msaidie mzazi uongeze furaha katika maisha yako.
Pesa ni takataka tu ambayo imepewa thamani na watu, thamani ni chakula mavazi na malazi.
Hakikisha wazee wako wanakula, wanavaa na kulala salama.
Jiulize tu kuwa hapa duniani ulipo ulitaka mwenyewe uje au umekuja kwa sababu wazazi wako ndo walipanga uje?
Kama hukupanga wewe kuja hapa unadhani kuwa aliepanga wewe uje atafurahi kuona haumjali wala kumthamini?
Eti unasema una mambo mengi huwezi kuwasaidia wazazi wako,yani umepelekwa ugenini na waenyeji alafu unataka ujifanye ushaujua mji tayari, heshimu wazazi.
Unajua kuwa wazazi kibao wanatoa mimba lakini wazazi wako wakakukaushia uje nawe ushangae hapa duniani?
Unaposubiri mzazi akuombe ndo umpe unadhani na wao wangesubiri wewe uombe kuzaliwa ungekuepo?
Unaposema mzazi anaomba hela sana,msumbufu,analeta umasikini kwa kukutegemea wewe mtoto kwani wao hawakuona kuwa wewe mtoto wanaekuleta duniani kuwa utaleta umasikini?
Unaonaje wewe kuwahudumia watu ambao wanajjilea wenyewe na vile wao kukuhudumia wewe ambae pia wanakulea.
Usisubiri mzazi akuombe, msaidie mzazi uongeze furaha katika maisha yako.
Pesa ni takataka tu ambayo imepewa thamani na watu, thamani ni chakula mavazi na malazi.
Hakikisha wazee wako wanakula, wanavaa na kulala salama.