Ushauri: Wanawake jengeni utamaduni wa kutembea na japo kanga moja kwenye pochi zenu.

Daaah
Sikutegemea kuona comment ya hivi, tena ya mwanamke :shock:

Wakati mwingine unaweza kudhani watu wanatumia mbinu ya kujifanya wajinga ili kujipatia umaarufu humu, lakini ndo tunawaona wajinga kweli hivyo.
 
Asante kwa ushauri, kanga ingemsaidiaje na hana fahamu, ingejitoa kwenye begi au. Mimi nasema waache kuiga mila si zao, wavae mavazi ya heshim full stop.
 
hongera kwa moyo huo lakini hata angekuwa na kanga asingeweza kujisetiri mwenyewe
 
hongera kwa moyo huo lakini hata angekuwa na kanga asingeweza kujisetiri mwenyewe
Sasa hapo ilitakiwa itumike tu busara ya walokuwapo hapo, mbona simu waliitoa ili waqaailiane na jamaa zake?
Hebu assume labda angekufa, si wangepekua tu mkopa walau kupata vitambulisho?
Hapakuwa na ugumu hapo, labda kama walifungua na wakaikosa.
 
Ni ushauri tu kwa akina dada:
Leo nikiwa njiani kuelekea kwenye deiwaka kulitokea jambo ambalo kidogo ni la kusikitisha.
Akiwa kwenye daladala ambayo ilijaza kupita kiasi dada mmoja alianguka ghafla ndani ya gari hiyo. Wakati huo daladala hiyo ilikuwa imesimama kwenye foleni. Basi konda pamoja na abiria wengine waliokuwemo humo wakamsaidia kumtoa dada huyo na kumlaza pembezoni mwa barabara.

Kimavazi, dada yule alikuwa amevaa kitopu kifupi kinachobana sana pamoja na kimini.
Kutokana na tukio lenyewe lilivyotokea wakati wa kumbeba kwa kweli ilikuwa kama vile yuko mtupu (try to imagine). Basi watu waliokuwa karibu ilibidi kila mtu aanze kusema lake (hasa kuhusiana na mavazi). Wengi walilaumu kuwa akina dada wa siku hizi wanavaa nguo zinazowashika mwili lakini kwa nini wanashindwa kuweka japo kaupande kamoja ka kanga ili kiwasetiri pindi watakapopata emergence. Walikuwepo pia akina mama ambao nao walishiriki katika lawama hizo dhidi ya "mabinti" zao.

Wakati huo mimi pia nilikuwa karibu na tukio. Dada yule ilikuwa kama vile hapumui. Basi nikajaribu kuwashauri wale watu ambao walikuwa wamejikita zaidi katika kulaumu kwamba kwa wakati huo lawama haikuwa kitu cha muhimu. Badala yake tujikite katika kuhakikisha kuwa tunaokoa maisha ya binti yule huku tukihakikisha kuwa tunamsetiri utu wake. Kitu cha kwanza nilimuomba mama mmoja ambaye alikuwa amejifunga kanga atuazime kanga moja tumsetiri. Mama alikubali.

Wakati huo dada mmoja alikuwa akimpepea kwa kitambaa chepesi. Mimi niligundua kuwa hiyo isingesaidia kitu kama nitakavyoeleza hapa chini.
Kwa kuwa dada yule ali-faint katika gari ambayo ilikuwa imejaa pomoni ni dhahiri kuwa alikosa oxygen ya kutosha hivyo moyo wake kushindwa kufanya kazi sawasawa na kupelekea ubongo kukosa oxygen ya kutosha. Kitabibu, inasadikika kuwa ubongo ukikosa oxygen ya kutosha mtu anaweza akapoteza maisha ndani ya dakika 5.

Kwa kuwa mimi nina idea ya huduma ya kwanza nikaona si vibaya nikampatia yule dada huduma ya kwanza kwa kadri ninavyoweza. Kitu cha kwanza nilijitambulisha kwa watu ambao sasa walikuwa wamejaa kumzunguka yule dada bila msaada wowote na kuwaeleza kuwa ninayo mafunzo ya huduma ya kwanza.
Baada ya hapo nikamfanyia kitu kinaitwa Cardio-Pulmonary Rescusitation (CPR) kwa ajili ya kuustua moyo wake na kumwongezea oxygen. Wakati huo nilimuomba jamaa mmoja aende kutoa taarifa kwa Traffic Police ambao walikuwa upande wa pili wa barabara wakiangalia usalama wa magari. Nilimpatia jamaa mwingine achukue simu ya yule dada na ajaribu ku-search namba za jamaa zake wa karibu na kuwataarifu juu ya mkasa huo.
Mimi niliendelea na CPR hadi nilipohakikisha kuwa yule dada amepata nafuu nikamweka kwenye "Recovery Position" halafu nikamkabidhisha kwa akina mama wawili ambao walikuwepo eneo la tukio na walikuwa wakitoa msaada wa hapa na pale then na mimi nikawahi kwenye "kijiwe changu cha kuponda kokoto".

