Ushauri: Wabunge Viti Maalum wapigiwe kura kwa uchaguzi utakaohusisha wanawake pekee ili kuweka uwazi wa upatikanaji wao

The lost

JF-Expert Member
Jul 3, 2017
2,695
8,209
Wakuu taifa letu linatekeleza maadhimio kadhaa kuhusiana na mikataba mbalimbali ya usawa wa kijinsia. Moja ya mikataba hiyo ni pamoja na ule wa kuhakikisha uwepo wa usaa katika vyombo vya maamuzi.

Bunge letu limeridhia kuwepo kwa wabunge wa viti maalum lakini upatikanaji wao umekuwa wa hisani hivyo kupelekea kuwa watu wasio na msimamo dhabiti wa kimaamuzi na kihoja bungeni. Pendekezo langu ni hili;

1. Wabunge viti maalumu wapigiwe kura kwenye majimbo yao kwa uchaguzi utakohusisha wanawake pekee.

2. Wabunge viti maalum wasigawiwe kwa mfumo wa vyama vya siasa ila wagombee kama wagombea wengine kupitia vyama vyao vya kisiasa kwa utaratibu wa wagombea wote katika kundi hili kuwa wanawake.

3. Viti maalumu vitambue uwepo wa walemavu na vijana na wasipungue watu 20 kutoka katika makundi hayo, mathalani katika bunge letu kuna wabunge 113 viti maalumu hivyo angalau wabunge 15 wawe ni kutoka kundi la wenye ulemavu na 15 kutoka kwa vijana na mama wajane, wazee na wafugaji.
 
Kuhusu Maamuzi ya Kupata Wabunge na Ubunge hiyo ni Kazi ya CCM maana ndio wenye Hati Miliki ya Nchi Hii. Kilichotoke October, 2020 Kikufungue Macho Maana so far Hakuna Kilichobadirika, Watawala ni wale wale CCM ni Ile ile Mifumo na Katiba ni Ile ile. Tofauti ni Moja tu, Wamepungua Idadi.
 
Hoja yako nzuri, shida itakuwa hela za rushwa hawa watapata wapi?

Vilema,

Wajane/wagane,

Vijana,

Wakulima,(ikiwa wanaibiwa kwa rombesa).

Wafugaji
 
Hoja YAKO ni ya msingi Sana. Tena ikibidi hao Wanawake sionlazma wawe na vyama. Yani inasikitisha Sana unakuta wabunge Wanawake wapo bungeni wanauza sura na kujiremba tu, wakati Wanawake wa Tanzania Wana changamoto kibao,, hawana wa kuwasemea.
NYINYI WANAWAKE HUKO BUNGENI SEMEENI WANAWAKE, WATETEENI, MSAIDIENI MAMA SAMIA MSIMWANGUSHE, ACHENI UBISHOO.
 
Wakuu taifa letu linatekeleza maadhimio kadhaa kuhusiana na mikataba mbalimbali ya usawa wa kijinsia. Moja ya mikataba hiyo ni pamoja na ule wa kuhakikisha uwepo wa usaa katika vyombo vya maamuzi.

Bunge letu limeridhia kuwepo kwa wabunge wa viti maalum lakini upatikanaji wao umekuwa wa hisani hivyo kupelekea kuwa watu wasio na msimamo dhabiti wa kimaamuzi na kihoja bungeni. Pendekezo langu ni hili;

1. Wabunge viti maalumu wapigiwe kura kwenye majimbo yao kwa uchaguzi utakohusisha wanawake pekee.

2. Wabunge viti maalum wasigawiwe kwa mfumo wa vyama vya siasa ila wagombee kama wagombea wengine kupitia vyama vyao vya kisiasa kwa utaratibu wa wagombea wote katika kundi hili kuwa wanawake.

3. Viti maalumu vitambue uwepo wa walemavu na vijana na wasipungue watu 20 kutoka katika makundi hayo, mathalani katika bunge letu kuna wabunge 113 viti maalumu hivyo angalau wabunge 15 wawe ni kutoka kundi la wenye ulemavu na 15 kutoka kwa vijana na mama wajane, wazee na wafugaji.
Wakamuwakilishe nani ?
 
Back
Top Bottom