mjinishure
Member
- Oct 19, 2012
- 86
- 56
Habari wanajukwaa
Miaka miwili iliyo pita nilibahatika kuanzisha mahusiano na dada mmoja ambae anafanya kazi moja ya benki hapa dar.
Hapo mwanzo mahusiano yetu yalikuwa ya kawaida sana ila siku zilivyozidi ndipo nikagundua kweli huyu dada alikuwa ananipenda. Kama mjuavyo mapenzi yalinoga sana kiasi cha kuwa nampitia kazini kila siku na usafiri wangu kumrudisha kwao
Pia kuna mambo mengi huyu dada alio nisaidia kwani huwa kila akija nilipopanga huwa haulizi akiona kuna mapungufu chumbani au sebeleni unakuta ananunua hakuna siri tena juu ya mshahara wake wala namba za siri za kadi yake ya benki nimekuwa kama mshauri kila mshahara wake uingiapo benki kumueleza namna ya matumizi.
Katika mapenzi nakumbuka aliwahi kufumania sms za mapenzi kwenye simu yangu nakumbuka alilia sana ila alinikalisha na kuniambia kuwa ananipenda sana hata kama hayo mambo nafanya kwa matamanio basi nifanye kwa siri bila yeye kuona kwani huwa anaumia, nilimuomba msamaha na yakaisha
Tatizo limekuja hivi karibuni baada ya kushibana na kuamua nibora tukaoana. Likaja swala la dini mimi ni mkristo na yeye ni mwislamu. Nilimwambia siwezi kuoa mtu mwenye dini tofauti na yangu. Ndipo alipo niambia hakuna tatizo yuko tayari hata kabla sijamuuliza alilijua hilo na atabadilisha.
Upande wa wazazi wake hawataki hata kusikia hii kitu na tayari wamemtisha kutokumtambua kwenye familia yake endapo tu atabadilisha. Nilipo muuliza yeye anaonaje hili alisema nipo tayari kuolewa nawewe, kwani nakupenda sana swala la wazazi potelea mbali.
Juzi nimetumia sms baada ya kupata baadhi ya ushauri toka kwa watu kuwa (nimeamua ni bora tukaheshimu mawazo ya wazazi wetu hivYo naona si sahihi mimi na wewe kuoana) leo nimepigiwa simu na mdogo wake kuwa siku ya pili hajala na analia tu na kazini hakuenda.
Wanajamvi naombeni mnishauri kwa hili janga nililonalo naikumbukwe mimi siwezi badilisha dini
Miaka miwili iliyo pita nilibahatika kuanzisha mahusiano na dada mmoja ambae anafanya kazi moja ya benki hapa dar.
Hapo mwanzo mahusiano yetu yalikuwa ya kawaida sana ila siku zilivyozidi ndipo nikagundua kweli huyu dada alikuwa ananipenda. Kama mjuavyo mapenzi yalinoga sana kiasi cha kuwa nampitia kazini kila siku na usafiri wangu kumrudisha kwao
Pia kuna mambo mengi huyu dada alio nisaidia kwani huwa kila akija nilipopanga huwa haulizi akiona kuna mapungufu chumbani au sebeleni unakuta ananunua hakuna siri tena juu ya mshahara wake wala namba za siri za kadi yake ya benki nimekuwa kama mshauri kila mshahara wake uingiapo benki kumueleza namna ya matumizi.
Katika mapenzi nakumbuka aliwahi kufumania sms za mapenzi kwenye simu yangu nakumbuka alilia sana ila alinikalisha na kuniambia kuwa ananipenda sana hata kama hayo mambo nafanya kwa matamanio basi nifanye kwa siri bila yeye kuona kwani huwa anaumia, nilimuomba msamaha na yakaisha
Tatizo limekuja hivi karibuni baada ya kushibana na kuamua nibora tukaoana. Likaja swala la dini mimi ni mkristo na yeye ni mwislamu. Nilimwambia siwezi kuoa mtu mwenye dini tofauti na yangu. Ndipo alipo niambia hakuna tatizo yuko tayari hata kabla sijamuuliza alilijua hilo na atabadilisha.
Upande wa wazazi wake hawataki hata kusikia hii kitu na tayari wamemtisha kutokumtambua kwenye familia yake endapo tu atabadilisha. Nilipo muuliza yeye anaonaje hili alisema nipo tayari kuolewa nawewe, kwani nakupenda sana swala la wazazi potelea mbali.
Juzi nimetumia sms baada ya kupata baadhi ya ushauri toka kwa watu kuwa (nimeamua ni bora tukaheshimu mawazo ya wazazi wetu hivYo naona si sahihi mimi na wewe kuoana) leo nimepigiwa simu na mdogo wake kuwa siku ya pili hajala na analia tu na kazini hakuenda.
Wanajamvi naombeni mnishauri kwa hili janga nililonalo naikumbukwe mimi siwezi badilisha dini