USHUHUDA: Kuku wa kienyeji (Pure) - Biashara kichaa isiyo na tija

Nahitaji jogoo kwaajil ya mbegu.. (ni PM Kama upo mkoa wa KAGERA/Mwanza) Nataka nianze kufuga kuku wa kienyeji! Banda tayari ninalo na mitetea 20 ninayo
 
Kuna ukweli katika maelezo ila pia kuna mistakes ulizofanya kama kuwaacha matetea na vifaranga..!

Na kutochanganya chakula chako mwenyewe chenye ubora.

Vifaranga ungevitenga vyenyewe nakuwekea bulb au chemli hata kama viko 300 na kuwapa chick mash...unamwacha mama yao awahi kutaga tena akiwa na majogoo.
 
Doh..kuna mdau alinambia nianze na kuku kumi tu baada ya mwaka ntakua bilionea
 
Hakuna kitu hapo.... Ujanja ujanja tu....

Hakuna biashara isiyokuwa na faida....

Ni suala la umakini na kuthubutu tu.

Kuku wa kiemyeji kutaga mayai 7 si kweli!!!!!

Kuku wa kienyeji anayekula vizuri hutaga hadi mayai 15-18.... Inategemea na ufugaji wako na teknik...

Kuhusu ugumu wa kutunza mayai pia si kweli....

Yai la kienyeji linakaaa hata mwezi mzima bila kuharibika...

Kuku hukalia mayai kuanzia 9 na kuendelea... Inamaana anakalia yai viza wakati daily ndio hutaga...?

Kuku wanalipa wadau... Na mimi nafanya iyo busineaa... La msingi ni kuchagua sehem bora ya kufuga... Masokko... Chakula na maji ya kutosha tu.
Mkuu Mimi Nina kuku 2 wanataga simchezo yaani mayai 30 na Kitu kila mmoja
 
Mkuu

Mkuu acha umesema kumekuwa na watu ambao ni wapotoshaji Kwa sababu tajwa hapo juu.
Kwanza niseme wewe si mbunifuu Kwenye ufugani unaonekana ni mbabaishaji na umelenga kuitangaza hiyo biashara yako yamachotara.
Okey nianze na hoja yako number moja kuhusu utagai wa kuku wa kienyeji.
Kama mjasiriamali ulipaswa kutoa elimu ni namna gani tunaweza mfanya kuku wakienyeji akatutagia mayai mengi zaidi Kwa mwaka.
Kwani Mimi nawafuga wote hao kienyeji na chotara na hakuta tofauti kubwa Kwenye utagaji wao Kwa mwaka.
Kwanza namna yakumfanya kuku wa kienyeji akupe mayai mengi Kwa mwaka yakupasa kufanya yafuatayo.
1:Kama Una kuku tuseme mmoja ndo umeanza nae na ameanza kutaga. Akianza kulalia mpe mayai alalie Kwa hizo siku 21 then akiangua vifaranga mnyanganye vitunze Kwenye brooder. Mama mzazi mchanganye na majogoo.
Hapo ataanza kutaga soon na utaongeaza uzalishaji kidogo.
2: Kama Una kuku wengi kuanzia kumi nakuendelea hapa kuna njia mbili.
i. Kuku wakitaga kusanya mayai Kwa idadi utakayo pata. Theni unashauriwa upeleke mayai Kwenye mashine yakutotoleshea vifaranga aka incubator.
Kufanya hivyo utakuwa umesave mda wa kulalia na mda wakutunza vifaranga.
Kwa kawaida kuku akimaliza taga na ukamnyima kulalia Kwa kumuweka sero Kwa wiki moja Ile Hali yakulia anaisahau na anaanza maisha mengine mapya yakuanza kutaga baada ya wiki mbili au tatu. Hali hii inaweza kukupa wastani mzuri wa mayai Kwa mwaka na ni zaidi ya mayai Mia Kwa kipindi cha mwaka.
2: Vile vile hakikisha kuku wako unawapa vyakula Bora vyenye madini yote ili kuongeza virutubisho vyakutosha mwilili.
Hali hii pia itamfanya aongeze uzalishaji wa mayai.
3: Hakikisha unawapatia chanzo Kwa wakati hapo itakusaidia kupunguza vifo na kumaintain uzalishaji wako.
4: Hakikisha mazingira Yao ni masafi kuanzia mabanda, maji ya kunywa vyombo etc. Kuku wanaathiriwa Sana na magonjwa ya tumbo na kuku akiwa mgonjwa hata uwezo wa kutaga unaoungua.
So kufanya hivyo kutakusaidia kuwa na idadi nzuri ya mayai pia.

