Ushirikiano wa China na nchi za Afrika ni wa kusaidiana na kunufaishana

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG31N1238091084.jpg


Na Caroline Nassoro

Mara nyingi kumekuwa na kauli zinazodai kuwa, China inazipa nchi za Afrika mzigo wa madeni, na hii inatokana na misaada na mikopo yenye riba nafuu inayotolewa na nchi hiyo katika miradi mbalimbali ya maendeleo ya nchi za Afrika.

Lakini tukifuatilia kwa undani zaidi, kauli hizo, ambazo zinatolewa na mataifa ya magharibi, zina lengo la kuichafua China, na pia kuharibu uhusiano mzuri kati ya China na nchi za Afrika ambao umedumu kwa miongo kadhaa sasa.

China imekuwa mwenzi muhimu wa maendeleo kwa nchi za Afrika kutokana na ushirikiano kati ya pande hizo mbili kwenye sekta mbalimbali, ikiwemo afya, ujenzi wa miundombinu, na biashara na uchumi. Mfano wa ushirikiano huo ni mradi wa ujenzi wa barabara kuu inayounganisha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta na jiji la Nairobi nchini Kenya. Huu ni mradi wa barabara kuu inayounganisha Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta na eneo la katkati mwa jiji la Nairobi nchini Kenya. Mradi huo wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 550, unatekelezwa na kampuni ya CRBC kutoka China, na tayari mradi huo umetoa ajira kwa wazawa karibu 2,000. Pamoja na kutoa ajira kwa idadi hiyo ya wazawa, mradi huo pia umewafaidisha watu wanaoishi kando ya barabara hiyo, ikiwemo wauzaji wa bidhaa za rejareja kama vile matunda, maji na hawa wauzaji wa chakula, na hivyo kuwasaidia kuinua kipato chao na kuboresha maisha yao. China pia imekuwa ni nchi inayowekeza zaidi barani Afrika katika miradi mbalimbali ya ujenzi wa miundombinu.

Katika mkutano wa Mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) uliofanyika mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka jana, rais wa China Xi Jinping katika hotuba yake alitangaza uwekezaji wa dola za kimarekani bilioni 40 barani Afrika katika Miradi Tisa, ikiwemo inayohusiana na kilimo, uchumi wa kidijitali, mabadiliko ya hali ya hewa, ukuzaji wa viwanda.

Kwa upande wa sekta ya afya, China imekuwa ikipeleka wahudumu wa afya katika nchi mbalimbali za Afrika ambao wanashirikiana na wenzao wa huko kutoa matibabu kwa wagonjwa. China pia imekuwa mstari wa mbele katika kuzisaidia nchi za Afrika kupambana na janga la COVID-19, ambapo katika mkutano wa FOCAC wa mwaka jana, rais Xi pia alitangaza kuwa China itatoa dozi bilioni moja za chanjo ya Covid-19 katika uchangiaji na utengenezaji wa pamoja.

Kwa mifano hiyo michache, tunaweza kusema kuwa, tofauti na kauli zinazotolewa na nchi za Magharibi, uhusiano na ushirikiano kati ya China na Afrika ni wa kunufaishana na kuendelea kwa pamoja.
 
China na mataifa mengine ulaya wanaihitaji Afrika kuliko Aftika inavyowahitaji wao.. Tuna malighafi ya kutosha wao hawana... Na kwenye dunia yao ya mashindano bila malighafi hawana uwezo wowote
 
Back
Top Bottom