mwikumwiku
Senior Member
- Jul 15, 2011
- 153
- 35
Kwa namna mambo yanavyoenda juu ya ushughulikiaji
wa mgogoro baina ya wizara ya afya na madaktari ni
wazi anayeumia ni mwananchi Wa kawaida ambaye hana haki wala uwezo wa kwenda kwa matibabu nje ya nchi.
Kinachoonekana wazi ni kwamba viongozi wa wizara wameshindwa kushughulikia mgogoro huo na kinachoendelea ni kuendelea kuitwika lawana serikali ya Kikwete....
Mh. Kikwete, Mh. Waziri Mkuu take action... wasaidieni wananchi walala hoi wanaotibiwa kwenye hospitali zetu hizi za kilala hoi ambazo ninyi hamtibiwi! Wananchi wakimbilie wapi? Wamlilie nani!
Kwa maoni yangu, huu ndo wakati muafaka kwa Rais wetu kuonyesha makucha yake... piga chini viongozi wanaoendele kudhoofisha serikali yako! Utaendele mpaka lini kuwabeba viongozi wasiobebeka kama hawa?
Hivi hakuna wabunge wengine wanaoweza kufanya kuongoza wizara ya afya zaidi ya hawa waliopo? Hivi haku mtumishi mwingine anayeweza kuwa KM zaidi ya huyu aliyopo? Hivi hakuna daktari mwingine anayeweza kuwa
mganga mkuu zaidi ya huyu aliyopo?
Eneo la tabibu ni moja ya maeneo nyeti sana! Ni eneo linalogusa maisha ya wananchi ya kila siku! Hakuna kitu kimuumiza mwananchi mlala hoi kama kuto kuwa na uhakika na uwepo Wa tiba hata hii ya kilala hoi! Tukimbilie wapi sisi tusio na haki wala uwezo Wa kwenda India kama ninyi!
Kwa nini Mh. Rais unaendelea kuwa na wema wa mshumaa! Kwa nini serikali yako iendelee kuonekana imeshindwa kwa sababu ya viongozi wabovu ambao wapo ndani ya mamlaka yako? Piga chini mawaziri, katibu mkuu na mganga mkuu weka wengine! Hii itasaidia kupeleka signal/sms kwa viongozi wengine wababaishaji kama hawa!
Bila kuchukua maamuzi magumu, serikali yako itaendelea kudhoofika siku hadi siku!
Wananchi tunaumia sana! Fanya kitu fulani ili imani yetu kwako na serikali yako irejee!
wa mgogoro baina ya wizara ya afya na madaktari ni
wazi anayeumia ni mwananchi Wa kawaida ambaye hana haki wala uwezo wa kwenda kwa matibabu nje ya nchi.
Kinachoonekana wazi ni kwamba viongozi wa wizara wameshindwa kushughulikia mgogoro huo na kinachoendelea ni kuendelea kuitwika lawana serikali ya Kikwete....
Mh. Kikwete, Mh. Waziri Mkuu take action... wasaidieni wananchi walala hoi wanaotibiwa kwenye hospitali zetu hizi za kilala hoi ambazo ninyi hamtibiwi! Wananchi wakimbilie wapi? Wamlilie nani!
Kwa maoni yangu, huu ndo wakati muafaka kwa Rais wetu kuonyesha makucha yake... piga chini viongozi wanaoendele kudhoofisha serikali yako! Utaendele mpaka lini kuwabeba viongozi wasiobebeka kama hawa?
Hivi hakuna wabunge wengine wanaoweza kufanya kuongoza wizara ya afya zaidi ya hawa waliopo? Hivi haku mtumishi mwingine anayeweza kuwa KM zaidi ya huyu aliyopo? Hivi hakuna daktari mwingine anayeweza kuwa
mganga mkuu zaidi ya huyu aliyopo?
Eneo la tabibu ni moja ya maeneo nyeti sana! Ni eneo linalogusa maisha ya wananchi ya kila siku! Hakuna kitu kimuumiza mwananchi mlala hoi kama kuto kuwa na uhakika na uwepo Wa tiba hata hii ya kilala hoi! Tukimbilie wapi sisi tusio na haki wala uwezo Wa kwenda India kama ninyi!
Kwa nini Mh. Rais unaendelea kuwa na wema wa mshumaa! Kwa nini serikali yako iendelee kuonekana imeshindwa kwa sababu ya viongozi wabovu ambao wapo ndani ya mamlaka yako? Piga chini mawaziri, katibu mkuu na mganga mkuu weka wengine! Hii itasaidia kupeleka signal/sms kwa viongozi wengine wababaishaji kama hawa!
Bila kuchukua maamuzi magumu, serikali yako itaendelea kudhoofika siku hadi siku!
Wananchi tunaumia sana! Fanya kitu fulani ili imani yetu kwako na serikali yako irejee!