Ushauri: Wanawake jengeni utamaduni wa kutembea na japo kanga moja kwenye pochi zenu.

Dah Smile...naona umeuchukulia huu ushauri ulitolea kama fedheha kwa wanawake...kumbuka maudhui ya ushauri yamekuja baada ya tukio zima lililotokea. hakutoa huu ushauri kwa nia mbaya..kikubwa hapa ni kumpongeza kwa ujasiri wake na utu na moyo wa huruma.ondoa jazba.
Kwani mwanaume akizimia inakuaje hzo ni ajali tu na yaweza mtokea hata mwanaume
anzeni nyie kutembea na kanga
upuuuzi tu huo
 
Hivi smile kuna mahali mwanamke amebebeshwa lawama hapa? Nijuavyo mimi imeletwa kama ushauri, na ushauri huwa unatolewa bure kuukubali au kuukataa ni haki yako ya msingi....ila pia sio lazima utoe lugha chafu, kama wewe huoni umuhimu wa kubeba kanga au mtandio kwenye handbag yako ni sawa na ungeweza kutufundisha na sie washamba tunaobeba mbadala wake ni nini. Jf ni mahali pa kufundishana na kujifunza hivyo mie binafsi ningefurahi kusikia mwenzetu una mbadala gani..

Mkuu hakuna haja ya kubishana na majuha.
 
Mko mbali kabisaaaaaaaaaa na maana ya mtoa mada. Yaani mmeelewa kama vile kasema "kutembea na khanga ndio njia pekee ya kujikinga na janga kama hilo". Too low understanding!!


Kaielezea khanga kama mojawapo ya njia ambayo ingesaidia, kati ya njia nyingi ambazo zingeweza kutumika. Ndio maana ktk mkasa huo walimuomba khanga mwanamke mwingine ili kumsitiri mwenzao. So its an advice. You can follow it or not.
Tumshukuru ameokoa maisha ya mwenzetu, hasa mwanamke na pia kasaidia kufanikisha kumsitiri mwili wake.


Ndio tatizo la mtu kujidai anaelewa mtu alicho maanisha kuliko mwenyewe aliyeandika,wewe ndiye usiye elewa.

Sizungumzii hilo tukio peke yake nazungumzia dhana nzima ya kutembea na kanga na
kwamba eti kanga sijui itakusitiri,sijui lazima
mwanamke kutembea nayo,sijui mwanamke akijitambua lazima abebe kanga na bla bla kama hizo hazina maana yoyote,labda ingekuwa inanihakikishia usalama wa fedha zangu,simu yangu na vitu vyangu kwa ujumla.
 
Kwani mwanaume akizimia inakuaje hzo ni ajali tu na yaweza mtokea hata mwanaume
anzeni nyie kutembea na kanga
upuuuzi tu huo

Sio wote wanaosema bwana bwana,watakaoingia katika ufalme wa mbinguni.
 
daah mada iko staight forward lakini imefanywa kama sayansi ya kurusha roketi angani...
Ngoja nilale labda kwanza
 
daah mada iko staight forward lakini imefanywa kama sayansi ya kurusha roketi angani...

Ngoja nilale labda kwanza

Sayansi nimeitumbukiza kidogo tu na nimeirahisisha kwa kiwango kikubwa ili ieleweke na wote kwa madhumuni ya kuleta mtiririko mzuri wa tukio bila kupoteza maudhui.
 
Sayansi nimeitumbukiza kidogo tu na nimeirahisisha kwa kiwango kikubwa ili ieleweke na wote kwa madhumuni ya kuleta mtiririko mzuri wa tukio bila kupoteza maudhui.
ni kweli mada ipo straight mleta mada issue ni kwamba kuna watu hawajui kujenga hoja zao kwenye kuchangia wanapenda malumbano
mimi nilikukosea kwamba issue sio mwanamke kubeba khanga maana hata alipozimia yule mdada hata kama angekuwa na khanga kwenye mkoba wake unadhani ingeonekana? maana huo mkoba sidhani kama kuna mtu mstaarabu anayeweza kufungua mkoba wa mtu.
au labda tuseme wanawake wawe wanavaa khanga mida yote maana mi kutembea nayo kwenye mkoba sioni kama itasaidia mkuu
nadhani cha kusema ungeshauri wadada wawe wanavaa nguo ambayo hata kama atakumbana na maswaibu njiani isiwe ni aibu kwake
hayo ni mawazo yangu simlazimishi mtu kuyakubali
ni vema watu wakajifunza jinsi ya kuchangia hoja na sio kutafuta ugomvi humu
 
Hongera sana mkuu. Tunategemea great thinkers wote wawe na moyo kama wa kwako. Vp wakati wa CPR, ulikula denda?
 
Kwani mwanaume akizimia inakuaje hzo ni ajali tu na yaweza mtokea hata mwanaume
anzeni nyie kutembea na kanga
upuuuzi tu huo

Vipochi vyenyewe hivi vipima joto, khanga itakaa wapi, na wanja je, na lipshine?

Anyway, Hongera sana kwa kuokoa maisha ya mdada... ungeandika note ukampa umwambie ajiunge JF huku angejifunza mambo mengi, including ushauri wako. Ubarikiwe
 
mkuu mimi siwezi kujitafutia umaarufu jf ror what? Nadhani kwa commet yako hii wewe ndo unaonekana mjinga zaidi
kama ni lazima mwanamke atembe na kanga ingekuwa imewekwa iyo sheria kwenye huduma ya kwanza
mimi kwangu sioni kama ni muhimu wala sitokaa nione ni muhimu kamwe,kuna njia nyingi za kukabiliana na majanga mkuu.sio kila lawama mnambebesha mwanamke khaaaaaaaaaa

No hard feelings babe, just keep your smile broader.
 
Vipochi vyenyewe hivi vipima joto, khanga itakaa wapi, na wanja je, na lipshine?

Anyway, Hongera sana kwa kuokoa maisha ya mdada... ungeandika note ukampa umwambie ajiunge JF huku angejifunza mambo mengi, including ushauri wako. Ubarikiwe

Hahahaaaaaaa uwiiiii kuna watu mmepinda humu ndani duuuh!
 
Mimi nataka kujua yule dada mliyemwazima khanga yake je mlirudisha? au baada ya nafuu kubwa huyo kisura alishuka nayo? Hilo ni la kwanza na la pili ni hili " Siyo khanga kwenye mkoba mimi nafikiri waanze na kuwa na Khanga ndani. yaani nyumbani. sasa nyumbani hawana ndo wanaweza kuwa nazo kwenye mkoba? Asante kwa somo hili zuri."
 
Back
Top Bottom