Developer IOS
JF-Expert Member
- Jun 20, 2017
- 1,457
- 1,409
Katika kipindi hichi cha uchaguzi nimeamua kupiga kambi katika jimbo la kinondoni mitaa ya kijitonyama ili kuangalia hali ya kisiasa inaendaje kwa lengo la kujifunza kupitia kampeni za wagombea wote na mawazo ya wananchi.Kikubwa nilichogundua ni jinsi gani wananchi wanavyofurahia na kukubali utendaji mkubwa wa serikali ya awamu ya tano.
Utendaji uliotukuka wa serikali pendwa ya awamu ya tano ni kielelezo tosha cha ushindi mkubwa wa kishindo utakaopatikana katika majimbo mawili.Katika pita pita zangu na kubadilishana mawazo na watu nimegundua njia nyeupe kwa mtulia kwenda kuwatumikia tena wanakinondoni.Wanakinondoni wanamkubali sana huyu jamaa kwa utendaji wake wa kazi .
Kwetu sisi ushindi ni lazima