Ushuhuda na ushauri kwa wenye tatizo la kupata mtoto...

Ramos

JF-Expert Member
May 13, 2010
498
130
Miaka kadhaa iliyopita nilileta posts nikiomba ushauri jinsi ya kukabiliana na hali ya kutokuwa na mtoto katika ndoa yangu kwa miaka kadhaa. Niliwashukuru, na naendelea kuwashukuru walionipa matumaini. Namshukuru Mungu kwani hatimaye, mapema mwaka huu mimi na mke wangu tulijaaliwa mtoto...
Kwa asilimia 100 naamini Mungu ndiye aliyetenda miujiza. Kama Mungu alitumia mkono wa mwanadamu pia katika hilo, basi naomba nimtaje Dr Kibona (simjui jina la pili) wa Dar. Ingawa mwanzoni tulimpuuzia Dr huyu anayetumia vidonge vya miti shamba, lakini baadaye (pengine kwa kuongozwa na Mungu), mke wangu alikuja kufuata ushauri na kwenda kumtembelea, na ingawa mimi nilitakiwa pia niende kuchekiwa na kupewa dawa, sikufanya hivyo (pengine kukata tamaa? sijui)...
Sitaki kueleza mengi, lakini waliomshauri mke wangu kwenda huko, walishuhudia kuwa wanandoa wengi walifanikiwa baada ya kutumia vidonge kutoka kwa huyu jamaa. Na hapa ninapoandika, marafiki zetu wawili (ndoa mbili tofauti), ambao tuliwashauri waende kwa Dr huyu, baada ya mke wangu ku-conceive, nao walifanikiwa, mmoja ameshajifungua na mwingine ana ujauzito mchanga siku miezi kama mitatu baada ya kuanza kutumia dawa...

Kwa bahati mbaya sijui hasa ofisi yake, lakini najua clinic yake ipo Dar, maeneo ya Ubungo au Shekilango ( I am not sure). Kwa ambao wana tatizo na wanadhani wako tayari kutest hiyo option, wajaribu.

Asanteni...
 
Kama you really intend this post to be useful, please weka contacts za huyo DR. maana unakuwa kama unaturingishia tu Lol
 
Kama you really intend this post to be useful, please weka contacts za huyo DR. maana unakuwa kama unaturingishia tu Lol

Nadhani ameeleza kuwa yeye hakuhusika sana na Dr huyo, bali mke wake. Nadhani kama mtu atahitaji msaada wake anaweza kuwasiliana naye zaidi...
 
Huyu Dr. Kibona hata mimi nampenda kwanza anajiamini afu ana hofu ya Mungu anakwambia usiogope kwenda kwake eti kisa una hela ndogo anakwambia wewe nenda mtajuana hukokuko hata Ushauri atakupa pia huwa mara moja moja sana kuonekana kwa Tv hasa channel 10!
Mi namkubali coz akiwa on air kwa tv atakufundisha dawa zingine za kujitengezea nyumban (home made) wewe mwenyewe kama ilikuwa kwa Isaack Ndodi
lkn Dr. Kibona anataka kuwasaidia waTz na si biashara
na ametoa Vitabu vingi kwa matoleo kinaitwa: Tulejee Edeni
na mimi nina kitabu hiki kidogo tu! Lkn mafua,kikohoz,malaria nk tokea 2010 haya magojwa nimeyasahu!!

Kama you really intend this post to be useful, please weka contacts za huyo DR. maana unakuwa kama unaturingishia tu Lol

hii hapa mkuu utajifunza mengi dr hanaga umimi

Dr. Kibona Dr.Kibona Herbalist
 
Back
Top Bottom