Ushiriki wa Nsa Kaisi na Watawala katika anguko la Mkoa wa Kagera

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Kuwa Profesa si kuwa Tajiri.

Uprofesa ni daraja katika taaluma.

Kuwa Profesa hakukupi nafasi HAZINA wala kukupa nafasi katika biashara. Kuna Maprofesa wa kutibu macho, kuimba, siasa, sheria, elimu,atomiki n.k. Vyote havina nafasi katika utajiri! Ni kweli wapo wengine ni matajiri wa kuweza kuwekeza huku lakini ile sheria ya UHUJUMU UCHUMI ya 1983 iliwatisha wengi ambao walikwishaanza kurudi huku kuwekeza.

Watu wengi wa Kagera (matajiri) waliwekwa rumande kwa zaidi ya mwaka. Jela ilijaa wafanya biashara hadi wengine walilazwa bwalo la Polisi Buyekera. Watu walimwaga mali zao kwenye mito na wengi wawekezaji wa miundombinu kama mabus gari ndogo walinyanganywa mali zao. Uhujumi huo uliwakamata hatawatu waliokutwa na laki, gari za mitumba na ajabu zaidi hata walioneemeka kupitia mikopo ya karadha(taasisi ya kukopesha ya serikali) wakaweza kununua malori wote gao waliwekwa mahabusi.

Yuko mmoja huko Kagoma Muleba alijijengea ghorofa yake naye aliwekwa ndani. Biashara zake ilikuwa Dar! Mkoa ulikuwa unang'ara na ghafla taa ikazimwa.

Sina la kufanya lakini sintosahau kumkumbuka Mkuu wa Mkoa wa Kagera Lt. Col. NSA KAISI 1981 -1987 kwa madhara aliyoyaleta hapa Kagera! VIJANA KAGERA haikuwa kama ilivyo sasa.

Tulikuwa tunaruka hewani! Niliwaambia kuhusu mikakati ya kuudhoofisha Mkoa kwa ujumla. Yaliyofanyika Kagera hayakufanyika mkoa mwingine wowote Tanzania. Ilikuwa kama hiyo Sheria ilitungwa kwa ajili ya kagera! Vijana mnaosema Kagera kuna fitna, si kweli! Nitajieni mkoa ambao hauna fitna! Anti-Economic Sabotage act 1983 ndiye mchawi wa Kagera.

Niwaambie kitu kimoja Tukiwa shule huko katika seminar presentation nilimbishia PhD holder darasani nikipinga kwamba sheria ya Uhujumu Uchumi ilikuwa ni sheria ya kitaifa kama nyingine. Katika presentation hiyo nikiwa ni presenter wa kundi letu wenzangu(wanafunzi) walinikana kabisa lakini mimi nilistick katika ukweli huo kwamba ile sheria ilikuwa mkakati wa Mkoa mmoja na kuroa impirical evidences. Mnajua? Presentation yetu ilipata 8/10 ! Wenzangu walinishangaa sana. Kagera hakuna fitna bali tumebanwa sana licha ya kuwa tunapakana na mataifa manne.

Eti Kagera tunafanya Magendo kuliko mikoa ya Kaskazini kusini na magharibi! Wasiofahamu:-
Makao Makuu ya Jimbo la Ziwa yalikuwa Bukoba ikiviongoza viwilaya vya Mwanza Mara shinyanga! Leo nenda Kahama Geita uangalie!!

Mifano mingine mumeiona wenyewe niwakumbushe ? "Tulipotandikwa na tetemeko la ardhi ni fitna za Kagera? Je hatukusikia lolote?

Nimechoka! Mengine Mtajaza wenyewe

Baada ya Sokoine kutembelea Mkoa Kagera na kufika Bohari ya Mkoa alitaka aonyeshwe mali nyingi iliyokamatwa Kagera wakati wa Uhujumu Uchumi. Hakukuta mali ye ye thamani iliyokuwa ikitangazwa redioni iliyofikia thamani ya mabilioni.

Hakuikuta na inasemekana alitaka maelezo ya hiyo mali na kuamuru RC wakutane Bunge Dodoma akiwa na taarifa ya mali ya uhujumu uchumi. Aliondoka na haikuwezekana kwa sababu alipatwa ajali "Dumila" na kufariki pale pale.
 