Naomba kusema kwamba hata hao chotara unaosema wanataga mayai mengi ukikosea kuwafuga kuanzia mwanzoni utagaji wao unaweza kuwa mdogo kuliko hata wa kuku wakienyeji.

Nasema hayo kwani kuku wote hao Mimi nawafuga.
Nafuga kuku kienyeji pure
Nafuga Kuroila ,Kenbro na saso
Nafuga Kuchi, bata bukini,mzinga ,bata kienyeji na kanga.
Changamoto hazitofautiani.
Mkuu Nimekusomaa vizurii, natumaini naweza pata mengi zaidi kutoka kwako

Daima toa bila kukumbuka na Pokea bila kusahau
 
Kumekuwa na upotoshaji kwa baadhi wa watu wanaojiita wataalamu wa ujasiriamali, hasa wanaofanya shughuli za ufugaji kwa maandiko ya whatsapp bila kuwa na hata kuku mmoja bandani.

Nimesukumwa kuandika bandiko hili hapa kutokana na jumbe mbali mbali za uufugaji wa kimtandao unaoshawishi vijana kuwa watatajirika mapema kwa shughuli za ufugaji kwa kuanza na kuku wa kienyeji kumi na moja na kuweza kupata Zaidi ya kuku miatatu ndani ya kipindi cha mwaka mmoja wa uzalishaji. Hoja yao inaweza kuwa sahihi, ila ningependa kusisitiza mafanikio katika ufugaji hayapo katika idadi ya kuku unayomiki, bali ni namna ulivyoweza kumanage biashara ya ufugaji.

Hoja yangu leo hapa ni kwamba, Biashara ya kuku wa kienyeji hailipi na nikupoteza muda wako. Na nitatetea hoja yangu kwa mifano hai na uzoefu wangu katika ufugaji.

Biashara ya Mayai. (idadi isiyo na tija kibiashara)

Kwa asili ya kuku wa kienyeji,huwa wanatabia ya utagaji wa mayai 7-10 na mara nyingi ni siku kwa siku 10 mfululizo, utamiaji -siku 21, na uleaji wa vifaranga - siku 50-60. Hii inampelekea kwa kuku mmoja kuweza kutaga wastani wa mayai 35-50 kwa mwaka kwani anapoteza muda mwingi kwa shughuli za utamiaji na malezi ya vifaranga badala ya kutaga. Idadi hii ya mayai haina tija kibiashara kwani kuku mmoja anaweza kukuzalishia tray 1 mpka mbili kasoro pekee kwa mwaka ambayo kwa bei ya soko si Zaidi ya shilingi za kitanzania 20,000 tu kwa mwaka.

Changamoto kwenye soko la mayai ya kienyeji. (Uhifadhi wa mayai)

Mayai ya kienyeji ni kati ya bidhaa ngumu Zaidi kuhifadhika. Ikumbukwe kuwa tofauti na mayai ya kisasa, mayai ya kienyeji huwa yamerutubishwa na majogoo. Hivyo kuharibika ndani ya muda ya week moja au pungufu kama hayatatuzwa katika mazingira salama kwaajili ya utunzaji. Kipindi cha joto kali, mayai haya huanza kujitenenezea kifaranga au mishipa ya damu ambayo baada ya muda mfupi hugeuka viza na kutofaa kwa matumizi tena.

Kwa uzoefu wangu binafsi, nilianza kusambaza mayai ya kienyeji kwenye supermarkets miaka mitatu iliyopita. Nilipata changamoto kubwa sana ya kubadilisha mayai mara kwa mara kwani mteja akichukua yai viza ni kumpoteza kabisa. Hii ni changamoto ya kwanza ambayo mpaka sasa bado inasumbua wafugaji wengi.