Nikiwa njiani nilijaribu kutafakari mambo mengi sana kichwani lakini kikubwa ambacho niliona si vibaya nikawashauri akina dada:
Jamani, pamoja na kupiga mapigo makali ya viwalo si vibaya kwenye hayo mapochi yenu mkaweka japo kaupande ka kanga. Huwezi jua njiani!

Note: Kisa hiki kimetokea kweli leo asubuhi kama nilivyokielezea.

Big Up Mkuu. Acha kuponda kokoto, tafuta kibarua kingine kizuri.
 
Umenikumbusha mbali , kuna siku tulienda kumwona jamaa mahabusu sasa tuliongozana na mdada mmoja kapiga trousers ya jeans , wakati tumeruhusiwa kwenda kumuona ghafla askari wa kike akamwita yule dada na kumwambia ajifunge kanga maana kule mahabusu ni kwa wanaume. Bahati nzuri yule dada alichukua kanga nyumbani kwake na kuiweka kwenye pakacha lakeh ivyo ilimsaidia wakati ule. Ni muhimu kuwa na kanga ama kitenge kwa akina sisters.
 
Hongera sana mkuu, Mungu akubariki sana kwa kujitolea.
Pia nahisi wamakusikia hao wasiotembea na kanga wala mitandio.
 
wakati mwingine unaweza kudhani watu wanatumia mbinu ya kujifanya wajinga ili kujipatia umaarufu humu, lakini ndo tunawaona wajinga kweli hivyo.
mkuu mimi siwezi kujitafutia umaarufu jf ror what? Nadhani kwa commet yako hii wewe ndo unaonekana mjinga zaidi
kama ni lazima mwanamke atembe na kanga ingekuwa imewekwa iyo sheria kwenye huduma ya kwanza
mimi kwangu sioni kama ni muhimu wala sitokaa nione ni muhimu kamwe,kuna njia nyingi za kukabiliana na majanga mkuu.sio kila lawama mnambebesha mwanamke khaaaaaaaaaa
 
mkuu mimi siwezi kujitafutia umaarufu jf ror what? Nadhani kwa commet yako hii wewe ndo unaonekana mjinga zaidi
kama ni lazima mwanamke atembe na kanga ingekuwa imewekwa iyo sheria kwenye
huduma ya kwanza



mimi kwangu sioni kama ni muhimu wala sitokaa nione ni muhimu kamwe,kuna njia nyingi za kukabiliana na majanga mkuu.sio kila lawama mnambebesha mwanamke khaaaaaaaaaa


Kanga ya nini?Mwingine anabeba ili na yeye aonekane mwanamke kwa vile kaaminishwa kubeba kanga ndio kutamfanya aonekane mwanamke na hasa mbele ya wanaume.

Ingekuwa kanga itakuzuia na wezi au matapeli hapa bongo kweli,vinginevyo hata mwanaume anatakiwa ajisitiri.
 
Asante mkuu. kadri mlivyowatendea hao mmenitendea mimi. maneno ya Mungu hayo. wewe utabarikiwa. kanga au mtandio ni wa muhimu wadada.
 
Mkeshaji, kanga/ mitandio tunabeba lkn kwa yaliyomukta huyo dada hata kama angekuwa na kanga angeivaa saa ngapi na tukio limetokea ghafla, ubarikiwe kwa kuokoa maisha ya bidada
 
kwa mwanamke khanga si kwa ajili ya kufunikwa ukizimia tu, wanawake tuna mambo mengi na ukiwa na khanga utasitirika, nadhani mleta mada ana nia safi kabisa sioni sababu ya kuwaambia na wanaume nao wavae khanga! Wakati mwingine tuko too sensitive unnecessarily!

SL rudisha ule upande wa kanga yangu iloandikwa 'utamu wa shoki shoki nyama peke yake'....ile ingine nakuachia

Pengine wengine wangeelewa zaidi ningeandika hivi:
"Faida za kanga kwa mwanamke ni hizi:
1......
2.....
3.....

Na hasara za kutokuwa na kanga kwa mwanamke ni hizi:
1....
2..... n.k."