Uchumi Kagera waweza kufufuliwa

MKOA wa Kagera ulikuwa ukiitwa mkoa wa Ziwa Magharibi (West Lake). Ulipata jina la sasa mwaka 1979, baada ya vita kati ya Tanzania na Uganda.

Hivi vilikuwa vita vya kumfukuza na hatimaye kumwondoa dikteta Iddi Amin wa Uganda aliyekuwa amevamia Tanzania.

Amin alivamia na kukalia eneo la Kagera akidai kuwa mpaka halali kati ya nchi hizi mbili ulikuwa Mto Kagera; pale Kyaka.

Kwa wenyeji wa mkoa huu, neno Kagera linatokana na “Akagera,” yaani kijito kinachotiririsha maji yake katika mto mkubwa au ziwa. Mto Kagera hutiririsha maji yake katika Ziwa Viktoria.

Maji haya ya Kagera huonekana wazi kuwa hayakai ziwani bali hukatisha ziwa na kuwa chanzo cha Mto Nile ambao ni mto mrefu kuliko yote duniani.

Mkoa wa Kagera ni miongoni mwa mikoa michache iliyobahatika kupata maendeleo makubwa kiuchumi na kijamii kabla na baada ya uhuru.

Wamisionari wa madhehebu ya Kilutheri na Wakatoliki (Missionaries of Africa/White Fathers), waliingia Bukoba mwishoni mwa miaka ya 1880 na kuanzisha shule za msingi, sekondari na vyuo vya ualimu.

Moja ya vyuo hivyo ni Chuo cha Ualimu cha Kajunguti, katika wilaya ya Muleba. Chuo hicho kilikwishafungwa. Miongoni mwa shule za sekondari zilizoanzishwa na wamisionari ni St. Thomas More College (Ihungo) na Nyakato.

Wamisionari pia walifungua hospitali mbalimbali na vituo vya afya. Miongoni mwa hospitali hizo ni Rubya, Kagondo na Ndolage, zote za wilaya ya Muleba; Mugana (Misenyi), Biharamulo, Nyakahanga na Isingiro, wilayani Karagwe na Murugwanza, wilayani Ngara.

Kwa takriban miaka 500 sasa, wakazi wa mkoa wa Kagera wamekuwa wakistawisha migomba kwa ajili ya chakula (ndizi) na mibuni – kwa ajili ya biashara (kahawa).

Wakulima wa kahawa walianzisha ushirika wao chini ya Chama Kikuu cha Ushirika cha Bukoba Cooperative Union (BCU), ambacho kilianzishwa mwaka 1948.

Miongoni mwa waanzilsihi wa BCU ni mzee George Clement Kahama, ambaye alishika nyadhifa mbalimbali serikalini.

Kupitia ushirika wao, wakulima wa Kagera waliweza kusomesha watoto wao ndani na nje ya nchi. BCU iligharamia masomo ya wanafunzi hao.

Wakulima pia walianzisha umoja wa aina ya sasa ya Kuweka na Kukopa, maarufu kama “Ihanika.” Hadi miaka ya 1955, mfuko huo ulikuwa na zaidi ya Sh. 400 milioni.

Lakini uchumi wa mkoa na wananchi ulianza kuonyesha mdororo baada ya uhuru. Inaonekana kuwa nguzo kuu zake zilianza kulegea na hatimaye kung’oka.

Utawala wa asili wa kichifu ulitupiliwa mbali. Pamoja na mfumo huo kuwa wa upendeleo kwa watawala na hata kuhalalisha unyonyaji kwa njia ya miliki ya ardhi, ulikuwa na taratibu shinikizi zilizowezesha uwajibikaji kimila na hasa katika uzalishaji mashambani.

Hili lilifuatiwa na mpango wa serikali wa kuweka ushirika chini yake badala ya kuwa mikononi mwa wananchi.

Katika mazingira haya, hata mfuko wa wananchi, Ihanika, ukatoweka na serikali haikufanya juhudi kuwafidia. Hapa uchumi uliokuwa umeshamiri ukaingia misukosuko.