Bei juu kwa mayai ya kienyeji

Gharama za mayai husika, bei ya mayai ya kienyeji iko juu ukilinganisha na gharama za mayai ya kuku wa kisasa. Soko kubwa la mayai ni pamoja na vibanda vya chips, migahawa na hoteli. hawa wanauhitaji mkubwa sana wa mayai na soko liko juu muda wote wa mwaka.

Soko la mayai ya kienyeji lipo Zaidi kwenye households(soko la familia) hasa kwa vigezo vya kuzingatia afya zaidi. Soko hili la familia sio kubwa, ni soko dogo na mara nyingi hutumia tray moja kwa kipindi cha wiki mbili au Zaidi. Kwa mzalishaji mkubwa wa mayai ya kienyeji ni lazma awe na soko la familia pana Zaidi kuweza kupata faida ndogo, nasema faida ndogo maana ili kuzalisha mayai tray kumi (mayai 300) kwa siku, utahitaji Zaidi ya matetea 700 mpaka 1000 ya kienyeji pure. idadi ambayo ni kubwa kuliko idadi ya mayai yanayopatikana.

Biashara ya Nyama

Na declare interest, mimi pia ni msambazaji wa nyama ya kuku wa kienyeji, hivyo naongea kwa uzoefu, na niko tayari kukosolewa. Pamoja na kufugwa katika misingi ya kijani (organic rearing), iyo pekee haitoshi kumpa thamani inayostahili huyu kuku sokoni.

Thamani ya kuku sokoni ni uzito alio nao, organic component ni jambo la ziada lililo muhimu pia. tunavyo jadili bei ya soko ya kuku huyu ni lazma tumliganishe na gharama za bidhaa pinzani zilizoko sokoni. Haitawezekana kumuuza kuku mwenye kilo moja au pungufu kwa bei ambayo tunashawishiana humu ya 15,000-20,000 wakati bidhaa pinzani (nyama nyeupe) kama samaki sato toka mwanza wanauzwakwa 7,500 kwa kilo, au kitimoto, nyama ya ngombe ambazo nazo kilo ni 7,500-8,000.

Hivyo basi, hoja yangu hapa ni uzito wa kuku husika. Ukiachana na jamii chache za kuku wa kienyeji (kuchi etc) wenye uzito mzuri, majority ya kuku pure wa asili/kienyeji kwa majogoo huwa na pungufu ya kilo moja na nusu. Kumbuka uzito wa kuku hawa sio kwasababu ya malisho duni, laah hasha, bali ni kutokana na vinasaba (genes) vyao kuwafanya kuwa na maumbo madogo madogo. kwa kuku wa aina hii, sitegemei mfugaji kama atafanikiwa kuwapeleka sokoni na kuweza kupata bei nzuri toka kwa mlaji wa mwisho.

Nini kifanyike?

Ili ufugaji uwe wenye tija kibiashara ufanyike, ni lazma wafugaji tuamke na kuachana na ufugaji wa kuku hawa asilia kwani hawana tija. Nikisema hivi simaanishi watu waache kufuga, hapana, ila wafuge aina /breeds za kuku zenye tija kibiashara. Kuku pekee unaoweza kuwafuga kwa mbinu za kienyeji na bado wakakuletea mfugaji faida nzuri kibiashara, ni kuku aina ya chotara (cross breeds). Hii ni aina ya kuku wenye sifa zote za ukienyeji kwa misingi ya mbinu zao za kuwafuga pamoja na namna walivyo nauwezo wa kuhimili mazingira hasa ya vijijini.

Kuna aina mbalimbali ya kuku hawa ikiwamo Black/ white australorps, kroiller, Rhodes island red, red hamshire, Sussex etc. Hawa ni kuku ambao wanaserve purpose zote za mayai na za nyama. Mfano kuku aina ya black/white australorps wao wanauwezo wa kutaga mpaka mayai 250 kwa mwaka, tofauti na wa kienyeji, mayai ya kuku hawa huwa makubwa na yenye kasha jeupe na kiini cha njano kama utawafuga kwenye mazingira na mbinu asilia (za kienyeji).

