Ushindani kampuni za simu

MNDEE

JF-Expert Member
Jul 10, 2009
491
68
Jamani nalileta hili la kampuni za simu jamvini. Kwa mtazamo wangu rate bado ziko juu sana na hakuna unafuu wa huduma mteja anapata. Hizi kampuni ziko za kutosha na wateja ni wengi cha kushangaza hakuna ushindani kati ya hizi kampuni ambao ungepelekea kuwepo kwa rate nzuri na huduma bora.

Kinachonishangaza ni kuwa kila kampuni inayochipuka haiji na jipya, zaidi ya kuangalia wengine wanafanya nini na wao wanafanya kile kile zaidi tu watarekebisha rate kwa kiasi kidogo sana. Hata hii pre-paid wanaweza kuiboresha kwa kubundle vitu kama free nights na weekends, family plans baba na mama kuongea bure, au wateja wa kampuni moja kupata mawasilino kama sio bure basi kwa rate nafuu zaidi. Hizi ni baadhi tu ya huduma zinazotolewa na kampuni za simu nchi nyingine ambazo kampuni zetu nazo zinaweza kutoa kama zitamjali mteja na si tu kujali faida.
 
Last edited:
TTCL ndio waliosabbisha haya yote they had everthing to compete with these guys.

Kumbuka tutazidi kuonewa kutokana na lifestyle yetu, mabepari hawana huruma , they finds opportunity and they use it!

Tuna culture ya kufanya chochote, serikali inaangalia kodi thats all.

I once worked with Vodacom , wao wanasema YES, THE RATE IS HIGH BUT AFFORDABLE!

kuna haja ya kufanya kitu sisi wenyewe raia, serikali hamna kitu..ni kampuni zao anyway
 
Hata kwenye free market tunahitaji some sort of regulations vinginenvyo hawa watu watajifanyia wanavyotaka. Wanaoumia ni raia wa kawaida vigogo, wakuu wa mashirika na vingunge wengine simu zao zinalipiwa aidha na serikali au mashirika yao. Sasa cha kujiuliza hiyo affordable rate ni kwa nani? Kuna vitu vingi tu serikali inaweza saidia toa mwongozo mfano namba za simu kuendelea kuuzwa kama njugu barabarani?
 
Ni kweli kabisa we are now having 7 companies of telecom which are TTCL,BOL,Sasatel,Tigo,Vodacom,Zain & Zantel.

The rate between the same network has go down but it should have gone beyond what they are charging right now.

As to other network only BOL have best rate compared to all other companies.

Only Zantel has come up with a very good offer from BAB KUBWA promotion and many customers of zantel have enjoyed this offer.
 
Unajua TCRA ndiyo wanaotoa leseni za makampuni ya mawasiliano hapa nchini na wao ndiyo wanaotakiwa kufanya monitoring katika hayo makampuni;ina maana wao wamerizika na hiyo hali?Binafsi,siamini kama wamelizika na hiyo hali;kwasababu walikwisha kaa vikao kama mara mbili kwa records ninayoijua mimi kujadili hili lillotwa na mwenzetu hapa jamvi.Sasa cha ajabu katika vikao hivyo muafaka ulikuwa haupatikani na hatimaye ilikuwa inaishia kuvunjika kwa vikao tu.
Nashindwa kuelewa kwanini TCRA wanashindwa kuyadhibiti haya makampuni?!
 
KiuyaJibu nadhani kuna mapungufu au mianya kwenye hayo masharti ya utoaji wa leseni. Kulitakiwa kuwe na misingi mizuri ya kumlinda consumer, taifa na hawa wawekezaji katika hii biashara. Mfano kama hawa watu wangebanwa kuwa na database za wateja, ingepelekea wao kuweka mikakati ya kuwavuta na kuwashika wateja kuhakikisha hawahamii kwingine. Pia ingebidi watoe namba za simu wao wenyewe badala ya kuuzwa vichochoroni. Hii ingepunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la ukwapuaji wa simu, leo kibaka akikwapua simu anakata kona ananunua namba kibandani mchezo umekwisha
 
Lazima watanzania tuwe wa kweli. hakika Serikali ya Tanzania wanaweka kodi nyingi sana kwa haya makampuni. Kuna customer namber charges,frequence charges, royalt fee, telecomm licence etc. Hizi kodo zote zinazotozwa na TCRA kwa niaba ya Serikali ya Tanzania zinasababisha bei ya kupiga simu kupaa.

Ukiangalia hata bajeti ya Tanzania mwaka 2009/2010 pg 79 (v) ii mpaka vii, hivi vyote vinaonyesha Serikali ili kuongeza mapato wanabana sana makampuni ya vinywaji baridi, bia na Simu.

hakika Serikali ya TZ inachukulia simu ni kitu cha hanasa na sio muhimu kwa jamii
 
Jamani msiyalaumu makampuni ya simu serikali yenu inaongoza kwa makodi mengi na makubwa mengine hata ulaziwa hayana mfano halisi leta mzigo wako pale bandarini toka nje halafu kautoe uone mikodi utakayobambikwa so kila sekta imeathirika mtalaumu sana haya makampuni lkn angalieni roots ni nani huko tcra wanabuluzwa tu hawana say hawa
 
Bila kuchukua hatua hizi rate zitaendelea kupanda siku hata siku, huo utitiri wa kodi Barubaru uliouorodhesha umeniacha hoi, mfano hiyo Customer number charge does not make sense to me. Chimunguru badala ya kusema 'nchi yenu' wewe, mimi na wengine tunatakiwa tuone nini cha kufanya ili serikali ipunguze hizi kodi na kuzimonitor hizi kampuni zisijiendee jinsi zinataka.
 
Kwa hiyo mnataka kupiga bure nn wakubwa? Mnataka xtreme ya bureee!!
Ha! Ha! hii ndo halali yenyewe.
 
Back
Top Bottom