lunyelunye
Member
- Apr 2, 2012
- 19
- 4
Kwa muda mrefu tumekuwa tukisikia kutoka kwa viongozi hasa wenye kuogopa wimbi la weledi wa vijana katika siasa mpya zinazotegemea facts na akili za kichambuzi zaidi kuliko propaganda mfu, wamekuwa wakijaribu kuonyesha kutuaminisha kwamba vijana wakiwa vyuoni kushiriki kwao katika mijadala ya uchambuzi na hata kujiunga na harakati mbalimbali za kupigania haki za wenzao katika maisha yao wakiwa chuoni, inaonekana kama vile ni uasi na vurugu.
Watu wenye mtazamo huo wangetamani au wanadhani hata katika ngazi hiyo ya elimu ya juu, na tena hata kwa mtu anaesoma masomo yanayohusu siasa na uongozi anapaswa kuishi maisha ya pembe tatu yaani darasani,kula na kulala kama vile wanasoma elimu ya msingi.
HOJA YANGU: Nyota njema huonekana asubuhi, wanasiasa maarufu, na hata viongozi wazuri tunaowajua wameanza kuonekana wakiwa vyuoni katika ushiriki wao wa siasa za wanafunzi. mfano JK nyerere akiwa makerere, kikwete,mseveni na warioba katika siasa za DUSO wakiwa UDSM. Pia kuna vijana kama kina ZITO, silinde, Nasari, Mwita Waitara na wengine wengi ambao wamelelewa na siasa za wanafunzi na kupata moyo wa harakati na uongozi na kazi zao tumeziona.
My Take:Fikra tete na moyo wa udadavuzi wa hoja na tafakuri jadidi unaanza kujengwa sheleni, tuwaache vijana wajifunze changamoto za uongozi wakiwa chuoni na washamiri na kupata hamu ya kuongoza taifa lao. Wazee tusiogope changamoto na nguvu za hoja za vijana bali tuwape nafasi na ushauri ili wakue katika busara na hekima. Ushindi Wa Nasari kama ulivo wa vijana wengine kama Zito,Silinde, January, Mnyika n.k uwafumbue macho muone umuhimu wa vijana ku-practice siasa zao za kiuanafunzi wakiwa shule maana ndizo huleta akisi picha ya baadae katika siasa za nchi yetu. NAOMBA KUTOA HOJA
Watu wenye mtazamo huo wangetamani au wanadhani hata katika ngazi hiyo ya elimu ya juu, na tena hata kwa mtu anaesoma masomo yanayohusu siasa na uongozi anapaswa kuishi maisha ya pembe tatu yaani darasani,kula na kulala kama vile wanasoma elimu ya msingi.
HOJA YANGU: Nyota njema huonekana asubuhi, wanasiasa maarufu, na hata viongozi wazuri tunaowajua wameanza kuonekana wakiwa vyuoni katika ushiriki wao wa siasa za wanafunzi. mfano JK nyerere akiwa makerere, kikwete,mseveni na warioba katika siasa za DUSO wakiwa UDSM. Pia kuna vijana kama kina ZITO, silinde, Nasari, Mwita Waitara na wengine wengi ambao wamelelewa na siasa za wanafunzi na kupata moyo wa harakati na uongozi na kazi zao tumeziona.
My Take:Fikra tete na moyo wa udadavuzi wa hoja na tafakuri jadidi unaanza kujengwa sheleni, tuwaache vijana wajifunze changamoto za uongozi wakiwa chuoni na washamiri na kupata hamu ya kuongoza taifa lao. Wazee tusiogope changamoto na nguvu za hoja za vijana bali tuwape nafasi na ushauri ili wakue katika busara na hekima. Ushindi Wa Nasari kama ulivo wa vijana wengine kama Zito,Silinde, January, Mnyika n.k uwafumbue macho muone umuhimu wa vijana ku-practice siasa zao za kiuanafunzi wakiwa shule maana ndizo huleta akisi picha ya baadae katika siasa za nchi yetu. NAOMBA KUTOA HOJA