Itovanilo
JF-Expert Member
- Jul 30, 2018
- 2,314
- 5,138
Habari za asubuhi wapendwa, Ni asubuhi ya jumapili hii najiandaa kwenda church, ila nikaona niwaache na hii
Nakumbuka miaka fulani nikiwa darasa la tano katika shule moja huko mkoani,aliingia mwl wa darasa kwaajili ya kuendesha zoezi la kumpata Monitor na monitress,
Hivyo yakapendekezwa majina mawili mawili kwa mvulana na msichana halafu kura zinapigwa, but kwa upande wa wasichana mshindi alipata asilimia karibu Zote za kura, kwa upande wetu mwenzangu alipata asilimia 93, Mimi nilipata aslimia 4 ya kura.
Nadhani 3 ziliharibika kutokana na baadhi ya wahuni ambao hawakosekani chini ya jua. Kilichonisukuma niandike haya Ni mwalimu kugeuza kibao na kunipendelea Mimi kwa kigezo yule hakuwa na uwezo kuanzia taaluma, nidhamu, usafi wa mavazi pia alikuwa mpiga kelele mzuri darasani hivyo hawezi kuongoza
Kiutoto mchizi hakumaindi Wala Nini licha ya zomeazomea ya hapa na pale tukiwa class, hivyo Mimi nikawa Monitor wao, kwa vigezo ambavyo teacher alivielezea.
Cha ajabu, nilijikuta naumia Sana, yaani nilijikuta mwenye hatia, takribani week nzima sikuwa na amani kwa kupewa nafasi ambayo najua wazi sistahili, siyo siwezi kuongoza bali najua darasa liliamua kumpa kura mtu flani na siyo Mimi jamani.
Kila nikikumbuka huwa nacheka tu,nawaza wenzetu wanasiasa wanawezaje kuishi na vyeo ambavyo wanajua wazi walipora watu?
Dhuluma ni dhambi, inanyong'onyesha sijui wengine wanawezaje. ni njaa? Ni kutafuta heshima? au Ni nini, kama Ni njaa wengine hawana, Kama ni heshima wengine wanayotoka enzi na enzi?
Je unajisikiaje kuwaongoza watu ambao hawana imani na wewe? kwasababu hawakuamini ndiyo maana hawajakuchagua wewe.
Asubuhi njema JamiiForums.
Nakumbuka miaka fulani nikiwa darasa la tano katika shule moja huko mkoani,aliingia mwl wa darasa kwaajili ya kuendesha zoezi la kumpata Monitor na monitress,
Hivyo yakapendekezwa majina mawili mawili kwa mvulana na msichana halafu kura zinapigwa, but kwa upande wa wasichana mshindi alipata asilimia karibu Zote za kura, kwa upande wetu mwenzangu alipata asilimia 93, Mimi nilipata aslimia 4 ya kura.
Nadhani 3 ziliharibika kutokana na baadhi ya wahuni ambao hawakosekani chini ya jua. Kilichonisukuma niandike haya Ni mwalimu kugeuza kibao na kunipendelea Mimi kwa kigezo yule hakuwa na uwezo kuanzia taaluma, nidhamu, usafi wa mavazi pia alikuwa mpiga kelele mzuri darasani hivyo hawezi kuongoza
Kiutoto mchizi hakumaindi Wala Nini licha ya zomeazomea ya hapa na pale tukiwa class, hivyo Mimi nikawa Monitor wao, kwa vigezo ambavyo teacher alivielezea.
Cha ajabu, nilijikuta naumia Sana, yaani nilijikuta mwenye hatia, takribani week nzima sikuwa na amani kwa kupewa nafasi ambayo najua wazi sistahili, siyo siwezi kuongoza bali najua darasa liliamua kumpa kura mtu flani na siyo Mimi jamani.
Kila nikikumbuka huwa nacheka tu,nawaza wenzetu wanasiasa wanawezaje kuishi na vyeo ambavyo wanajua wazi walipora watu?
Dhuluma ni dhambi, inanyong'onyesha sijui wengine wanawezaje. ni njaa? Ni kutafuta heshima? au Ni nini, kama Ni njaa wengine hawana, Kama ni heshima wengine wanayotoka enzi na enzi?
Je unajisikiaje kuwaongoza watu ambao hawana imani na wewe? kwasababu hawakuamini ndiyo maana hawajakuchagua wewe.
Asubuhi njema JamiiForums.