Ukilinganisha uwezo wa utagaji wa kuku hawa utagundua utagaji wao ni Zaidi ya asilimia 500% ukilinganisha na ule wa kienyeji pure. Idadi hii ya mayai toka kwa kuku mmoja kwa mwaka, anaweza kumwezesha mfugaji kuzalisha mayai kwa wingi na kushusha Zaidi bei ya mazao yake (mayai) kuwa chini kuweza kuliteka soko kwa urahisi Zaidi. Kumbuka, bei ya juu ya mayai ya kienyeji ni kwaajili ya kulipia gharama kubwa za utunzaji wa kuku huyu ilihali utagaji wake ni hafifu.

Pili, kuku hawa wana nyama nyingi Zaidi kuliko hawa wa kienyeji kwa majogoo hufikia mpaka uzito wa kilo 3-3.5. huku matetea hufikia kilo 2-2.5 na huwa na nyama nzuri, iliyokomaa vyema na yenye ladha. kwa uzito huu kwa majogoo, kuku hawa uuzwa kwa bei ya 20,000 - 25,000 wakiwa hai. bei ambayoni kwa mujibu wa bei ya soko kwa makadirio ya shilingi 8,000 kwa kilo kwa nyama nyeupe.

Mapungufu

Pamoja na ubora wa kuku hawa katika ufugaji wa kibiashara, kuku hawa pia wanachangamoto mbali mbali ikiwemo kutokuwa na uwezo wa kutamia. Pamoja na hii kuwa changamoto pia ni fursa kwani kwa yeye kutotamia kunamwongezea nafasi ya yeye kuendelea kutaga mara nyingi Zaidi bila kupumzika. Hivyo changamoto hii ni faida kwa mfugaji anaelenga kufuga kwa tija. Kwa vile mayai haya huwa yamerutubishwa na majogoo, nirahisi kwa mfugaji kuongeza idadi ya kuku kwa kupitia kutotolesha kwa mshine za kuangulia vifaranga au kumpa kuku mwingine ayatamie kwa niaba.


Neno la kufungia:

“ I think I touched a raw nerve when I said farming is NOT cool! I believe farming takes a lot of HARD work and dedication. Lets not lie to the youth that they'll become instant millionaires when they get into farming. It becomes "cool" once you master the trade......” caleb

Ufugaji unalipa ukiweza kuibudu biashara ya ufugaji,


Kwa ushauri Zaidi kuhusu shughuli za ufugaji, tuwasiliane kwa namba 0755815174. pia pata fursa kusoma ya Makala mbali na utaalamu kutoka kwenye mtandao wetu www.instagram.com/becky_chicks or www.facebook.com/becky_chicks

Nimejaribu kuattach picha za baadhi ya kuku bora wanaofaakufugwa kienyeji na wakaleta tija kibiashara hapa chini. Neno langu si sharia, nakaribisha Michango

View attachment 385750
View attachment 385751
View attachment 385752
View attachment 385753
View attachment 385754
Uko sahihi mkuu. Kama unataka pressure tegemea kuku.
Kuna shida mbili au tatu katika ufugaji wa kuku.
1.Kuna magonjwamengi sana, hata ukichanja, kuna dawa za chanjo ambazo ni fake (feki) kwenye soko letu. Hivyo unaweza kuchanja na bado wakafa.wakati mwingine unapata vifaranga ambao wana maambukizi toka kwa msambazaji wa vifaranga Ukifanikiwa katika hatua hii, unapata shida ya pili
2.Masoko. Kuna matapeli wengi sana wanajipangia bei ya kuku na mazao yake. wataomba uwape kuku wakauze kisha ukachuke hela, hapo imekula kwako
3.Kuna hawa watu wenye mashine za kutotolesha vifaranga wa kienyeji nao ni hatari. unapeleka mayai 100 unapata vifaranga 30 ,mengine yoote unaambiwa viza
 
Asante sana mtoa mada daah 2016 nilikua siwaz haya kabisa kumbe kuna watu wanapeana madini tu uku, hongereni sana wachangiaji nimejitahidi sana kusoma comments

