Faith
Member
- Jul 9, 2008
- 52
- 11
from
http://www.lukwangule.blogspot.com
ushirikina wachakaza sarafu za Tanzania
Ubora wa sarafu ya Tanzania katika mzunguko unaathiriwa na imani za kichawi ambapo nyingi ya sarafu hizo huharibika kutokana na kutumbukizwa katika mapipa ya pombe kwa lengo la kuvutia wanywaji.
Matukio ya imani za aina hiyo yapo katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.
Msimamizi wa kitengo cha fedha cha benki kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya Vicenti Mtani amesema kwamba imani hizi za kishirikina ambazo zinaharibu sarafu ya shilingi mia na shilingi hamsini pia huharibu noti za shilingi mia tano ambazo huchanwa kidogo pembeni kuzuia mtu mwingine kuchukua fedha za yule anayetoa noti hiyo asizichukue kiuchawi.
Ofisa huyo ambaye alinukuliwa mjini hapa katika banda la maonyesho la nanenane na mwandishi Rashid Mwinda wa Majira amesema kwamba imani hizo za kishirikina zinachakaza sarafu kwa kasi na kusababisha hasara katika uchumi wa nchi.
Amesema niu gharama kubwa kurejesha sarafu na noti hizo katika mzunguko kwani zinatakiwa kutengenezwa upya na kuliiingizia taifa hasara.
Afisa huyo alikuwa akielezea matumizi bora ya fedha katika maonyesho hayo ya nanenane kwa kulingana na utafiti ambao tayari benki hiyo umeufanya.
Amesema kwamba watu wanaamini kwamba madini yaliyotumika katika kutengeneza sarafu yana mvuto mkubwa kwa watumiaji pombe ikiwa na kuifanya kuwa kali na kuvutia.
Aidha inaaminika kuwa fedha hizo pia zikitumika katika chungu cha kuuzia huvutia wateja
kwa kweli hii kali!kwa dunia ya leo hii!
http://www.lukwangule.blogspot.com
ushirikina wachakaza sarafu za Tanzania
Ubora wa sarafu ya Tanzania katika mzunguko unaathiriwa na imani za kichawi ambapo nyingi ya sarafu hizo huharibika kutokana na kutumbukizwa katika mapipa ya pombe kwa lengo la kuvutia wanywaji.
Matukio ya imani za aina hiyo yapo katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.
Msimamizi wa kitengo cha fedha cha benki kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya Vicenti Mtani amesema kwamba imani hizi za kishirikina ambazo zinaharibu sarafu ya shilingi mia na shilingi hamsini pia huharibu noti za shilingi mia tano ambazo huchanwa kidogo pembeni kuzuia mtu mwingine kuchukua fedha za yule anayetoa noti hiyo asizichukue kiuchawi.
Ofisa huyo ambaye alinukuliwa mjini hapa katika banda la maonyesho la nanenane na mwandishi Rashid Mwinda wa Majira amesema kwamba imani hizo za kishirikina zinachakaza sarafu kwa kasi na kusababisha hasara katika uchumi wa nchi.
Amesema niu gharama kubwa kurejesha sarafu na noti hizo katika mzunguko kwani zinatakiwa kutengenezwa upya na kuliiingizia taifa hasara.
Afisa huyo alikuwa akielezea matumizi bora ya fedha katika maonyesho hayo ya nanenane kwa kulingana na utafiti ambao tayari benki hiyo umeufanya.
Amesema kwamba watu wanaamini kwamba madini yaliyotumika katika kutengeneza sarafu yana mvuto mkubwa kwa watumiaji pombe ikiwa na kuifanya kuwa kali na kuvutia.
Aidha inaaminika kuwa fedha hizo pia zikitumika katika chungu cha kuuzia huvutia wateja
kwa kweli hii kali!kwa dunia ya leo hii!