Kwa miaka mingi, wananchi wa Kagera walikuwa wakifanya biashara na wenzao wa Uganda. Utawala wa Amin uliondoa ushirikiano na kupunguza mwingiliano.

Kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977 kulikofuatia, kuliziba vifereji vya mahusiano ya kiuchumi yasiyorasmi vilivyokuwa vimesalia.

Vita vya Kagera (1978/79), vilipiganiwa katika ardhi ya mkoa wa Kagera. Biashara ndogo na kubwa ziliharibika. Mtindo wa maisha ulivuruguka. Wananchi wakawa wakimbizi ndani ya nchi yao. Uchumi ukaanguka zaidi na umasikini ukashamiri.

Watu wengi walifariki katika vita. Mali zao ziliharibiwa pamoja na miundombuinu – barabara, shule, hospitali na mabenki.

Rais Julius Nyerere alitoa miezi 18 kumaliza matatizo hayo na kurejesha maisha katika hali ya kawaida; lakini miezi hiyo haijaisha hadi leo.

Ndipo ikaja “Operation Uhujumu Uchumi” mwaka 1983. Zoezi hilo liliendeshwa chini ya aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Kagera, Kanali Nsa Kaisi.

Katika sakasaka na kamatakamata, watu wengi waliswekwa ndani; mali zilikamatwa, baadhi walifilisiwa kwa halali au haramu na, katika hali isiyo na maelezo, baadhi ya mali, zikiwa zimeharibika, zilirejeshwa kwa wenyewe bila hata “pole.”

Kukamatwa kwa magari (malori), kwa mfano, kulisababisha maisha magumu vijijini kwa kuwa wananchi hawakupata mahitaji.

Wakati huo, vyama vya ushirika ambavyo sasa vilikuwa vimerejeshwa chini ya mfumo wa kiserikali, vikawa vimeingiliwa na kile wanaita “mchwa.”

Watu wasiokuwa waaminifu wakajipenyeza na kuwaibia wakulima wa kahawa. Imani ya wananchi ikapungua. Ari ya kilimo ikaanza kupotea.

Hapa ushirika wa BCU/KCU uliokuwa na nguvu, ukameguka. Wananchi wa wilaya ya Karagwe wakajitenga na kuanzisha Karagwe District Cooperative Union (KDCU). Biharamulo nao wakajitenga wakaanzisha Biharamulo Cooperative Union (BCU).

Yote haya yalikuwa na athari mbaya kwa uchumi na maisha ya wananchi mkoani Kagera.

Kana kwamba hayo yalikuwa hayatoshi, ukaingia ugonjwa wa ukimwi. Mgonjwa wa kwanza wa ukimwi aligundulika mkoani Kagera mwaka 1983.

Uzito wa janga hilo unashuhudiwa kwa makaburi “mabichi” yaliyojaa mashambani. Vijana waliokuwa wakichakarika kwa kufanya biashara, wamekufa kwa kasi isiyomithilika.

Wakati mwingine waweza kutembelea nyumba moja na kukuta pikipiki tatu au nne zimeegeshwa. Ni za vijana waliokufa “kwa ukimwi” ambao walikuwa watafutaji wa neema kwa familia.

Hivyo wazalishaji wakubwa wakaangamia kwa ukimwi. Wakabaki wazee. Familia nyingi zikawa na mzigo wa kutunza yatima. Muda mwingi wa kuzalisha mali ukapotea kuuguza wagonjwa, kutunza yatima na kuhudhuria mazishi na matanga.

Ndipo likaja janga la kuzama kwa meli – mv BUKOBA, tarehe 21 Mei 1996. Inakadiriwa wengi wa abiria waliokufa katika ajali hiyo walikuwa wa mkoa wa Kagera; wengi wao wakiwa vijana watafutaji waliokuza uchumi wa mkoa.

Sasa kumezuka ugonjwa wa kunyausha migomba (Banana Xanthomonas Wilt-BXW) na ugonjwa wa kahawa (Coffee Fusarium Wilt-CFW).

Kama hakuna kahawa na hakuna migomba (ndizi), siyo tu uchumi bali maisha ya wananchi yako hatarini. Hakujawa na mbadala wa maana.

Nani ataisemea Kagera? Kuna matatizo mengi lakini mengine yaweza kuwekwa kwenye ngazi ya changamoto.

