Usiache kununua ardhi. Niliyojifunza Goba sikufanya makosa Madale

Usiache kununua ardhi. Niliyojifunza Goba sikufanya makosa Madale

Xi Jinping

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2023
Posts
9,299
Reaction score
27,767
Miaka ya 2005-2008 nilikuwa napita sana barabara ya Goba-Makongo Juu hadi Chuo. Kipindi hicho lile daraja la Goba kwenda Makongo Juu halijajengwa.

Plus ujana ulikuwa bado mwingi nikapuuzia tu eneo hilo. Itoshe tu kusema yalikuwa mapori, viwanja hata kuanzia 1mln kushuka chini ulikuwa unapata vikubwa tu. Goba kalikuwa kakijiji leo nikipita huwa naumia sana.

Ni kweli hata leo unaweza kupata maeneo hapo Goba lakini kwa gharama kubwa sana. Eneo ambalo hasa nyumba zilikuwa zimejengwa ni Makongo juu na wengi inaonekana walipachukulia poa sana Goba ila baada ya barabara ya lami tu kupita na madaraja kujengwa daaah maeneo yakawa hayashikiki.

Kuanzia miaka ya 2010s nilipoanza ujenzi Salasala nikawa napitapita sana njia ya Madale kukiwa pori kipindi hicho barabara ya vumbi wakati wa masika hupiti na gari hilo tope. Hapo ndipo nikasema sifanyi tena makosa ya Goba, nikajichanganya na madalali na wenyeji nikapata viwanja vikubwa hapo Madale kukiwa bado pori.

Sasa hivi lami imepita Madale, leo ukifika Madale viwanja vimepanda bei sana na inaenda kuwa kama Goba. Ukweli ni kwamba mpaka leo sijaheal kwa yaliyonikuta Goba.

Hapo Dar na Pwani usiseme sehemu mbali, mbali kutokea wapi? Na sio tu Dar na Pwani popote pale nunua ardhi ili mradi inafaa kwa makazi au kilimo.

Usiseme hakujachangamka nunua tu, wewe ni miongoni mwa watakaopachangamsha. Twenzetu Mabwepande.
 
Juzi tu Msumi palikuwa panauzwa 2m, 3m. Leo lami inajengwa hapashikiki tena.
Nilipita pande hizo niliona lami inajengwa, nikasema Msumi itakuwa ya moto, na hiyo lami itapitia Mbopo eneo ambalo watu walilichukulia poa sana then lami itakuja kuungwa pale Madale mwisho

Ina maana sasa hivi ardhi ya Mbopo nayo inaenda kupanda thamani
 
2003 Nilipelekwa kibaha kuoneshwa ardhi pale picha ya ndege. Nikafika eneo husika ni robo kilometer kufika lami
Ile ardhi ilikuwa ekari moja na nusu kasoro.. Yule mzee alitaka 1M tena kwa instalments
Kwenye draw ya gari nilikuwa na na kama 1.2 haina kazi. Yule mzee akanisihi sana nisipaache pale mahali na kama nina laki 2 nimpe kwanza
Kuna kasauti kakaniambia moyoni achana naye huyo anakupanga kwani utakuja kuishi lini huku kwa ujinga wa ujana nikakasikiliza kale kasauti
Nikamwambia mzee Leo sina hela ila nakupa hii 20,000 ya usumbufu.. Akaipokea kisha akasema asante lakini ukiweza ongeza 80,000 itimie laki nikuwekee hii ardhi utanukumbuka. Nikagoma
Tukaondoka na mtu niliyekuja naye kufika Kibaha container bar tukapiga ugali samaki wa nguvu
Tukaondoka mpaka Mbezi kufika pale tukaanza kupiga maji.. Tukaondoka kwenye saa 9 mchana
Kufika saa 11 jioni tuko Mama land bar External .. Bata likaendelea
Saa tatu usiku tukanyanyua kuelekea Moshi Bar Goms! Hiyo haikuwa na come back
Siku iliyofuata kuangalia balance nina kama laki7 na ushee
Mwaka 2016 nikapata kazi Kibaha na kuamua sasa kujiwekeza baada ya ujinga kunitoka, nikasema niende kwa yule mzee
Kufika pale nikakuta palishauzwa na kukatwa viwanja vya 20 kwa 20
Kilikuwa kimebaki kimoja tu bondeni na bei ilikuwa million 3 haipungui hata mia😂
 
Miaka ya 2005-2008 nilikuwa napita sana barabara ya Goba-Makongo Juu hadi Chuo. Kipindi hicho lile daraja la Goba kwenda Makongo Juu halijajengwa.