Kwa ufupi najiandaa kufanya ufugaji wa kuku, na mm nilikua nawaza kuku wa kienyeji na hao chotara, mpaka napata uzi huu ilikua katika kutafuta maarifa
Natarajia kuoata eneo kama heka moja hivi lipo mbali na makazi ya watu

Naomba kupata a be che kuanzia kwenye structure ya eneo hili pia mabanda ndani yakaaje, nilisikia kuku wanapenda kuning'inia
Hapa mm najua mtaji ni iyo heka moja nafasi nafasi nafasi ni muhimu sana

Je, hamna shida kuweka chotara na kuku wa kienyeji sehemu moja?

Jinsi ya kutafuta masoko nifanyeje?

Jinsi ya kuandaa chakula cha kuku, kuna mdau pale alitoa website lakini chini nikaja kuona kuna mtu akasema iyo website haifunguki

La mwisho hao kuku wa kienyeji nawapataje kwa hapa dar na pia chotara nawapataje na bei zake pia

Natanguliza shukrani zangu na mbarikiwe sana ndugu zangu
Ginner
mfuga kuku
@
 
black austrolop nimetembelea kwenye blogs na web za wabongo naona wanamterm kama ni kuku wa malawi, je ni kweli kuku weusi maarufu kama wa malawi ndio breed ya black austrolop?
 
Kumekuwa na upotoshaji kwa baadhi wa watu wanaojiita wataalamu wa ujasiriamali, hasa wanaofanya shughuli za ufugaji kwa maandiko ya whatsapp bila kuwa na hata kuku mmoja bandani.

Nimesukumwa kuandika bandiko hili hapa kutokana na jumbe mbali mbali za uufugaji wa kimtandao unaoshawishi vijana kuwa watatajirika mapema kwa shughuli za ufugaji kwa kuanza na kuku wa kienyeji kumi na moja na kuweza kupata Zaidi ya kuku miatatu ndani ya kipindi cha mwaka mmoja wa uzalishaji. Hoja yao inaweza kuwa sahihi, ila ningependa kusisitiza mafanikio katika ufugaji hayapo katika idadi ya kuku unayomiki, bali ni namna ulivyoweza kumanage biashara ya ufugaji.

Hoja yangu leo hapa ni kwamba, Biashara ya kuku wa kienyeji hailipi na nikupoteza muda wako. Na nitatetea hoja yangu kwa mifano hai na uzoefu wangu katika ufugaji.

Biashara ya Mayai. (idadi isiyo na tija kibiashara)

Kwa asili ya kuku wa kienyeji,huwa wanatabia ya utagaji wa mayai 7-10 na mara nyingi ni siku kwa siku 10 mfululizo, utamiaji -siku 21, na uleaji wa vifaranga - siku 50-60. Hii inampelekea kwa kuku mmoja kuweza kutaga wastani wa mayai 35-50 kwa mwaka kwani anapoteza muda mwingi kwa shughuli za utamiaji na malezi ya vifaranga badala ya kutaga. Idadi hii ya mayai haina tija kibiashara kwani kuku mmoja anaweza kukuzalishia tray 1 mpka mbili kasoro pekee kwa mwaka ambayo kwa bei ya soko si Zaidi ya shilingi za kitanzania 20,000 tu kwa mwaka.

Changamoto kwenye soko la mayai ya kienyeji. (Uhifadhi wa mayai)

Mayai ya kienyeji ni kati ya bidhaa ngumu Zaidi kuhifadhika. Ikumbukwe kuwa tofauti na mayai ya kisasa, mayai ya kienyeji huwa yamerutubishwa na majogoo. Hivyo kuharibika ndani ya muda ya week moja au pungufu kama hayatatuzwa katika mazingira salama kwaajili ya utunzaji. Kipindi cha joto kali, mayai haya huanza kujitenenezea kifaranga au mishipa ya damu ambayo baada ya muda mfupi hugeuka viza na kutofaa kwa matumizi tena.

