#COVID19 Ushirikiano na Juhudi za Pamoja ndiyo Suluhu kwa Afrika kupambana na Janga la Covid-19

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,008
1,032
nmbvmbvmbvmbnv.png


Mwaka wa 2021 janga la Covid-19 linaendelea kuathiri karibu sekta zote za uchumi na jamii duniani. Watu hawawezi kujizuia kuuliza, je dunia yetu bado ni mahali salama pa kuishi?

Tangu kuripotiwa kwa virusi vya Corona barani Afrika, zaidi ya watu milioni saba wameambukizwa virusi hivyo, japokuwa idadi ya vifo vya waafrika kutokana na corona siyo kubwa sana, lakini uchumi wake umeathirika vibaya, hasa sekta ya utalii.

Kuondokana na janga la Covid-19 ni moja ya mambo muhimu katika kufufua uchumi barani Afrika, na kudungwa chanjo ya virusi vya corona ni hatua yenye ufanisi zaidi katika kuzuia maambukizi ya virusi hivyo.

Takwimu zilizotolewa kwenye tovuti ya Our World in Data zinaonyesha kuwa, hadi leo, dozi bilioni 8.31 za chanjo ya Corona zimetolewa duniani kote, 55.4% ya watu duniani wamepokea angalau dozi moja ya chanjo ya COVID-19. Lakini ni 6.3% tu ya watu katika nchi zenye mapato ya chini wamepokea angalau dozi moja.



Njia za kupambana na Covid-19 zilikuwa na athari gani barani Afrika.

Tangu kuripotiwa kwa maambukizi ya kwanza ya Covid-19 mwaka 2020 nchi nyingi zilichukua hatua za dharura ili kulinda watu wake.

Shule, masoko, mipaka na maeneo mengi ya maisha ya kila siku yalifungwa na kafyu kuwekwa kama njia ya kudhibiti mikusanyiko na maambukizi.

Matokeo yake yalikuwa ni kudorora kwa biashara haswa za sekta za huduma kama hoteli na uchukuzi, mamilioni ya watu kupoteza ajira, au mapato kupungua.

Benki ya Dunia inakadiria kuwa janga la Covid-19 litasababisha zaidi ya waafrika milioni 29 kuzama kwenye umaskini uliokithiri ifikapo mwisho wa mwaka wa 2021.

Lakini athari chanya imeanza kuoneakana wakati angalau asilimia 6 ya waafrika wakipata chanjo.

Nchi nyingi za Afrika zimeondoa kafyu na mahitaji ya karantini kwa wageni wanaotalii au wenyeji wanaorejea nyumbani.

Hali hiyo imechochea kufufuka kwa sekta ya hoteli, uchukuzi na utalii kwa jumla.

Na ili kuhimiza watu zaidi kupokea chanjo, baadhi ya serikali zimeweka sheria kwamba lazima watu wote watoe vyeti vya kuthibitisha kuwa wamechanjwa kabla ya kupata huduma.

Hali hiyo inasaidia kufufuka kwa uchumi barani Afrika, kwenye ripoti yake ya mwaka huu, Benki ya Maendeleo ya Afrika inasema uchumi wa Afrika ulishuka kwa asilimia 2.1 mwaka wa 2020 kutokana na mlipuko wa janga la Corona duniani, na pato lake kwa jumla (GDP) litaongezeka kwa asilimia 3.4 mwaka 2021.

Juhudi za Pamoja ndiyo suluhu lipasavyo

Kwenye kikao cha 55 cha Baraza la Uchumi na Jamii la Umoja wa Mataifa kilichofanyika Februari 2017, lilipitishwa kwa kauli moja azimio la “Vipimo vya kijamii vya Ushirikiano Mpya wa Maendeleo ya Afrika”, na kwenye azimio hilo liliandikwa wazo lililotolewa na rais Xi Jinping la “kujenga jumuiya ya binadamu yenye mustakabali wa pamoja”.

China imeendelea kutekeleza kwa vitendo wazo hilo la “kujenga jumuiya ya binadamu yenye mustakabali wa pamoja”, na matokeo yake yameonekana kwa jinsi China inavyosambaza chanjo ya Covid-19 kwa nchi mbalimbali duniani zinazohitaji.

Kimsingi nchi za Magharibi zimezalisha chanjo nyingi, lakini mgao wake kwa nchi maskini ni wa chini ikilinganishwa na ule unaotolewa na China ikiwa nchi moja.

Kwenye Mkutano wa 8 wa Mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC uliofanyika hivi karibuni, rais Xi Jinping wa China alitoa hotuba iitwayo “China na Afrika ziko pamoja, na zinashikana mikono kujenga jumuiya ya China na Afrika yenye mustakbali wa pamoja katika enzi mpya”.

Kwenye mkutano huo, China iliahidi kutoa dozi bilioni moja za chanjo kwa nchi za Afrika kwa ajili ya kusaidia Umoja wa Afrika kufikia lengo lake la kuchanja asilimia 60 ya watu wake ifikapo mwaka 2022, ikiwa ni pamoja na dozi milioni 600 kama mchango na dozi milioni 400 kwa njia za uzalishaji wa pamoja wa makampuni ya China na nchi husika za Afrika.
 
Back
Top Bottom