Je, tukianza na kongamano kubwa la wanaoitakia mema Kagera, hatuwezi kutotoa njia za kuinua uchumi na maisha ya wananchi mkoani?

Mkoa una hali ya joto la wastani la sentigredi 26.02. Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800 hadi 1,200 kwa mwaka – kati ya Septemba na Januari na kati ya Machi na Mei.

Inawezekana.

Meddy Mulisa

0754 079 577
 
"eti" mradi wa ujenzi wa kituo cha mabasi Msamvu - Morogoro ulikuwa ujengwe Bukoba mkafanyiana fitina wenyewe kwa wenyewe hadi ukahamishiwa huko kwa wenye kujua fursa! Nasikia pia kandarasi za ujenzi wa miundombinu ya mji wa Bukoba mnapeana kwa dili...
 
Wana JF,

Wanasema ya kale hayanuki lakini uwezi kupita siku ukakumbuka kukwama kwako. Pengine unaweza kujilaumu au kulaumu yule aliyesababisha kukwama kwako, kukwama kunaweza kuletwa na mzazi, rafiki, jirani hata utawala uliopo. Mwaka 1984, kagera ndiyo iliasilika sana na kesi za uhujumu uchumi, mali za watu wengi ziliteketezw, matajiri, walinyanganywa magari, maduka , hata mashamba, magari yalipelekwa kuwa Kagera Retco, Maduka yaka wa RTC, bidhaa nyingi zilitupwa mtoni ili kuepuka kukamatwa, pesa ilibadilishwa ghafla ili wenye nazo ziteketee.

mkoa wa kagera ndio ulilengwa makusudi na alipelekwa huyu NSA KAISi kuharibu uchumi wa Mkoa huu ambao ulikuwe umesheeni mali na viwanda. Kiini kikubwa hakijulikani, pengine wanasema ni makusudi ya kudhoofisha mkoa huuwa akina mshomile kwa kuwa walihusika sana katika kutaka kupindua nchi. watu wengi walikimbilia Uganda, naRwanda, wengine hawajarudi kabisa. Matajiri wengi walifilisiwa na kuutwa na kesi, wengine walifungwa kwa muda fulani.

Hakika kilikuwa ni kilio cha kusaga meno, mkoa huu tangia uumizwe hakuna ambaye huwa anapenda kuiinvest, mkoa huu ulikuwa na wahindi wengi na waarabu, sasa hivi wamebaki wenyeji tuu. miji iliyokuwa inakua kwa kasi ni Kamachumu, Mshamba, Katoro na Muleba mjini.

marehemu huwa hatupendi kuwasema lakini Mbona hiltla bado anakumbukwa kwa mabaya, hata osama vile vile
 
Wana JF,

Wanasema ya kale hayanuki lakini uwezi kupita siku ukakumbuka kukwama kwako. Pengine unaweza kujilaumu au kulaumu yule aliyesababisha kukwama kwako, kukwama kunaweza kuletwa na mzazi, rafiki, jirani hata utawala uliopo. Mwaka 1984, kagera ndiyo iliasilika sana na kesi za uhujumu uchumi, mali za watu wengi ziliteketezw, matajiri, walinyanganywa magari, maduka , hata mashamba, magari yalipelekwa kuwa Kagera Retco, Maduka yaka wa RTC, bidhaa nyingi zilitupwa mtoni ili kuepuka kukamatwa, pesa ilibadilishwa ghafla ili wenye nazo ziteketee.

mkoa wa kagera ndio ulilengwa makusudi na alipelekwa huyu NSA KAISi kuharibu uchumi wa Mkoa huu ambao ulikuwe umesheeni mali na viwanda. Kiini kikubwa hakijulikani, pengine wanasema ni makusudi ya kudhoofisha mkoa huuwa akina mshomile kwa kuwa walihusika sana katika kutaka kupindua nchi. watu wengi walikimbilia Uganda, naRwanda, wengine hawajarudi kabisa. Matajiri wengi walifilisiwa na kuutwa na kesi, wengine walifungwa kwa muda fulani.