Kwa uzoefu wangu binafsi, nilianza kusambaza mayai ya kienyeji kwenye supermarkets miaka mitatu iliyopita. Nilipata changamoto kubwa sana ya kubadilisha mayai mara kwa mara kwani mteja akichukua yai viza ni kumpoteza kabisa. Hii ni changamoto ya kwanza ambayo mpaka sasa bado inasumbua wafugaji wengi.

Bei juu kwa mayai ya kienyeji

Gharama za mayai husika, bei ya mayai ya kienyeji iko juu ukilinganisha na gharama za mayai ya kuku wa kisasa. Soko kubwa la mayai ni pamoja na vibanda vya chips, migahawa na hoteli. hawa wanauhitaji mkubwa sana wa mayai na soko liko juu muda wote wa mwaka.

Soko la mayai ya kienyeji lipo Zaidi kwenye households(soko la familia) hasa kwa vigezo vya kuzingatia afya zaidi. Soko hili la familia sio kubwa, ni soko dogo na mara nyingi hutumia tray moja kwa kipindi cha wiki mbili au Zaidi. Kwa mzalishaji mkubwa wa mayai ya kienyeji ni lazma awe na soko la familia pana Zaidi kuweza kupata faida ndogo, nasema faida ndogo maana ili kuzalisha mayai tray kumi (mayai 300) kwa siku, utahitaji Zaidi ya matetea 700 mpaka 1000 ya kienyeji pure. idadi ambayo ni kubwa kuliko idadi ya mayai yanayopatikana.

Biashara ya Nyama

Na declare interest, mimi pia ni msambazaji wa nyama ya kuku wa kienyeji, hivyo naongea kwa uzoefu, na niko tayari kukosolewa. Pamoja na kufugwa katika misingi ya kijani (organic rearing), iyo pekee haitoshi kumpa thamani inayostahili huyu kuku sokoni.

Thamani ya kuku sokoni ni uzito alio nao, organic component ni jambo la ziada lililo muhimu pia. tunavyo jadili bei ya soko ya kuku huyu ni lazma tumliganishe na gharama za bidhaa pinzani zilizoko sokoni. Haitawezekana kumuuza kuku mwenye kilo moja au pungufu kwa bei ambayo tunashawishiana humu ya 15,000-20,000 wakati bidhaa pinzani (nyama nyeupe) kama samaki sato toka mwanza wanauzwakwa 7,500 kwa kilo, au kitimoto, nyama ya ngombe ambazo nazo kilo ni 7,500-8,000.

Hivyo basi, hoja yangu hapa ni uzito wa kuku husika. Ukiachana na jamii chache za kuku wa kienyeji (kuchi etc) wenye uzito mzuri, majority ya kuku pure wa asili/kienyeji kwa majogoo huwa na pungufu ya kilo moja na nusu. Kumbuka uzito wa kuku hawa sio kwasababu ya malisho duni, laah hasha, bali ni kutokana na vinasaba (genes) vyao kuwafanya kuwa na maumbo madogo madogo. kwa kuku wa aina hii, sitegemei mfugaji kama atafanikiwa kuwapeleka sokoni na kuweza kupata bei nzuri toka kwa mlaji wa mwisho.

Nini kifanyike?

Ili ufugaji uwe wenye tija kibiashara ufanyike, ni lazma wafugaji tuamke na kuachana na ufugaji wa kuku hawa asilia kwani hawana tija. Nikisema hivi simaanishi watu waache kufuga, hapana, ila wafuge aina /breeds za kuku zenye tija kibiashara. Kuku pekee unaoweza kuwafuga kwa mbinu za kienyeji na bado wakakuletea mfugaji faida nzuri kibiashara, ni kuku aina ya chotara (cross breeds). Hii ni aina ya kuku wenye sifa zote za ukienyeji kwa misingi ya mbinu zao za kuwafuga pamoja na namna walivyo nauwezo wa kuhimili mazingira hasa ya vijijini.

Kuna aina mbalimbali ya kuku hawa ikiwamo Black/ white australorps, kroiller, Rhodes island red, red hamshire, Sussex etc. Hawa ni kuku ambao wanaserve purpose zote za mayai na za nyama. Mfano kuku aina ya black/white australorps wao wanauwezo wa kutaga mpaka mayai 250 kwa mwaka, tofauti na wa kienyeji, mayai ya kuku hawa huwa makubwa na yenye kasha jeupe na kiini cha njano kama utawafuga kwenye mazingira na mbinu asilia (za kienyeji).

