Wanabodi,
Baada ya serikali kuhamishia makao makuu yake jijini Dodoma iliweka wazi kwamba, Jiji la Dar es Salaam lililokuwa makao makuu, sasa ni Jiji la Kibiashara.
Lakini cha ajabu, Jiji la Kibiashara, bado biashara zinafanywa kwa masharti. Mfano; bado baa zinauza pombe kwa muda na kufunga baa kwa masharti ya muda.
Bado maduka makubwa ya kuuza bidhaa mbalimbali, yanafungwa kwa muda wa usiku kucha na kufunguliwa baada ya jua kutoka.
Bado, daladala nyingi zinalala saa tano usiku na kuanza kazi alfajiri.
Namshauri mkuu wa mkoa wetu ambaye si mpaza sauti sana ila ni mtekelezaji, aweke mazingira mazuri ili Jiji liendane na sifa ya Kibiashara.
Endapo biashara zitakesha, daladala zitakesha (automatiki). Endapo baa zitakuwa saa 24, daladala zitakesha (automatiki). Kwa sasa baadhi ya maeneo daladala hazipo usiku kwa sababu hakuna abiria. Watapatikanaje wakati baa saa tano zimefungwa?
Abiria watapatikanaje wakati maduka Kariakoo saa moja yanafungwa?
Sifa ya Jiji la Kibiashara ni shughuli zote kuwa wazi kwa saa 24. Hao wafanyabiashara wenye jiji lao, wanasema baishara haina saa.
Ahadi ya biashara hata saa sita usiku. Mchana kutwa wamelala. Ahadi ya biashara hata saa kumi na moja alfajiri, usiku kucha wamelala.
Nakusihi RC tafakari sifa za Jiji kuwa la Kibiashara kisha waandalie mazingira wezeshi. (kidogo niseme Amina).
Baada ya serikali kuhamishia makao makuu yake jijini Dodoma iliweka wazi kwamba, Jiji la Dar es Salaam lililokuwa makao makuu, sasa ni Jiji la Kibiashara.
Lakini cha ajabu, Jiji la Kibiashara, bado biashara zinafanywa kwa masharti. Mfano; bado baa zinauza pombe kwa muda na kufunga baa kwa masharti ya muda.
Bado maduka makubwa ya kuuza bidhaa mbalimbali, yanafungwa kwa muda wa usiku kucha na kufunguliwa baada ya jua kutoka.
Bado, daladala nyingi zinalala saa tano usiku na kuanza kazi alfajiri.
Namshauri mkuu wa mkoa wetu ambaye si mpaza sauti sana ila ni mtekelezaji, aweke mazingira mazuri ili Jiji liendane na sifa ya Kibiashara.
Endapo biashara zitakesha, daladala zitakesha (automatiki). Endapo baa zitakuwa saa 24, daladala zitakesha (automatiki). Kwa sasa baadhi ya maeneo daladala hazipo usiku kwa sababu hakuna abiria. Watapatikanaje wakati baa saa tano zimefungwa?
Abiria watapatikanaje wakati maduka Kariakoo saa moja yanafungwa?
Sifa ya Jiji la Kibiashara ni shughuli zote kuwa wazi kwa saa 24. Hao wafanyabiashara wenye jiji lao, wanasema baishara haina saa.
Ahadi ya biashara hata saa sita usiku. Mchana kutwa wamelala. Ahadi ya biashara hata saa kumi na moja alfajiri, usiku kucha wamelala.
Nakusihi RC tafakari sifa za Jiji kuwa la Kibiashara kisha waandalie mazingira wezeshi. (kidogo niseme Amina).