brave one
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 4,876
- 7,366
Hizi ni kauli za wanachama wa simba kabla ya mechi ya mtani jembe na Yanga.
''mara baada ya mechi na yanga tukishinda au tukifungwa tutaenda nyumbani kwa Rage atuonyeshe fedha za Okwi ziko wap na hatuondoki mpaka ajiuzulu'' mwingine akasema'' tunataka tujue pia pesa za mauzo ya samata, ochan na kazimoto zimetumika vipi maana ziliingia kwenye account ya mwanamke fulani'' n wengine wakathubutu kwenda hadi Bungeni kwa Mh. Spika. Lakini pia bado kukawa na mvutano kati ya mwenyekiti na kamati ya utendaji.
Lakini baada ya mechi ya mtani jembe na Simba kushinda goli 3 kwa 1 , matatizo yote ya wanasimba yamefutika na yale yote waliodhamilia yamepatiwa ufumbuzi hali sasa ni shwari kabisa gogolo hakuna tena, kweli simba na yanga ni zaidi uzijuavyo, mafanikio makubwa kabisa katika timu hizi ni mmoja kumfunga mwenzake hata kama mechi isiyo ya kimashindano.
Mpira wa Tanzania kukua itabaki kuwa ndoto isiyotimia kama Simba kumfunga Yanga au Yanga kumfunga Simba ni zaidi ya kuwa na matumizi bora ya fedha, uadilifu, kuwa na viwanja bora vya timu na timu kujitegemea.
Maana 3 kwa 1 imelipa fedha za okwi, Rage amegeuka kuwa kiongozi bora, mpira pesa na Rage wanakula sahani na wote wameshiba na kuridhika.
Simba na Yanga zinaingia katika maajabu ya Dunia na sasa tuna maajabu 8 ya dunia.
''mara baada ya mechi na yanga tukishinda au tukifungwa tutaenda nyumbani kwa Rage atuonyeshe fedha za Okwi ziko wap na hatuondoki mpaka ajiuzulu'' mwingine akasema'' tunataka tujue pia pesa za mauzo ya samata, ochan na kazimoto zimetumika vipi maana ziliingia kwenye account ya mwanamke fulani'' n wengine wakathubutu kwenda hadi Bungeni kwa Mh. Spika. Lakini pia bado kukawa na mvutano kati ya mwenyekiti na kamati ya utendaji.
Lakini baada ya mechi ya mtani jembe na Simba kushinda goli 3 kwa 1 , matatizo yote ya wanasimba yamefutika na yale yote waliodhamilia yamepatiwa ufumbuzi hali sasa ni shwari kabisa gogolo hakuna tena, kweli simba na yanga ni zaidi uzijuavyo, mafanikio makubwa kabisa katika timu hizi ni mmoja kumfunga mwenzake hata kama mechi isiyo ya kimashindano.
Mpira wa Tanzania kukua itabaki kuwa ndoto isiyotimia kama Simba kumfunga Yanga au Yanga kumfunga Simba ni zaidi ya kuwa na matumizi bora ya fedha, uadilifu, kuwa na viwanja bora vya timu na timu kujitegemea.
Maana 3 kwa 1 imelipa fedha za okwi, Rage amegeuka kuwa kiongozi bora, mpira pesa na Rage wanakula sahani na wote wameshiba na kuridhika.
Simba na Yanga zinaingia katika maajabu ya Dunia na sasa tuna maajabu 8 ya dunia.