Hakika kilikuwa ni kilio cha kusaga meno, mkoa huu tangia uumizwe hakuna ambaye huwa anapenda kuiinvest, mkoa huu ulikuwa na wahindi wengi na waarabu, sasa hivi wamebaki wenyeji tuu. miji iliyokuwa inakua kwa kasi ni Kamachumu, Mshamba, Katoro na Muleba mjini.

marehemu huwa hatupendi kuwasema lakini Mbona hiltla bado anakumbukwa kwa mabaya, hata osama vile vile


Mkuu mgt software hongera kwa bandiko lako. Kama Mh. Nsa Kaisi alipelekwa Kagera 1984 kama unavyodai, basi mchango wake katika vita ya wahujumu uchumi huko Kagera hauwezi kuwa mkubwa kama unavyotaka tuamini. Kama utakumbuka vizuri watu kama akina Edward Barongo walikuwa wameshatiwa ndani kabla ya mwaka tajwa hapo juu. Zaidi ya hapo mkuu mgt software ni vyema ukakumbuka kwamba, katika mwaka 1984 vita dhidi ya wahujumu Uchumi ilidumu kwa kipindi kisichozidi miezi minne (January- April 1984) hadi pale kiongozi wa hiyo vita Mh. Edward Sokoine alipokufa katika ile ajali yenye utata mkubwa tarehe 12/04/1984. Kama utakumbuka vizuri, kifo cha Mh. Edward Sokoine kilitamatisha vita dhidi ya wahujumu uchumi (Hii Vita ilikufa Natural Death)

Ahsante
 
Mpola mkodomi
Kuwa Profesa si kuwa Tajiri.

Uprofesa ni daraja katika taaluma.

Kuwa Profesa hakukupi nafasi HAZINA wala kukupa nafasi katika biashara. Kuna Maprofesa wa kutibu macho, kuimba, siasa, sheria, elimu,atomiki n.k. Vyote havina nafasi katika utajiri! Ni kweli wapo wengine ni matajiri wa kuweza kuwekeza huku lakini ile sheria ya UHUJUMU UCHUMI ya 1983 iliwatisha wengi ambao walikwishaanza kurudi huku kuwekeza.

Watu wengi wa Kagera (matajiri) waliwekwa rumande kwa zaidi ya mwaka. Jela ilijaa wafanya biashara hadi wengine walilazwa bwalo la Polisi Buyekera. Watu walimwaga mali zao kwenye mito na wengi wawekezaji wa miundombinu kama mabus gari ndogo walinyanganywa mali zao. Uhujumi huo uliwakamata hatawatu waliokutwa na laki, gari za mitumba na ajabu zaidi hata walioneemeka kupitia mikopo ya karadha(taasisi ya kukopesha ya serikali) wakaweza kununua malori wote gao waliwekwa mahabusi.

Yuko mmoja huko Kagoma Muleba alijijengea ghorofa yake naye aliwekwa ndani. Biashara zake ilikuwa Dar! Mkoa ulikuwa unang'ara na ghafla taa ikazimwa.

Sina la kufanya lakini sintosahau kumkumbuka Mkuu wa Mkoa wa Kagera Lt. Col. NSA KAISI 1981 -1987 kwa madhara aliyoyaleta hapa Kagera! VIJANA KAGERA haikuwa kama ilivyo sasa.

Tulikuwa tunaruka hewani! Niliwaambia kuhusu mikakati ya kuudhoofisha Mkoa kwa ujumla. Yaliyofanyika Kagera hayakufanyika mkoa mwingine wowote Tanzania. Ilikuwa kama hiyo Sheria ilitungwa kwa ajili ya kagera! Vijana mnaosema Kagera kuna fitna, si kweli! Nitajieni mkoa ambao hauna fitna! Anti-Economic Sabotage act 1983 ndiye mchawi wa Kagera.

Niwaambie kitu kimoja Tukiwa shule huko katika seminar presentation nilimbishia PhD holder darasani nikipinga kwamba sheria ya Uhujumu Uchumi ilikuwa ni sheria ya kitaifa kama nyingine. Katika presentation hiyo nikiwa ni presenter wa kundi letu wenzangu(wanafunzi) walinikana kabisa lakini mimi nilistick katika ukweli huo kwamba ile sheria ilikuwa mkakati wa Mkoa mmoja na kuroa impirical evidences. Mnajua? Presentation yetu ilipata 8/10 ! Wenzangu walinishangaa sana. Kagera hakuna fitna bali tumebanwa sana licha ya kuwa tunapakana na mataifa manne.

