Aliyepewa tenda ya kukusanya ushuru wa magari arusha ana njaa kali anakusanya ushuru hadi mochwari na vituo vya polisi hadi benki kuu na tra.Ccm mnatupeleka wapi?
Yaani huu ushuru ni kero hapa morogoro unapaki sehemu yoyote hata kama unaangalia pacha utakuta mtu wa kukusanya ushuru amefika....Huu ni ujinga kama munispaa inataka mapato kwanini wasijenge parking......Hii ni kero kwakweli. Na hata hizo pesa zinazokusanywa hatuoni maendeleo yoyote hii nchi tunaipeleka wapi? Viongozi hawaoni haya? au ndio miradi yao?
ni wapuuzi sana hawa watu wanaokusanya ushuru, hata ukiingia mahali ukakaa dakika kumi au tano lazima ulipe elfu moja, mimi kuna siku nimekataa kulipa na nikaondoka kwa sababu nilikuwa nataka kuibiwa kitendo cha kupaki nikamshusha mtu stand alikuwa anaelekea babati eti nikasikia wanakuja na myororor wao kwa nyuma wananifunga, ilitokea mtiti wa kufa mtu ikabidi waniachie wenyewe
Kwa kweli ushuru wa maegesho Hapa Arusha umekuwa kero kubwa ukienda stand kubwa ya mabus wanatoza ushuru usiku kucha mchana kutwa, kibaya zaidi wanatoza ushuru mpaka siku za sikukuu zakitaifa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.