Bahati nzuri incidence hii imetokea ndo maana nimeweza/nimekumbuka kuunganisha na matumizi ya kanga kwa mwanamke.
Mwingine angeweza kuelezea maudhui kama haya kwa maneno mengine na kisa kingine penginepo.
 
::: Cardio-Pulmonary U-rescusitation (CPU) :::
kumbe mi ni huduma ya kwanza . . . . :lol:

Mkuu naona umepiga kona halafu kabla haijaguswa na mtu ukawahi kufunga mwenyewe :lol:
 
  • Thanks
Reactions: CPU
Wakati mwingine unaweza kudhani watu wanatumia mbinu ya kujifanya wajinga ili kujipatia umaarufu humu, lakini ndo tunawaona wajinga kweli hivyo.

Kwahiyo ameona kutumia busara na hekima hawez kuwa maarufu?
 
mkuu mimi siwezi kujitafutia umaarufu jf ror what? Nadhani kwa commet yako hii wewe ndo unaonekana mjinga zaidi
kama ni lazima mwanamke atembe na kanga ingekuwa imewekwa iyo sheria kwenye huduma ya kwanza
mimi kwangu sioni kama ni muhimu wala sitokaa nione ni muhimu kamwe,kuna njia nyingi za kukabiliana na majanga mkuu.sio kila lawama mnambebesha mwanamke khaaaaaaaaaa
Hivi smile kuna mahali mwanamke amebebeshwa lawama hapa? Nijuavyo mimi imeletwa kama ushauri, na ushauri huwa unatolewa bure kuukubali au kuukataa ni haki yako ya msingi....ila pia sio lazima utoe lugha chafu, kama wewe huoni umuhimu wa kubeba kanga au mtandio kwenye handbag yako ni sawa na ungeweza kutufundisha na sie washamba tunaobeba mbadala wake ni nini. Jf ni mahali pa kufundishana na kujifunza hivyo mie binafsi ningefurahi kusikia mwenzetu una mbadala gani..
 
mkuu mimi siwezi kujitafutia umaarufu jf ror what? Nadhani kwa commet yako hii wewe ndo unaonekana mjinga zaidi
kama ni lazima mwanamke atembe na kanga ingekuwa imewekwa iyo sheria kwenye huduma ya kwanza
mimi kwangu sioni kama ni muhimu wala sitokaa nione ni muhimu kamwe,kuna njia nyingi za kukabiliana na majanga mkuu.sio kila lawama mnambebesha mwanamke khaaaaaaaaaa


Kanga ya nini?Mwingine anabeba ili na yeye aonekane mwanamke kwa vile kaaminishwa kubeba kanga ndio kutamfanya aonekane mwanamke na hasa mbele ya wanaume.

Ingekuwa kanga itakuzuia na wezi au matapeli hapa bongo kweli,vinginevyo hata mwanaume anatakiwa ajisitiri.

Mko mbali kabisaaaaaaaaaa na maana ya mtoa mada. Yaani mmeelewa kama vile kasema "kutembea na khanga ndio njia pekee ya kujikinga na janga kama hilo". Too low understanding!!

Kaielezea khanga kama mojawapo ya njia ambayo ingesaidia, kati ya njia nyingi ambazo zingeweza kutumika. Ndio maana ktk mkasa huo walimuomba khanga mwanamke mwingine ili kumsitiri mwenzao. So its an advice. You can follow it or not.
Tumshukuru ameokoa maisha ya mwenzetu, hasa mwanamke na pia kasaidia kufanikisha kumsitiri mwili wake.
 
Hivi smile kuna mahali mwanamke amebebeshwa lawama hapa? Nijuavyo mimi imeletwa kama ushauri, na ushauri huwa unatolewa bure kuukubali au kuukataa ni haki yako ya msingi....ila pia sio lazima utoe lugha chafu, kama wewe huoni umuhimu wa kubeba kanga au mtandio kwenye handbag yako ni sawa na ungeweza kutufundisha na sie washamba tunaobeba mbadala wake ni nini. Jf ni mahali pa kufundishana na kujifunza hivyo mie binafsi ningefurahi kusikia mwenzetu una mbadala gani..

I like and love this comment!
 
hongera sana mkeshaji kwa moyo wako huo wa huruma. Umenikumbusha pale ud udasa kuna mdada alishuka kwenye daladala na kipedo chake cha kaki ,kilikuwa kimelowa damu ya bleed kuanzia hapo mbele hadi nyuma kwenye makalio,yaani full red, ilikuwa ni aibu tupu. Mbaya zaidi hakuwa na kanga wala mtandio, ilibidi akomae hivyo hivyo hadi hall 5.
 
Back
Top Bottom