Eti Kagera tunafanya Magendo kuliko mikoa ya Kaskazini kusini na magharibi! Wasiofahamu:-
Makao Makuu ya Jimbo la Ziwa yalikuwa Bukoba ikiviongoza viwilaya vya Mwanza Mara shinyanga! Leo nenda Kahama Geita uangalie!!

Mifano mingine mumeiona wenyewe niwakumbushe ? "Tulipotandikwa na tetemeko la ardhi ni fitna za Kagera? Je hatukusikia lolote?

Nimechoka! Mengine Mtajaza wenyewe

Baada ya Sokoine kutembelea Mkoa Kagera na kufika Bohari ya Mkoa alitaka aonyeshwe mali nyingi iliyokamatwa Kagera wakati wa Uhujumu Uchumi. Hakukuta mali ye ye thamani iliyokuwa ikitangazwa redioni iliyofikia thamani ya mabilioni.

Hakuikuta na inasemekana alitaka maelezo ya hiyo mali na kuamuru RC wakutane Bunge Dodoma akiwa na taarifa ya mali ya uhujumu uchumi. Aliondoka na haikuwezekana kwa sababu alipatwa ajali "Dumila" na kufariki pale pale.
 
Mwandishi atuambie Kagara ilikuwa na viwanda vingapi, biashara kubwa ngapi za exports kwa nchi 4 ilizopakana nazo, hotels ngapi za utalii...
Baada ya ujio wa RC Nsa Kaisi Kagera akadidimia kwa kupoteza viwanda vingapi
Biashara ngapi zikafa,
Kazi kiasi gani zikapotea,
Ndege za watalii kiasi gani zikakoma hivyo kuathiri uchumi wa Kagera.

Kahawa kiasi gani ilikuwa exported overseas, ujio wa RC Nsa Kaisi akaharibu.

Mkiwa objective hivi, itawasaidia wasomaji na wanakagera ili next time wajue wako wapi, walitoka wapi na wanaelekea wapi.

Na kama ni kweli makao makuu ya Kanda ya ziwa yalikuwa Kagera, ilikuwaje yakaenda Mwanza. Nsa Kaisi alifaidika vip kuyapeleka Mwanza?
Kwanini hakupeleka Shinyanga au Mara (Musoma) kwao na Mwl. Nyerere??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watazuiwa na serikali hii ya jiwe. Kama rambirambi tu ziliporwa itakuwa hivyo vingine?
Serikali ya Jiwe ndio nini?
Rambirambi walipewa waliondokewa na wapendwa wao.
Hata kama wangelipewa zingelikuwa zimekwisha,kwa sasa wanatengenezewa meli kubwa.
 
Kuwa Profesa si kuwa Tajiri.

Uprofesa ni daraja katika taaluma.

Kuwa Profesa hakukupi nafasi HAZINA wala kukupa nafasi katika biashara. Kuna Maprofesa wa kutibu macho, kuimba, siasa, sheria, elimu,atomiki n.k. Vyote havina nafasi katika utajiri! Ni kweli wapo wengine ni matajiri wa kuweza kuwekeza huku lakini ile sheria ya UHUJUMU UCHUMI ya 1983 iliwatisha wengi ambao walikwishaanza kurudi huku kuwekeza.

Watu wengi wa Kagera (matajiri) waliwekwa rumande kwa zaidi ya mwaka. Jela ilijaa wafanya biashara hadi wengine walilazwa bwalo la Polisi Buyekera. Watu walimwaga mali zao kwenye mito na wengi wawekezaji wa miundombinu kama mabus gari ndogo walinyanganywa mali zao. Uhujumi huo uliwakamata hatawatu waliokutwa na laki, gari za mitumba na ajabu zaidi hata walioneemeka kupitia mikopo ya karadha(taasisi ya kukopesha ya serikali) wakaweza kununua malori wote gao waliwekwa mahabusi.

Yuko mmoja huko Kagoma Muleba alijijengea ghorofa yake naye aliwekwa ndani. Biashara zake ilikuwa Dar! Mkoa ulikuwa unang'ara na ghafla taa ikazimwa.

