USHIROMBO GEITA: Kijana ampiga mateke baba yake mzazi

Dola Iddy Wa Chelsea

JF-Expert Member
Sep 26, 2014
2,114
1,485
Wakati nipo nyunbani hapa karibu na Makoye lodge nikiwa zangu naweka oil kwenye pikipiki yangu ghafla nikashuhudia ugomvi mkubwa maeneo ya Makoye lodge.

Nikajaribu kujisogeza ili kupata mawili matatu juu ya nini kinachoendelea aisee kijana wa miaka 20s amekamatwa na baba yake kwa madai ameiba kiasi cha laki 3 jana usiku kutoka kwa baba yake mzazi na kwenda kuchukua chumba Makoye lodge ambapo ndipo alipokamatiwa na mzazi wake.

Ila kabla hajamdhibitiwa alimshambulia baba yake mzazi kwa mateke hadharani mbele ya umati wa watu ila baada ya muda raia walimdhibiti kwa kumfunga kamba na kumpeleka kituo cha polisi Ushirombo.

Pia kipindi baba yake anampekua kijana wake mifukoni mwa suruali alimkuta na kisu cha kukunja, pochi na fedha kiasi.

Kutokana na tukio hili je laiti kama wewe ndio ungekuwa baba mzazi wa kijana huyo utachukua hatua gani dhidi ya kijana wako?
 
...kinachoendelea aisee kijana wa miaka 20s amekamatwa na baba yake kwa madai ameiba kiasi cha laki 3 jana usiku kutoka kwa baba yake mzazi na kwenda kuchukua chumba Makoye lodge ambapo ndipo alipokamatiwa na mzazi wake.

Huyo makoye naye kwanini amejenga Lodge karibu na wezi
 
Huyo kumuozesha mke tu,umri huo m'baya sana damu inachemka kama tanuri la moto wa chuma ukicheza unaweza kumwachia laana kijana,angekutwa vibanda vya pombe tungesema apelekwe chuo cha mafunzo ila kukutwa lodge imamaanisha kuwa alikuwa anasuuza damu.
 
Wakati nipo nyunbani hapa karibu na Makoye lodge nikiwa zangu naweka oil kwenye pikipiki yangu ghafla nikashuhudia ugomvi mkubwa maeneo ya Makoye lodge.

Nikajaribu kujisogeza ili kupata mawili matatu juu ya nini kinachoendelea aisee kijana wa miaka 20s amekamatwa na baba yake kwa madai ameiba kiasi cha laki 3 jana usiku kutoka kwa baba yake mzazi na kwenda kuchukua chumba Makoye lodge ambapo ndipo alipokamatiwa na mzazi wake.

Ila kabla hajamdhibitiwa alimshambulia baba yake mzazi kwa mateke hadharani mbele ya umati wa watu ila baada ya muda raia walimdhibiti kwa kumfunga kamba na kumpeleka kituo cha polisi Ushirombo.

Pia kipindi baba yake anampekua kijana wake mifukoni mwa suruali alimkuta na kisu cha kukunja, pochi na fedha kiasi.

Kutokana na tukio hili je laiti kama wewe ndio ungekuwa baba mzazi wa kijana huyo utachukua hatua gani dhidi ya kijana wako?
Kisha chukua urithi wake.kuiba kunasameheka tatizo ni teke
 
Mkuu ila kwetu kina baba sidhani kama hilo linawezekana hapo mtoto anaenda kukaa hata miaka miwili jela.
Hapana mi huwezi kumuweka ndani mwanangu miaka yote hiyo kisa laki 2 na mateke
Hapo polisi itabidi achapwe viboko na mkia Wa taa basi maisha yakaendelee
 
Huyo kumuozesha mke tu,umri huo m'baya sana damu inachemka kama tanuri la moto wa chuma ukicheza unaweza kumwachia laana kijana,angekutwa vibanda vya pombe tungesema apelekwe chuo cha mafunzo ila kukutwa lodge imamaanisha kuwa alikuwa anasuuza damu.
 
Back
Top Bottom