Ukilinganisha uwezo wa utagaji wa kuku hawa utagundua utagaji wao ni Zaidi ya asilimia 500% ukilinganisha na ule wa kienyeji pure. Idadi hii ya mayai toka kwa kuku mmoja kwa mwaka, anaweza kumwezesha mfugaji kuzalisha mayai kwa wingi na kushusha Zaidi bei ya mazao yake (mayai) kuwa chini kuweza kuliteka soko kwa urahisi Zaidi. Kumbuka, bei ya juu ya mayai ya kienyeji ni kwaajili ya kulipia gharama kubwa za utunzaji wa kuku huyu ilihali utagaji wake ni hafifu.

Pili, kuku hawa wana nyama nyingi Zaidi kuliko hawa wa kienyeji kwa majogoo hufikia mpaka uzito wa kilo 3-3.5. huku matetea hufikia kilo 2-2.5 na huwa na nyama nzuri, iliyokomaa vyema na yenye ladha. kwa uzito huu kwa majogoo, kuku hawa uuzwa kwa bei ya 20,000 - 25,000 wakiwa hai. bei ambayoni kwa mujibu wa bei ya soko kwa makadirio ya shilingi 8,000 kwa kilo kwa nyama nyeupe.

Mapungufu

Pamoja na ubora wa kuku hawa katika ufugaji wa kibiashara, kuku hawa pia wanachangamoto mbali mbali ikiwemo kutokuwa na uwezo wa kutamia. Pamoja na hii kuwa changamoto pia ni fursa kwani kwa yeye kutotamia kunamwongezea nafasi ya yeye kuendelea kutaga mara nyingi Zaidi bila kupumzika. Hivyo changamoto hii ni faida kwa mfugaji anaelenga kufuga kwa tija. Kwa vile mayai haya huwa yamerutubishwa na majogoo, nirahisi kwa mfugaji kuongeza idadi ya kuku kwa kupitia kutotolesha kwa mshine za kuangulia vifaranga au kumpa kuku mwingine ayatamie kwa niaba.


Neno la kufungia:

“ I think I touched a raw nerve when I said farming is NOT cool! I believe farming takes a lot of HARD work and dedication. Lets not lie to the youth that they'll become instant millionaires when they get into farming. It becomes "cool" once you master the trade......” caleb

Ufugaji unalipa ukiweza kuibudu biashara ya ufugaji,



Kwa ushauri Zaidi kuhusu shughuli za ufugaji, tuwasiliane kwa namba 0755815174. pia pata fursa kusoma ya Makala mbali na utaalamu kutoka kwenye mtandao wetu www.instagram.com/becky_chicks or www.facebook.com/becky_chicks

Nimejaribu kuattach picha za baadhi ya kuku bora wanaofaakufugwa kienyeji na wakaleta tija kibiashara hapa chini. Neno langu si sharia, nakaribisha Michango

View attachment 385750
View attachment 385751
View attachment 385752
View attachment 385753
View attachment 385754
Nami pia nakubaliana na michango chanya iliyomo kwenye uzi huu.
Mwanzilishi wa uzi ni mfugaji, ambaye anafuga kuku chotara.
Nakubaliana na hoja za Ginner.
Mimi nafuga Kuku wa kienyeji kwa sasa.
Huko nyuma, nimefuga Kuku wa mayai, 'layers', Kuku wa nyama, 'broilers', Kuku chotara, 'black Australop', aka Kuku wa Malawi.
Hivi sasa nafuga Kuku wa kienyeji, ambao binafsi nawaita "Shombe".
Siyo Chotara.
Kuku wangu ni 'Shombe' kwa sababu 'Mitetea' ni kuku wetu wa kawaida, wa kienyeji, lakini 'Majogoo' ninayotumia ni 'Kuku wa Kisukuma', maarufu kwa jina la 'Kuchi'.
Kwa hali hii, watoto wanaozaliwa wanakua haraka, (grows faster) ingawa napata tatizo la idadi kubwa ya 'Vilema', maana miguu yao ni mirefu sana.
Shombe hawa wanakua haraka, lakini miguu yao mirefu inashindwa kubeba uzito wao.
Baadhi, kama asilimia 5 hivi, wanakuwa vilema.
Asilimia 5 ni kubwa sana kwa Mfugaji.
Inanibidi kuongeza kiasi cha Madini na Mifupa na DCP kwenye chakula cha vifaranga ili kupunguza viwete.
Nafugia Wilaya ya Mvomero, Tarafa ya Mkindo, Kijiji cha Mkindo.
Kuhusu soko la kuku, mpaka sasa, mahitaji ya Wakaangaji wa chips na kuku katika eneo ninaloishi pamoja na maeneo jirani ni zaidi ya kuku 200 kwa wiki.
Soko lipo.
 