Sina la kufanya lakini sintosahau kumkumbuka Mkuu wa Mkoa wa Kagera Lt. Col. NSA KAISI 1981 -1987 kwa madhara aliyoyaleta hapa Kagera! VIJANA KAGERA haikuwa kama ilivyo sasa.

Tulikuwa tunaruka hewani! Niliwaambia kuhusu mikakati ya kuudhoofisha Mkoa kwa ujumla. Yaliyofanyika Kagera hayakufanyika mkoa mwingine wowote Tanzania. Ilikuwa kama hiyo Sheria ilitungwa kwa ajili ya kagera! Vijana mnaosema Kagera kuna fitna, si kweli! Nitajieni mkoa ambao hauna fitna! Anti-Economic Sabotage act 1983 ndiye mchawi wa Kagera.

Niwaambie kitu kimoja Tukiwa shule huko katika seminar presentation nilimbishia PhD holder darasani nikipinga kwamba sheria ya Uhujumu Uchumi ilikuwa ni sheria ya kitaifa kama nyingine. Katika presentation hiyo nikiwa ni presenter wa kundi letu wenzangu(wanafunzi) walinikana kabisa lakini mimi nilistick katika ukweli huo kwamba ile sheria ilikuwa mkakati wa Mkoa mmoja na kuroa impirical evidences. Mnajua? Presentation yetu ilipata 8/10 ! Wenzangu walinishangaa sana. Kagera hakuna fitna bali tumebanwa sana licha ya kuwa tunapakana na mataifa manne.

Eti Kagera tunafanya Magendo kuliko mikoa ya Kaskazini kusini na magharibi! Wasiofahamu:-
Makao Makuu ya Jimbo la Ziwa yalikuwa Bukoba ikiviongoza viwilaya vya Mwanza Mara shinyanga! Leo nenda Kahama Geita uangalie!!

Mifano mingine mumeiona wenyewe niwakumbushe ? "Tulipotandikwa na tetemeko la ardhi ni fitna za Kagera? Je hatukusikia lolote?

Nimechoka! Mengine Mtajaza wenyewe

Baada ya Sokoine kutembelea Mkoa Kagera na kufika Bohari ya Mkoa alitaka aonyeshwe mali nyingi iliyokamatwa Kagera wakati wa Uhujumu Uchumi. Hakukuta mali ye ye thamani iliyokuwa ikitangazwa redioni iliyofikia thamani ya mabilioni.

Hakuikuta na inasemekana alitaka maelezo ya hiyo mali na kuamuru RC wakutane Bunge Dodoma akiwa na taarifa ya mali ya uhujumu uchumi. Aliondoka na haikuwezekana kwa sababu alipatwa ajali "Dumila" na kufariki pale pale.
Kagera sasa inatakiwa kuangalia mbele maana Dunia inaenda kwa kasi, waliofanya hayo kama walioyafanya kwa nia ovu hayataweza kuzuia mafanikio ya mkoa siku za mbeleni, maana mbeleni Kuna mwanga na matumaini. Sehemu nyingi za nchi yetu bado ni masikini hivyo wala Kagera isijiangaishe na kuomba kulipwa fidia kuhusu yaliyotokea nyuma. Wafundisheni Watoto kufanyakazi kwa bidii na maarifa, wasomesheni na kuhakikisha wanapata ujuzi. Kagera wekezeni kwenye viwanda kama anavyosema Rais wetu ili tuweze kuingia katika mapambano ya Dunia hii. Tena wekezeni katika viwanda vya Kuzaliwa vipuri, ili Kagera kiwe kituo cha Kuzaliwa vipuri kwa viwanda vyetu na viwanda vya Afrika, huo ndiyo utakuwa mkombozi wetu sasa wala tusirudie tena kuangalia ya nyuma, Tanzania kila eneo linahitaji msaada.
Hapa ni lazima nishauri kwamba wala tusiangaike kununua machine Mpya, tununue machine zilizotumika tuwatafuta wachina wawafundishe Watoto wetu namna ya kutumia CNC machine center na six axis CNC ili mkoa uweze kutoa wataalam wanaotakiwa katika viwanda vya ndani na nje ya Nchi, na kuzalisha vipuri vinavyotakiwa ndani na nje ya nchi. Hivyo ndiyo walioyafanya wachina na wakorea, na ndiyo anajaribu kufanya Rwanda. Bado hatujachelewa, tuchukue hatua, wala hatuhitaji kulalamika katika Dunia ya sasa hakuna atakayetuonea huruma na wala tuache visingizio kwamba Serikali inatatuzuia, Serikali kuzuia muda huo umepita, awamu ya tano imetufungulia njia, tukishindwa tujilaumu wenyewe
 