Plus ujana ulikuwa bado mwingi nikapuuzia tu eneo hilo.

Itoshe tu kusema yalikuwa mapori, viwanja hata kuanzia 1mln kushuka chini ulikuwa unapata vikubwa tu. Goba kalikuwa kakijiji leo nikipita huwa naumia sana.

Ni kweli hata leo unaweza kupata maeneo hapo Goba lakini kwa gharama kubwa sana.

Eneo ambalo hasa nyumba zilikuwa zimejengwa ni Makongo juu na wengi inaonekana walipachukulia poa sana Goba ila baada ya barabara ya lami tu kupita na madaraja kujengwa daaah maeneo yakawa hayashikiki.

Kuanzia miaka ya 2010s nilipoanza ujenzi Salasala nikawa napitapita sana njia ya Madale kukiwa pori kipindi hicho barabara ya vumbi wakati wa masika hupiti na gari hilo tope.

Hapo ndipo nikasema sifanyi tena makosa ya Goba, nikajichanganya na madalali na wenyeji nikapata viwanja vikubwa hapo Madale kukiwa bado pori.

Sasa hivi lami imepita Madale, leo ukifika Madale viwanja vimepanda bei sana na inaenda kuwa kama Goba.

Ukweli ni kwamba mpaka leo sijaheal kwa yaliyonikuta Goba. Hapo Dar na Pwani usiseme sehemu mbali, mbali kutoka wapi?

Na sio tu Dar na Pwani popote pale nunua ardhi ili mradi inafaa kwa makazi au kilimo.

Usiseme hakujachangamka nunua tu, wewe ni miongoni mwa watakaopachangamsha. Twenzetu Mabwepande.

Bro umeongea Ukwel mtupu.

Shida vijana ambao wanatakiwa kuwekeza (20's - 30's) bado wako Sinza , kinondoni kijitonyama na hawawez kujua haya.
Wanawaza Mamillion meng. Na kuyapata ndio mtihani.

Maeneo kama Mabwepande, mbopo, msumi, makabe, Kibamba na kule kibwegere . Ukiwa na 6 Mill unapata kiwanja kikubwa wastan wa 20*20.

Kwahiyo Ukiwa na 10+ Mill unapata kaeneo kakubwa tu kutosha kujenga nyumba.

Kijana wakat unasubiria Mill 100 za kununua kiwanja prime areas. Hebu anza na kuwekeza na kiwanja sehem za mbali.
You never know. Unaweza usipate hizo hela ukazeekea nyumba za kupanga.
 
2003 Nilipelekwa kibaha kuoneshwa ardhi pale picha ya ndege. Nikafikq eneo husika ni robo kilometer kufika lami
Ile ardhi ilikuwa ekari moja na nusu kasoro.. Yule mzee alitaka 1M tena kwa instalments
Kwenye draw ya gari nilikuwa na na kama 1.2 haina kazi. Yule mzee akanisihi sana nisipaache pale mahali na kama nina laki 2 nimpe kwanza
Kuna kasauti kakaniambia moyoni achana naye huyo anakupanga kwani utakuja kuishi lini huku kwa ujinga wa ujana nikakasikiliza kale kasauti
Nikamwambia mzee Leo sina hela ila nakupa hii 20,000 ya usumbufu.. Akaipokea kisha akasema asante lakini ukiweza ongeza 80,000 itimie laki nikuwekee hii ardhi utanukumbuka. Nikagoma
Tukaondoka na mtu niliyekuja naye kufika Kibaha container bar tukapiga ugali samaki wa nguvu
Tukaondoka mpaka Mbezi kufika pale tukaanza kupiga maji.. Tukaondoka kwenye saa 9 mchana
Kufika saa 11 jioni tuko Mama land bar External .. Bata likaendelea
Saa tatu usiku tukanyanyua kuelekea Moshi Bar Goms! Hiyo haikuwa na come back
Siku iliyofuata kuangalia balance nina kama laki7 na ushee
Mwaka 2016 nikapata kazi Kibaha na kuamua sasa kujiwekeza baada ya ujinga kunitoka, nikasema niende kwa yule mzee
Kufika pale nikakuta palishauzwa na kukatwa viwanja vya 20 kwa 20
Kilikuwa kimebaki kimoja tu bondeni na bei ilikuwa million 3 haipungui hata mia😂
Umenifanya nikacheka sana, ulichoandika kimetutokea wengi, kudharau mambo na kuona hayafai kwa mda huo. Ninapoishi leo isingekuwa ndugu yangu huenda wala nisingenunua. Nani aishi huku porini...hayo ndio yalikuwa maneno yangu!!
 
