Marumeso
JF-Expert Member
- Oct 3, 2009
- 1,410
- 1,313
Suala la ushiriki wa watanzania wenzetu kwenye shindano la bigbrother lilikwisha jadiliwa bungeni na Serikali ilieleza kuwa hao washiriki wanajiwakilisha wenyewe na kuwa washiriki hao hawaiwakilishi nchi. Tatizo langu ni pale wakati wa ushiriki kwenye shindano hili wawakilishi hutambulishwa kwa utaifa wao na mara zote wanakuwa na bendera za nchi zao mikononi.
Najiuliza iwapo watu hawa hawatuwakilishi watanzania inakuwaje wanakuwa na bendera ya taifa? Bendera ya taifa kwa ufaham wangu ni moja ya alama muhimu ya utambulisho wa taifa na kamwe sio kitu cha mchezomchezo. Kama Serikali imekwisha sema hawa wenzetu hawatuwakilishi, je na hizo bendera zinafikaje mikononi mwao.
Na je hivi kwa kitu muhimu kama bendera ya taifa hivi hakuna protokali zinazoongoza matumizi yake sahihi au unaweza kuchukua bendera ya taifa na kuitumia popote pale utakavyo.
Najiuliza iwapo watu hawa hawatuwakilishi watanzania inakuwaje wanakuwa na bendera ya taifa? Bendera ya taifa kwa ufaham wangu ni moja ya alama muhimu ya utambulisho wa taifa na kamwe sio kitu cha mchezomchezo. Kama Serikali imekwisha sema hawa wenzetu hawatuwakilishi, je na hizo bendera zinafikaje mikononi mwao.
Na je hivi kwa kitu muhimu kama bendera ya taifa hivi hakuna protokali zinazoongoza matumizi yake sahihi au unaweza kuchukua bendera ya taifa na kuitumia popote pale utakavyo.