Kuna ukweli ndani yake huu mkoa na jinsi nilivyokuwa nawafahamu raia wa huko haukupaswa kuwa kama ulivyo leo. Hujuma dhidi ya mkoa wa Kagera bado zinaendelea mpaka sasa japo mengi yanabaki kuwa siri za ki mfumo..nawashauri wana Kagera hawajachelewa wanaweza kuusimamisha upya na uka ng'aa kama ilivyokuwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali ya Jiwe ndio nini?
Rambirambi walipewa waliondokewa na wapendwa wao.
Hata kama wangelipewa zingelikuwa zimekwisha,kwa sasa wanatengenezewa meli kubwa.

Comments nyingine defies logic, eti "kutengenezewa MELI Kubwa" kwani meli itakuwa inasafirisha wenyeji wa Kagera tu? Kitu kingine kwani Meli hiyo mpya inatofauti gani kubwa katika capacity ya kubeba abiria ni mizigo ukilinganisha na meli ya Victoria iliyo jengwa na wakoloni wa Uingereza in late 1950s na kunganiswa Mwanza in 1960s - tofauti ya meli mpya na Victoria ni ndogo sana.

Wana Kagera si wajinga, abaguzi wa wazi wazi wa kutaka kudumaza Mkoa wa Kagera kimaendeleo hupo wazi kabisa - mwenye macho ambiwi tazama. Watueleze hivi inakuwaje Mkoa ambao unashika nafasi ya pili Tanzania kwa kuwa na idadi kubwa wakazi zaidi ya Million plus ikiwa nyuma ya Mkoa wa Mwanza kwa idadi ya watu - mtu ungetegemea pawepo walao Hospitali ya rufaa hilo wala alijawahi kupewa kipa umbele wanacho fanya ni ku face rift hospitali iliyo achwa na Mjerumani na inabaki hospitali ya kawaida tu and they are least concern wako mbioni ku fast track ujenzi wa Modern Hospitals kwenye Mikoa na Wilaya nyingine, kujenga vituo vya mabasi vya kisasa, ujenzi wa Masoko wakati Bukoba inabaki inatumia majengo ya zamani yaliyo achwa na wakoloni, hali inasikitisha sana, just imagine barabara za lami ndani ya manispaa ya Bukoba zilikwanguliwa na kubaki vumbi na changarawe - Mkuu wa Mkoa, RPC, RAS na viongozi wengine wa Mkoa wanapita kwa magari barabara hizo kila siku lakini hakuna aliye wahi ku-address aibu hii, je, mkoa huwa haupewi mgao wa fedha wa kuendeleza manispaa, iweje miji na Wilaya za zipewe kipa umbele lakini si Mkoa wa Kagera, nenda Kahama, Katavi, Singida,Geita(Chato),Ifakara na Wilaya za Kusini hakuna inayo fanana inayo fanana na manispaa ya Bukoba ambayo inafanana na mahame.

Bottom line is: Tanzania ni Taifa moja, maendeleo miji na Mikoa yote Tanzania ipewe haki sawa bila ya upendeleo uliyo wazi wazi, muangalie vile vile na idadi ya wakazi kila Mkoa hasa linapokuja suala la Ujenzi wa Hospitali na mashule na vyuo vya ufundi pamoja na ujenzi wa viwanda, sio kurundika viwanda ukanda wa Pwani tu, tujaribu kuwaiga wenzetu Wachina linapo kuja suala la ujenzi wa viwanda - vina jengwa kwenye economic zones ambazo zipo mipakani hawajali kama Mikoa unakaliwa na kabila la Ki Han au Wa Haigur!
 
Back
Top Bottom