Miaka ya 2005-2008 nilikuwa napita sana barabara ya Goba-Makongo Juu hadi Chuo. Kipindi hicho lile daraja la Goba kwenda Makongo Juu halijajengwa.

Plus ujana ulikuwa bado mwingi nikapuuzia tu eneo hilo.

Itoshe tu kusema yalikuwa mapori, viwanja hata kuanzia 1mln kushuka chini ulikuwa unapata vikubwa tu. Goba kalikuwa kakijiji leo nikipita huwa naumia sana.

Ni kweli hata leo unaweza kupata maeneo hapo Goba lakini kwa gharama kubwa sana.

Eneo ambalo hasa nyumba zilikuwa zimejengwa ni Makongo juu na wengi inaonekana walipachukulia poa sana Goba ila baada ya barabara ya lami tu kupita na madaraja kujengwa daaah maeneo yakawa hayashikiki.

Kuanzia miaka ya 2010s nilipoanza ujenzi Salasala nikawa napitapita sana njia ya Madale kukiwa pori kipindi hicho barabara ya vumbi wakati wa masika hupiti na gari hilo tope.

Hapo ndipo nikasema sifanyi tena makosa ya Goba, nikajichanganya na madalali na wenyeji nikapata viwanja vikubwa hapo Madale kukiwa bado pori.

Sasa hivi lami imepita Madale, leo ukifika Madale viwanja vimepanda bei sana na inaenda kuwa kama Goba.

Ukweli ni kwamba mpaka leo sijaheal kwa yaliyonikuta Goba. Hapo Dar na Pwani usiseme sehemu mbali, mbali kutoka wapi?

Na sio tu Dar na Pwani popote pale nunua ardhi ili mradi inafaa kwa makazi au kilimo.

Usiseme hakujachangamka nunua tu, wewe ni miongoni mwa watakaopachangamsha. Twenzetu Mabwepande.
Mabwepande wazaramo kibao kule siendi mkuu
 
Milion 6 mkuu ukanunue kibwegere? Wakati malamba mawil huku kinyerezi mpaka m3 unapat eneo fresh
Bro umeongea Ukwel mtupu.

Shida vijana ambao wanatakiwa kuwekeza (20's - 30's) bado wako Sinza , kinondoni kijitonyama na hawawez kujua haya.
Wanawaza Mamillion meng. Na kuyapata ndio mtihani.

Maeneo kama Mabwepande, mbopo, msumi, makabe, Kibamba na kule kibwegere . Ukiwa na 6 Mill unapata kiwanja kikubwa wastan wa 20*20.

Kwahiyo Ukiwa na 10+ Mill unapata kaeneo kakubwa tu kutosha kujenga nyumba.

Kijana wakat unasubiria Mill 100 za kununua kiwanja prime areas. Hebu anza na kuwekeza na kiwanja sehem za mbali.
You never know. Unaweza usipate hizo hela ukazeekea nyumba za kupanga.
 
Juzi tu Msumi palikuwa panauzwa 2m, 3m. Leo lami inajengwa hapashikiki tena.
KUna jamaa alisema hawezi nunua Msumi ni chaka sana,,,,,amekuja mwaka juzi kakuta kuna umeme,,,anaanza kulia ati alilogwa.....miaka hiyo angeweza kupata hata heka moja....eti leo anawaambia madalali ana milioni tatu,,,duuuh,,,,kweli kalogwa....
 
Back
Top Bottom