Nami pia nakubaliana na michango chanya iliyomo kwenye uzi huu.
Mwanzilishi wa uzi ni mfugaji, ambaye anafuga kuku chotara.
Nakubaliana na hoja za Ginner.
Mimi nafuga Kuku wa kienyeji kwa sasa.
Huko nyuma, nimefuga Kuku wa mayai, 'layers', Kuku wa nyama, 'broilers', Kuku chotara, 'black Australop', aka Kuku wa Malawi.
Hivi sasa nafuga Kuku wa kienyeji, ambao binafsi nawaita "Shombe".
Siyo Chotara.
Kuku wangu ni 'Shombe' kwa sababu 'Mitetea' ni kuku wetu wa kawaida, wa kienyeji, lakini 'Majogoo' ninayotumia ni 'Kuku wa Kisukuma', maarufu kwa jina la 'Kuchi'.
Kwa hali hii, watoto wanaozaliwa wanakua haraka, (grows faster) ingawa napata tatizo la idadi kubwa ya 'Vilema', maana miguu yao ni mirefu sana.
Shombe hawa wanakua haraka, lakini miguu yao mirefu inashindwa kubeba uzito wao.
Baadhi, kama asilimia 5 hivi, wanakuwa vilema.
Asilimia 5 ni kubwa sana kwa Mfugaji.
Inanibidi kuongeza kiasi cha Madini na Mifupa na DCP kwenye chakula cha vifaranga ili kupunguza viwete.
Nafugia Wilaya ya Mvomero, Tarafa ya Mkindo, Kijiji cha Mkindo.
Kuhusu soko la kuku, mpaka sasa, mahitaji ya Wakaangaji wa chips na kuku katika eneo ninaloishi pamoja na maeneo jirani ni zaidi ya kuku 200 kwa wiki.
Soko lipo.
Bei elekezi ya kuuza hawa chotara ni shilingi ngapi?
 
Bei elekezi ya kuuza hawa chotara ni shilingi ngapi?
Ginner atusaidie katika hili la bei elekezi ya kuku chotara.
Bei ya kuku wa kienyeji huku Kijijini ni kati ya Sh. 10,000/= na 15,000/=.
Majike yana bei ya chini huku majogoo yakiuzwa bei ya juu kidogo.
Nilienda kwa Mfugaji Dar, eneo la Goba, kutafuta mbegu ya Kuchi, nikakuta majogoo chotara aina ya 'Kroiler' yanauzwa Sh. 25,000/= kila moja.
 
Ginner atusaidie katika hili la bei elekezi ya kuku chotara.
Bei ya kuku wa kienyeji huku Kijijini ni kati ya Sh. 10,000/= na 15,000/=.
Majike yana bei ya chini huku majogoo yakiuzwa bei ya juu kidogo.
Nilienda kwa Mfugaji Dar, eneo la Goba, kutafuta mbegu ya Kuchi, nikakuta majogoo chotara aina ya 'Kroiler' yanauzwa Sh. 25,000/= kila moja.
Okay kama bei zipo ivyo, soko lake ni mahotelin tu na migahawa mikubwa labda, maana vibanda vya chips kuku wao ni hawa wa 7000/=
au nipe somo kidogo kwenye masoko kama hautojali ndugu yangu
 
98 Reactions
Reply
Back
Top Bottom