utukufu mwanjisi
JF-Expert Member
- Aug 19, 2017
- 2,830
- 2,417
Habarini hapa jukwaani
Katika mnyukano ambao unaendelea katika mitandao ya kijamii kati ya watu ambao wamewahi kushika nyadhifa kubwa katika Chama Changu cha Mapinduzi, ambapo ni ndugu Humphrey Polepole na Ndugu Nape Nnauye. Ni kili kwamba hakuna jambo ambalo linatokea kwa bahati mbaya katika Chama chetu narudia tena hakuna.
KABLA ya kuendelea, lazima niwaambie ya kwamba ninaeandika hii thread hapa ni Mwana CCM ASILIA na sijawahi kuogopa kusema hivyo hata kipindi cha Mwenyekiti wangu aliefariki hapo karibuni, ukitaka kulijua hilo pitia thread zangu zote zilizopita hapo awali.
TUENDELEE, wengi wenu hapa jukwaani na huko mitandaoni mmemuona ndugu Nape kama amekosa busara katika mchakato mzima wa kitu kinachoendelea kwa sasa kwa chama chetu, lakini niwe wazi kuwa Nape anajua nini anakifanya na mnayoyaona leo kipo katika mahesabu na mikakati ya hapo mbeleni.
HIVYO, nilitaka kuwashauri tu kuwa ndugu wapinzani mngeendelea na shughuli zingine maana ngoma inayochezwa na watu wa CCM kwenu nyinyi ni kubwa sana na hamtaweza kujua midundo yake abadani hata tuliomo ndani ya chama baadhi ya midundo inatushinda, sasa mtaiweza nyinyi mlio nje ya chama.
CCM NI DUBWANA KUBWA LINAJUA NINI LINAKIFANYA NA KWA WAKATI GANI.
Katika mnyukano ambao unaendelea katika mitandao ya kijamii kati ya watu ambao wamewahi kushika nyadhifa kubwa katika Chama Changu cha Mapinduzi, ambapo ni ndugu Humphrey Polepole na Ndugu Nape Nnauye. Ni kili kwamba hakuna jambo ambalo linatokea kwa bahati mbaya katika Chama chetu narudia tena hakuna.
KABLA ya kuendelea, lazima niwaambie ya kwamba ninaeandika hii thread hapa ni Mwana CCM ASILIA na sijawahi kuogopa kusema hivyo hata kipindi cha Mwenyekiti wangu aliefariki hapo karibuni, ukitaka kulijua hilo pitia thread zangu zote zilizopita hapo awali.
TUENDELEE, wengi wenu hapa jukwaani na huko mitandaoni mmemuona ndugu Nape kama amekosa busara katika mchakato mzima wa kitu kinachoendelea kwa sasa kwa chama chetu, lakini niwe wazi kuwa Nape anajua nini anakifanya na mnayoyaona leo kipo katika mahesabu na mikakati ya hapo mbeleni.
HIVYO, nilitaka kuwashauri tu kuwa ndugu wapinzani mngeendelea na shughuli zingine maana ngoma inayochezwa na watu wa CCM kwenu nyinyi ni kubwa sana na hamtaweza kujua midundo yake abadani hata tuliomo ndani ya chama baadhi ya midundo inatushinda, sasa mtaiweza nyinyi mlio nje ya chama.
CCM NI DUBWANA KUBWA LINAJUA NINI LINAKIFANYA NA KWA WAKATI GANI.